Naliona anguko la makampuni ya bia na biashara zinazotegemea uuzaji wa bia na aina zote za vilevi

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
46,982
144,306
Kama kweli serikali itaamua kufuta posho za watumishi wa umaa na kudhibiti baadhi ya Taasisi za serikali zilizokuwa na mamlaka ya kujipangia mishahara na posho kupitia bodi za mashirika hayo,eneo mojawapo litakaloathirika sana na uamuzi huu ni uuzaji wa bia na aina nyingine ya vilevi katika mabaa,grocery,n.k pamoja na kampuni zinazojihusisha na utengenezaji na usambazaji wa vinywaji hivi.

Baada ya serikali kuzuia safari za watumishi,semina,washa,mikutano na makongamano,watu wengi uwezo wao kununua vinywaji(pombe) ulipungua na uhudhuriaji katika mabaa mbalimbali ulishuka na wengi walimudu kwenda bar tarehe za mwisho wa mwezi tofauti na walivyokuwa wamezoea hapo awali.

Ni ukweli kuwa baada ya vikao vya kuhudhuria semina,washa,makongamano,mikutano,n.k mida ya jioni watumishi hawa huhamia kwenye mabaa kunywa wakitumia posho za vikao na perdiem zao.

Kwa wale wanaopata posho za kila mwezi nao hali ni hivyo hivyo kwani kila wakipata posho yao baadhi huenda bar na ku-spend maisha yaende ila na hawa sasa posho yao ndio hiyo hatujui kama itaendelea kutolewa au laa kwa mujibu wa marekebisho ambayo serikali inakusudia kuyafanya.

Hivyo basi,kama posho katika hizi Taasisi ambazo watumishi wake bado wanapokea zitasitishwa, Mashirika na Taasi ambazo zilizokuwa na mamlaka ya kujipangia bajeti zake na kujiendesha zenyewe bila kuingiliwa na serikali nazo zitanyang'anywa mamlaka hayo na hivyo kulazimika kupunguza safari na posho za watumishi wake,n.k,sioni ni wangapi watakaomudu kuendelea kwenda bar na kuagiza vinywaji zaidi ya kusubiri mwisho wa mwezi na hapa itategemea na madeni aliyonayo mtaani na kwenye salary slip yake(kama alikopa benki,n.k).

Posho hizi ndio zilikuwa zinasaidia watumishi kufukia mashimo(madeni ya mabenki,saccos,n.k)na kuwawezesha watumishi hawa kuhudhuria bar ila sasa ndio hizo nazo taratibu zinaota mbawa.

Uamuzi wa serikali wa kutoongeza mishahara,kuzuia safari ,mikutano, washa,makongamano,n.k na sasa kutaka kufuta hata baadhi ya posho zilizopo kisheria katika baadhi ya mashirika na Taasisi za umma, utakwenda kuathiri mapato ya makampuni ya bia na mwisho wa siku serikali nayo itaathirika kwa kukosa mapato yatakonayo na kodi ya kuuza vinywaji hivi.

Kama kweli sekta binafsi zinayumba kama tunavyosikia,serikalini nako tight,wafanyabiashara nao lazima wayumbe kwasababu watumishi hawa ndio wataje wao.

Sasa kama mtumishi wa umaa amebanwa,wa sekta binafsi nae hana kitu au amekuwa jobless na mfanyabiashara nae kipato chake kimeshuka,sioni uwezekano wa biashara ya vinywaji kuongezeka zaidi ya kupungua na kupelekea serikali kukosa mapato.

Aliezoea kunywa bia 5 sasa atalazimika kunywa bia 2 ama kuacha kabisa tofauti na mahitaji mengine ya nyumbani ambayo ni ya lazima(sio anasa).

Hii itakuwa ni moja ya athari ya kubana watumishi ambayo kwa sasa inaweza isionekane ila ni swala la muda tu kabla madhara yake hayajaanza kuonekana.

