NALA MONEY yafungua ofisi yake ya kwanza Afrika jijini Nairobi, Kenya

I am Groot

JF-Expert Member
Jul 20, 2018
3,726
10,020
Kampuni ya NALA MONEY Nala ya kijana Mtanzania Benjamini Fernandes imefungua rasmi ofisi yake ya kwanza Afrika, mjini Nairobi nchini Kenya.

Ufunguzi wa ofisi hiyo uliambatana na utiaji saini mkataba wa kibiashara kati ya NALA na benki ya Equity nchini Kenya ili kuwawezesha Watu kutuma fedha kutoka Uingereza na Marekani kwenda Kenya kwenye akaunti za Safaricom, Airtel pamoja na benki.

“Ninafuraha sana kwa hatua hii nyingine ya mafanikio kuweza kuwa na ofisi yetu ya kwanza Afrika nchini Kenya pamoja na kuendelea kuwa na ushirika wa kibiashara na benki ya Equity, hii itazidi kutusaidia kuendelea kutoa gharama nafuu, haraka na salama zaidi kwenye utumaji fedha kwa Watu waishio ughaibuni” amesema Benjamin.

Kampuni hii inamiliki APP inayopatikana kwenye google play store na apple store ambapo sio Kenya pekee bali hata Watanzania walio nchini Marekani na Uingereza wanaweza kuitumia kutuma pesa Tanzania kqa gharama nafuu na haraka.

Chanzo: Millard Ayo
 
Wew Fernandez kapiga sanaa kitabu sio failure

Sent from my 220333QAG using JamiiForums mobile app
Huijui historia yake..
Alifeli form 6, alisoma Tanzania katika mtaala wa Cambridge

Baada ya kufeli akahangaika kutafuta Scholarship akapata na ayo ayo matokeo yake mabovu.. Baada ya hapo ndio alienda kufanya Maajabu kwenye Vyuo vya Marekani huko alikokua anasoma kwa Scholarship
 
Ukisikiliza interview yake na millard ayo hauwezi kushangaa, bongo hii wabunifu hawapewi incetives kulinganisha na milolongo isiyokwisha..

Ila ndo tutafanyaje, kila siku tunahimizwa tukalime ili tuendelee kuwa wateja wa digital products hata kwa zile ambazo vijana tunaweza kutengeneza..
 
Ukisikiliza interview yake na millard ayo hauwezi kushangaa, bongo hii wabunifu hawapewi incetives kulinganisha na milolongo isiyokwisha..

Ila ndo tutafanyaje, kila siku tunahimizwa tukalime ili tuendelee kuwa wateja wa digital products hata kwa zile ambazo vijana tunaweza kutengeneza..
Wakata mauno,machawa,wadakudaku

Wanapewa kipaumbele

Ova
 
Tanzania alifungua ila akafunga coz TRA na TCRA walimpelekea invoices za mlolongo wa makodi ambayo alishindwa kuyalipa akaona akaweke headquarters zake London tu.
Sasa badala ya kusaidia mzalendo huyu wamamufikisi na milolongo ya makodi ha ha ha, badala wampe kibali an then fedha jinsi zitakavyokuwa zinatumwa wawe wanakata parcentage humohumo / 4%,1.5%its benefit and so so
 
Huijui historia yake..
Alifeli form 6, alisoma Tanzania katika mtaala wa Cambridge

Baada ya kufeli akahangaika kutafuta Scholarship akapata na ayo ayo matokeo yake mabovu.. Baada ya hapo ndio alienda kufanya Maajabu kwenye Vyuo vya Marekani huko alikokua anasoma kwa Scholarship
Ww ulie faulu Tanzania mpk umebuni kitu gani?
 
Back
Top Bottom