Pamoja na yote hayo,msisahau na sheria ya kuzuia watu kunywa pombe kabla ya saa 10 jioni, sheria ambayo imeanza kutekelezwa katika awamu hii ili watu wafanye kazi.

Lingine la kuzingati ni ukweli kuwa watu wengi huwa hawaendi baa peke yao bali hufuatana na ama mke,mchumba,kimada,rafiki,ndugu,jamaa n.k, hivyo kipato cha mtu mmoja tu kina mchango mkubwa sana katika biashara hii ya vilevi kuliko tunavyofikiri.
 
Unachoongea kina ukweli kiasi chake ila vilevile kuna watumishi wa baadhi ya mashirika posho zao zitaongezeka na vivyo hivyo kwa wale wanaokula posho nono zitapungua.

Cha muhimu ni kuondoa mamlaka ya taasisi kujipangia posho yenyewe, lazima kutakuwa na changamoto ila baada ya muda utaratibu utanyooka tu.
 
Kama kweli serikali itaamua kufuta posho za watumishi wa umaa na kudhibiti baadhi ya Taasisi za serikali zilizokuwa na mamlaka ya kujipangia mishahara na posho kupitia bodi za mashirika hayo,eneo mojawapo litakaloathirika sana na uamuzi huu ni uuzaji wa bia na aina nyingine ya vilevi katika mabaa,grocery,n.k pamoja na kampuni zinazojihusisha na utengenezaji na usambazaji wa vinywaji hivim

Baada ya serikali kuzuia safari za watumishi,semina,washa,mikutano na makongamano,watu wengi uwezo wao kununua vinywaji(pombe) ulipungua na uhudhuriaji katika mabaa mbalimbali ulishuka na wengi walimudu kwenda bar tarehe za mwisho wa mwezi tofauti na walivyokuwa wamezoea hapo awali.

Watumishi ambao walikuwa na nafuu kidogo ni wale ambao katika Taasisi wanazofanya kazi bado walikuwa wanapata posho ya katikati ya mwezi (kama vile polisi, mageraza, n.k) watumishi ambao mishahara yao iko juu,mashirika yao hayategemei OC kutoka serikali kujiendesha,n.k.
Hivyo basi,kama posho katika hizi Taasisi ambazo watumishi wake bado wanapokea posho hizi zitasitishwa, Mashirika na Taasi ambazo zilizokuwa na mamlaka ya kujipangia bajeti zake na kujiendesha zenyewe bila kuingiliwa na serikali nazo zitanyang'anywa mamlaka hayo na hivyo kulazimika kupunguza safari na posho za watumishi wake,n.k,sioni ni wangapi watakaomudu kuendelea kwenda bar na kuagiza vinywaji zaidi ya kusubiri mwisho wa mwezi na hapa itategemea na madeni aliyonayo mtaani na kwenye salary slip yake(kama alikopa benki,n.k).

Posho hizi ndio zilikuwa zinasaidia watumishi kufukia mashimo(madeni ya mabenki,saccos,n.k)na kuwawezesha watumishi hawa kuhudhuria bar ila sasa ndio hizo nazo taratibu zinaota mbawa.

Uamuzi wa serikali wa kutoongeza mishahara,kuzuia safari ,mikutano, washa,makongamano,n.k na sasa kutaka kufuta hata baadhi ya posho zilizopo kisheria katika baadhi ya mashirika na Taasisi za umma, utakwenda kuathiri mapato ya makampuni ya bia na mwisho wa siku serikali nayo itaathirika kwa kukosa mapato yatakonayo na kodi ya kuuza vinywaji hivi.

Kama kweli sekta binafsi zinayumba kama tunavyosikia,serikalini nako tight,wafanyabiashara nao lazima wayumbe kwasababu watumishi hawa ndio wataje wao.

Sasa kama mtumishi wa umaa amebanwa,wa sekta binafsi nae hana kitu au amekuwa jobless na mfanyabiashara nae kipato chake kimeshuka,sioni uwezekano wa biashara ya vinywaji kuongezeka zaidi ya kupungua na kupelekea serikali kukosa mapato.

Aliezoea kunywa bia 5 sasa atalazimika kunywa bia 2 ama kuacha kabisa tofauti na mahitaji mengine ya nyumbani ambayo ni ya lazima(sio anasa).

Hii itakuwa ni moja ya athari ya kubana watumishi ambayo kwa sasa inaweza isionekane ila ni swaka la muda tu itakuja kujidhihirisha.

Pamoja na yote hayo,msisahau na sheria ya kuzuia watu kunywa pombe kabla ya saa 10 jioni, sheria ambayo imeanza kutekelezwa katika awamu hii ili watu wafanye kazi.

Watu mna haha nyie mpaka basi...yaani unachagua bia in place ya huduma kwa jamii? Pesa zitakuja kwa njia nyingine kama kuzalisha na kuuza mazao kwakuongeza thamani...binadamu kaumbwa na akili so serikali inapopunguza anasa haina maana kutabakia tu kumesimama tu..inamaana uwezo wa kununua bidha za anasa utapungua lakini substitutes zipo, kule vijijini ambapo kuna bidhaa za msingi kama chakula na vitafunwa kama viazi vitamu, mihogo etc kwahiyo watu wata spend kwenye hizo instead of maandazi za Azam zilizotengeneza monopoly, itabidi agawe soko kwa wale wa kule shamba kwa mfano na mama lishe wa mijini..badala ya kunywa maziwa ya Kenya utatafuta kwa wafugaji wetu ambao huko Malinyi wana mwaga maziwa na kutakuwepo na wafanya biashara wataochukua hiyo fursa ya maziwa hayo kuyaleta mjini...kwahiyo utaonna sasa soko la bidhaa zetu kuongezeka in place ya vile vya nje ambavyo hakuna mwenye nguvu ya kununua kuileta huku...mwisho wa siku bidhaa zetu zitaanza kuongezwa thamani na uchumi wetu kukua baada ya waliochangamka kujenga uwezo zaidi...watu wengi wakiunganishwa kwenye uchumi inamaana wigo wa kodi utaongezeka kwani mifumo ya kodi na mianya ya ukwepaji imepungua hiyo itaziba pengo la budget iliyopatilana through kampuni yetu ya bia iliyo binafsishwa na mashamba yake ya ngano kuachwa kwakua mbia ana maslahi na kwao pia..there we go na mdogo mdogo mpaka uchumi wa kati na hatimaye uchumi mkubwa...mwendo wetu hauwezi kutabirika unaweza kuwa wa haraka au polepole kutokana na mwitikio wa jamii na nguvu ya kiongozi wetu kuendelea kwa mwendo kasi...

Think out of box msiwakatishe tamaa raia...ni kwa kufanya kazi kwa juhudi na maarifa tutaijenga nchi yetu
 
Suluisho ni kufanya Kazi kwa masaa tu. Ila nasilia fiesta ilijaa kiingilio kilikuwa buku 20
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Lengo la serikali ni kuhakikisha mnashindwa hata kununua maji safi , mrudi kwenye maji ya visima au ya dawasco .

Hao polisi ndio wa kuhurumiwa sana , zile bia za extreme ( unalipa buku unapewa 3 ) walizokuwa wanapewa zimefutiliwa mbali , kwa mishahara yao hafifu wengi wamerudia gongo .
 
Watu mna haha nyie mpaka basi...yaani unachagua bia in place ya huduma kwa jamii? Pesa zitakuja kwa njia nyingine kama kuzalisha na kuuza mazao kwakuongeza thamani...binadamu kaumbwa na akili so serikali inapopunguza anasa haina maana kutabakia tu kumesimama tu..inamaana uwezo wa kununua bidha za anasa utapungua lakini substitutes zipo, kule vijijini ambapo kuna bidhaa za msingi kama chakula na vitafunwa kama viazi vitamu, mihogo etc kwahiyo watu wata spend kwenye hizo instead of maandazi za Azam zilizotengeneza monopoly, itabidi agawe soko kwa wale wa kule shamba kwa mfano na mama lishe wa mijini..badala ya kunywa maziwa ya Kenya utatafuta kwa wafugaji wetu ambao huko Malinyi wana mwaga maziwa na kutakuwepo na wafanya biashara wataochukua hiyo fursa ya maziwa hayo kuyaleta mjini...kwahiyo utaonna sasa soko la bidhaa zetu kuongezeka in place ya vile vya nje ambavyo hakuna mwenye nguvu ya kununua kuileta huku...mwisho wa siku bidhaa zetu zitaanza kuongezwa thamani na uchumi wetu kukua baada ya waliochangamka kujenga uwezo zaidi...watu wengi wakiunganishwa kwenye uchumi inamaana wigo wa kodi utaongezeka kwani mifumo ya kodi na mianya ya ukwepaji imepungua hiyo itaziba pengo la budget iliyopatilana through kampuni yetu ya bia iliyo binafsishwa na mashamba yake ya ngano kuachwa kwakua mbia ana maslahi na kwao pia..there we go na mdogo mdogo mpaka uchumi wa kati na hatimaye uchumi mkubwa...mwendo wetu hauwezi kutabirika unaweza kuwa wa haraka au polepole kutokana na mwitikio wa jamii na nguvu ya kiongozi wetu kuendelea kwa mwendo kasi...

Think out of box msiwakatishe tamaa raia...ni kwa kufanya kazi kwa juhudi na maarifa tutaijenga nchi yetu
Hivi bia si tax payer namba one, akigoma taabu sana.
 
Hivi bia si tax payer namba one, akigoma taabu sana.

Atapata wakum replace though we shall suffer for a year or two...ukiunganisha mitaji usagaji unaweza kui substitute bia kwa haraka sana na kuleta impacts kubwa zaidi kuliko hata bia...
 
Nilichogundua ni kiwa siso tunapenda sana mteremko na hatupo tayari kwa change...inashangaza kila siku watu wanaleta arguments za status quo as if ilikuwa sustainable...you cannot eat your cake and have at the same time...ukivunja lazima upate pahala pa muda kabla ya kujenga...huwezi kuendelea kuona utulivu huku ukiwa unafanya mabadiliko...hata mama anapokuwa labour huwa na uchungu mpaka mtoto azaliwe...tupo kweenye labour ward ya uchumi wetu katika mfumo mpya sasa unategemea kukosa maumivu?
 
kuna watu utafikiri wapiga ramli kila siku misamiati yao ni ya kushindwa shindwa tu, saa nyingine unaweza kuliishi jambo kulingana na unavyofikiri kuna watu wakifilisika na kuanguka sitashangaa sababu mawazo na ubongo umesharidhia kushindwa kwa Lugha rahisi kuna watu Bongo zao zimefikia ukomo wa kuishi na sasa zinaishi kwa utashi wa Mazingira. Akili na mwili Binadamu imeumbwa na Flexibility principles, ndo maana ukiwa na njaa glucose iliyohifadhiwa inapambana ili kusogeza muda wa wewe kuweza kuishi hadi mwili utakapo pata chakula, the same ukiumwa kinga ya mwili inapambana. Ndivyo ilivyo hata katika maisha, Akili ni flexible mbinu flani ikishindwa mtu anajaribu nyengine mpaka afanikiwe, Wote tungewaza hivi leo dunia isingekuwa hivi, Akili iliyochoka kufikiri ni heri mwili uliozikwa mavumbini unarutubisha udongo na kutunza stock ya mafuta kuliko mtu anayeishi huku amekubali akili yake imeshindwa kuyakabili mazingira ambayo yanamzunguka, in simple way jukumu tulilopewa la kutawala na kuvitiisha vyote viijazavyo dunia wapo watu wameshakubali kuwa wameshindwa
 
Nilichogundua ni kiwa siso tunapenda sana mteremko na hatupo tayari kwa change...inashangaza kila siku watu wanaleta arguments za status quo as if ilikuwa sustainable...you cannot eat your cake and have at the same time...ukivunja lazima upate pahala pa muda kabla ya kujenga...huwezi kuendelea kuona utulivu huku ukiwa unafanya mabadiliko...hata mama anapokuwa labour huwa na uchungu mpaka mtoto azaliwe...tupo kweenye labour ward ya uchumi wetu katika mfumo mpya sasa unategemea kukosa maumivu?
Mngekuwa ni watu wenye kuona mbali mngeachana na bajeti za kutegemea walevi na mngebuni vyanzo vingine vya mapato ila mnabana vipato vya wanywa pombe huku mnategemea kodi ya vilevi.Sijui mnawaza nini nyinyi watu!
 
kuna watu utafikiri wapiga ramli kila siku misamiati yao ni ya kushindwa shindwa tu, saa nyingine unaweza kuliishi jambo kulingana na unavyofikiri kuna watu wakifilisika na kuanguka sitashangaa sababu mawazo na ubongo umesharidhia kushindwa kwa Lugha rahisi kuna watu Bongo zao zimefikia ukomo wa kuishi na sasa zinaishi kwa utashi wa Mazingira. Akili na mwili Binadamu imeumbwa na Flexibility principles, ndo maana ukiwa na njaa glucose iliyohifadhiwa inapambana ili kusogeza muda wa wewe kuweza kuishi hadi mwili utakapo pata chakula, the same ukiumwa kinga ya mwili inapambana. Ndivyo ilivyo hata katika maisha, Akili ni flexible mbinu flani ikishindwa mtu anajaribu nyengine mpaka afanikiwe, Wote tungewaza hivi leo dunia isingekuwa hivi, Akili iliyochoka kufikiri ni heri mwili uliozikwa mavumbini unarutubisha udongo na kutunza stock ya mafuta kuliko mtu anayeishi huku amekubali akili yake imeshindwa kuyakabili mazingira ambayo yanamzunguka, in simple way jukumu tulilopewa la kutawala na kuvitiisha vyote viijazavyo dunia wapo watu wameshakubali kuwa wameshindwa

Wengine walibahatisha kufika walipofika so any change is like dooms day kwao...haoni kingine zaidi ya anguko...so sad!
 
Nilichogundua ni kiwa siso tunapenda sana mteremko na hatupo tayari kwa change...inashangaza kila siku watu wanaleta arguments za status quo as if ilikuwa sustainable...you cannot eat your cake and have at the same time...ukivunja lazima upate pahala pa muda kabla ya kujenga...huwezi kuendelea kuona utulivu huku ukiwa unafanya mabadiliko...hata mama anapokuwa labour huwa na uchungu mpaka mtoto azaliwe...tupo kweenye labour ward ya uchumi wetu katika mfumo mpya sasa unategemea kukosa maumivu?

Ndugu watu wanatuthibitishia kuwa vichwa vyao vimechoka, kuna wakati unaweza kujikuta unatenda dhambi ya kukufuru bure, sasa kwanini mtu anaishi sasa kama kachoka??

Duniani toka ulipozaliwa ni survival for the fittest ukiwa mnyonge nature itakutoa tu automatically, usipokomaa hufiki popote na hii ni principle sio tajir au maskini, wa mjini au kijijini, aliyesoma au hajasoma, mwanaume au mwanamke, mtoto au mtu mzima everyone struggle kulingana na mazingira anayoyaishi vinyonge havi survive hata kidogo.
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Lengo la serikali ni kuhakikisha mnashindwa hata kununua maji safi , mrudi kwenye maji ya visima au ya dawasco .

Hao polisi ndio wa kuhurumiwa sana , zile bia za extreme ( unalipa buku unapewa 3 ) walizokuwa wanapewa zimefutiliwa mbali , kwa mishahara yao hafifu wengi wamerudia gongo .
Wacha waisome namba mkuu sisi yetu macho na masikio.
 
Kama kweli serikali itaamua kufuta posho za watumishi wa umaa na kudhibiti baadhi ya Taasisi za serikali zilizokuwa na mamlaka ya kujipangia mishahara na posho kupitia bodi za mashirika hayo,eneo mojawapo litakaloathirika sana na uamuzi huu ni uuzaji wa bia na aina nyingine ya vilevi katika mabaa,grocery,n.k pamoja na kampuni zinazojihusisha na utengenezaji na usambazaji wa vinywaji hivim

Baada ya serikali kuzuia safari za watumishi,semina,washa,mikutano na makongamano,watu wengi uwezo wao kununua vinywaji(pombe) ulipungua na uhudhuriaji katika mabaa mbalimbali ulishuka na wengi walimudu kwenda bar tarehe za mwisho wa mwezi tofauti na walivyokuwa wamezoea hapo awali.

Watumishi ambao walikuwa na nafuu kidogo ni wale ambao katika Taasisi wanazofanya kazi bado walikuwa wanapata posho ya katikati ya mwezi (kama vile polisi, mageraza, n.k) watumishi ambao mishahara yao iko juu,mashirika yao hayategemei OC kutoka serikali kujiendesha,n.k.

Hivyo basi,kama posho katika hizi Taasisi ambazo watumishi wake bado wanapokea posho hizi zitasitishwa, Mashirika na Taasi ambazo zilizokuwa na mamlaka ya kujipangia bajeti zake na kujiendesha zenyewe bila kuingiliwa na serikali nazo zitanyang'anywa mamlaka hayo na hivyo kulazimika kupunguza safari na posho za watumishi wake,n.k,sioni ni wangapi watakaomudu kuendelea kwenda bar na kuagiza vinywaji zaidi ya kusubiri mwisho wa mwezi na hapa itategemea na madeni aliyonayo mtaani na kwenye salary slip yake(kama alikopa benki,n.k).

Posho hizi ndio zilikuwa zinasaidia watumishi kufukia mashimo(madeni ya mabenki,saccos,n.k)na kuwawezesha watumishi hawa kuhudhuria bar ila sasa ndio hizo nazo taratibu zinaota mbawa.

Uamuzi wa serikali wa kutoongeza mishahara,kuzuia safari ,mikutano, washa,makongamano,n.k na sasa kutaka kufuta hata baadhi ya posho zilizopo kisheria katika baadhi ya mashirika na Taasisi za umma, utakwenda kuathiri mapato ya makampuni ya bia na mwisho wa siku serikali nayo itaathirika kwa kukosa mapato yatakonayo na kodi ya kuuza vinywaji hivi.

Kama kweli sekta binafsi zinayumba kama tunavyosikia,serikalini nako tight,wafanyabiashara nao lazima wayumbe kwasababu watumishi hawa ndio wataje wao.

Sasa kama mtumishi wa umaa amebanwa,wa sekta binafsi nae hana kitu au amekuwa jobless na mfanyabiashara nae kipato chake kimeshuka,sioni uwezekano wa biashara ya vinywaji kuongezeka zaidi ya kupungua na kupelekea serikali kukosa mapato.

Aliezoea kunywa bia 5 sasa atalazimika kunywa bia 2 ama kuacha kabisa tofauti na mahitaji mengine ya nyumbani ambayo ni ya lazima(sio anasa).

Hii itakuwa ni moja ya athari ya kubana watumishi ambayo kwa sasa inaweza isionekane ila ni swaka la muda tu itakuja kujidhihirisha.

Pamoja na yote hayo,msisahau na sheria ya kuzuia watu kunywa pombe kabla ya saa 10 jioni, sheria ambayo imeanza kutekelezwa katika awamu hii ili watu wafanye kazi.

Lingine la kuzingati ni ukweli kuwa watu wengi huwa hawaendi baa peke yao bali hufuatana na ama mke,mchumba,kimada,rafiki,ndugu,jamaa n.k, hivyo kipato cha mtu mmoja tu kina mchango mkubwa sana katika biashara hii ya vilevi kuliko tunavyofikiri.
IMEIMARISHA SANA NDOA ZA WATU WALIKUWA WANASHINDAA BAR WAKISAHAU FAMILIA ZAOO AWANA ADABU NA HAYOMKAMPUNI YAZIME TU WAANZE NA BAR UNAMWACHAJELEVI ANAKUNYWA MPAK SASABA MUME WA MTU LOH
 
Kumbe ina m
Watu mna haha nyie mpaka basi...yaani unachagua bia in place ya huduma kwa jamii? Pesa zitakuja kwa njia nyingine kama kuzalisha na kuuza mazao kwakuongeza thamani...binadamu kaumbwa na akili so serikali inapopunguza anasa haina maana kutabakia tu kumesimama tu..inamaana uwezo wa kununua bidha za anasa utapungua lakini substitutes zipo, kule vijijini ambapo kuna bidhaa za msingi kama chakula na vitafunwa kama viazi vitamu, mihogo etc kwahiyo watu wata spend kwenye hizo instead of maandazi za Azam zilizotengeneza monopoly, itabidi agawe soko kwa wale wa kule shamba kwa mfano na mama lishe wa mijini..badala ya kunywa maziwa ya Kenya utatafuta kwa wafugaji wetu ambao huko Malinyi wana mwaga maziwa na kutakuwepo na wafanya biashara wataochukua hiyo fursa ya maziwa hayo kuyaleta mjini...kwahiyo utaonna sasa soko la bidhaa zetu kuongezeka in place ya vile vya nje ambavyo hakuna mwenye nguvu ya kununua kuileta huku...mwisho wa siku bidhaa zetu zitaanza kuongezwa thamani na uchumi wetu kukua baada ya waliochangamka kujenga uwezo zaidi...watu wengi wakiunganishwa kwenye uchumi inamaana wigo wa kodi utaongezeka kwani mifumo ya kodi na mianya ya ukwepaji imepungua hiyo itaziba pengo la budget iliyopatilana through kampuni yetu ya bia iliyo binafsishwa na mashamba yake ya ngano kuachwa kwakua mbia ana maslahi na kwao pia..there we go na mdogo mdogo mpaka uchumi wa kati na hatimaye uchumi mkubwa...mwendo wetu hauwezi kutabirika unaweza kuwa wa haraka au polepole kutokana na mwitikio wa jamii na nguvu ya kiongozi wetu kuendelea kwa mwendo kasi...

Think out of box msiwakatishe tamaa raia...ni kwa kufanya kazi kwa juhudi na maarifa tutaijenga nchi yetu
Kumbe ina maana Azam akikosa soko basi wafanyakazi wa Azam wanaendelea kupata neema ya mishahara... Sijui hapo umefikiria kwenda mbele au kurudi nyuma
 
Mnahangaika sana vijana... Market trend ya bia za TBL iko vyema tu sokoni na ndio maana Shares zake kule DSE hazijatetereka... Kwa namna yeyote ile kama TBL ingekuwa inaperform vibaya sokoni lazima wangeshusha price za share zao ili kuraise Capital kufidia hasara wazipatazo sokoni..

BTW hizi kelele huwa mnazipiga mara zote. Mwezi September baada ya mauzo ya shares kushuka kule DSE mlisema uchumi unateremka kwa kasi. Tuliwaelimisha humu mkatuone wajinga. Leo hii Shares zimenunuliwa double ukilinganisha na miezi ya nyuma..
 
....
....Tukutane Karatu ijumaa uzinduzi kwa Martha Carnival ntatuma wawakilishi wabeba box nama paundi ya kutosha ...member wa j4 bia buree
 
Back
Top Bottom