Nakuuliza hivi Mheshimiwa JK...

Engineer Mohamed

JF-Expert Member
Jul 27, 2007
451
9
Nakuuliza mheshimiwa JK....JF members na wa-TZ wenzangu wote HAKUNA MZANZIBARI MWENYE SIFA YA KUCHAGULIWA KUWA GAVANA WA BoT???? haaaaaa ametoka,dr idrissa rashid(mtanganyika) amekuja BALALI(MTANGANYIKA) na huyo wa sasa Prof NANI HATA JINA SIMJUI anatoka TANGANYIKA also.

Mheshimiwa JK angalia na upande wa PILI WA SHILLINGI.
 
HAYA NDIO SEHEMU YA MATATIZO YA MUUNGANO VYOMBO MUHIMU SIKU ZOTE HUKAMATA WATU WA UPANDE MMOJA

MIE NNAONA UMEFIKA WAKATI WA UPANDE WA PILI KUPEWA HASA UKIZINGATIA
hakuna m-znz aloshika wizara ya muungano akaondoshwa kwa wizi au ubadhirifu
 
Baadaye utadai hata uwaziri wa wizara mbali mbali uwe ni kwa zamu! IGP, CDF, etc, nao wateuliwe kwa zamu kati ya Zanzibar na bara?

Zanzibar ina watu kidogo zaidi ya Wilaya ya Kinondoni. Mbona kujilinganisha na bara kila mara? Wacheni usumbufu. Sasa tuna Tanzania na hatuna Tanganyika. Gavana akitoka Tanzania ametoka Zanzibar vile vile kwani Zanzibar ni sehemu ya Tanzania
 
zanzibar kubwa yakhe! atoke pemba au unguja?. maana vyeo vingi wameshika waunguja, wapemba je?
 
Nakuuliza mheshimiwa JK....JF members na wa-TZ wenzangu wote HAKUNA MZANZIBARI MWENYE SIFA YA KUCHAGULIWA KUWA GAVANA WA BoT???? haaaaaa ametoka,dr idrissa rashid(mtanganyika) amekuja BALALI(MTANGANYIKA) na huyo wa sasa Prof NANI HATA JINA SIMJUI anatoka TANGANYIKA also.

Mheshimiwa JK angalia na upande wa PILI WA SHILLINGI.
Mimi naona kabla ya waZanzibari kuanza kulalamikia vyeo vya Muungano, kwanza mngeanza kulalamikia jirani na ndugu zenu halisa wa hapo Pemba, wapewe nafasi kwenye serikali ya mapinduzi. Nna uhakika mkianzia hapo basi hata kwenye muungano mnaweza mkapata sauti ya kutaka madaraka. Waswahili wana msemi wao, Nyani huona ku... la mwenzake lakini lake halioni.

Kwa kuongezea kidogo, niliwahi kumsikia mZanzibari mmoja akisema "tena waPemba wana akili sana", sasa kama ni hivyo kwa nini hamuanzii hapo? au hamjui system ni nini?
 
zanzibar kubwa yakhe! atoke pemba au unguja?. maana vyeo vingi wameshika waunguja, wapemba je?

Pemba nayo kubwa Ami, sasa atoke Gombani, Wete, Ziwani, Kengeja, Kijiwe au Konde?
 
Pemba nayo kubwa Ami, sasa atoke Gombani, Wete, Ziwani, Kengeja, Kijiwe au Konde?

ndo maana akitoka Tanzania basi yatosha, si lazima iwe pemba au unguja, au daresalama ama kagera, wote ni wamoja. kuna swali la nyongeza?
 
Nakuuliza mheshimiwa JK....JF members na wa-TZ wenzangu wote HAKUNA MZANZIBARI MWENYE SIFA YA KUCHAGULIWA KUWA GAVANA WA BoT???? haaaaaa ametoka,dr idrissa rashid(mtanganyika) amekuja BALALI(MTANGANYIKA) na huyo wa sasa Prof NANI HATA JINA SIMJUI anatoka TANGANYIKA also.

Mheshimiwa JK angalia na upande wa PILI WA SHILLINGI.

Kama unaona yupo mtaje!
 
Ukikaa na mawazo ya "tunaonewa, tunaonewa" huwezi kuendelea milele, utasubiri favors, affirmative action, reparations, quotas and all that jazz.

Watu wasome, wapige kazi vizuri utaona watafuatwa tu kwa utaalamu wao, kama siyo benki kuu hata na benki ya dunia na madili mengine makubwa huko ambako hawajui tofauti ya Unguja Pemba Mafia na Ukerewe.
 
Nakuuliza mheshimiwa JK....JF members na wa-TZ wenzangu wote HAKUNA MZANZIBARI MWENYE SIFA YA KUCHAGULIWA KUWA GAVANA WA BoT???? haaaaaa ametoka,dr idrissa rashid(mtanganyika) amekuja BALALI(MTANGANYIKA) na huyo wa sasa Prof NANI HATA JINA SIMJUI anatoka TANGANYIKA also.

Mheshimiwa JK angalia na upande wa PILI WA SHILLINGI.
UKisema au kulalamika hivyo weka majina ya baadhi wanao qualify na position ile na elimu zao
 
wao wazanzibari..sisi wazanzibara...it seems tukiendelea na imani hizo itafikia stage hata makabila mbali mbali yataanza dai na wao...sasa hapo nashukuru aliyeanzisha post hii amejibiwa vyema kama wa unguja wakilalamika je wapemba wasemeje??
tusitake kuendeshwa na imani za namna hii hatutafika kokote
 
hapo ndipo huwa namkubali sana Mwl JKN RIP, kama siyo kuonyesha kwa logic ya hali ya juu kuhusiana na ubaguzi wa Uzanzibari na Uzanzibara hoja za wabaguzi zingekuwa ngumu kweli kweli kuzivunja!
 
Mbona Ya Mkuu Wa Majeshi Haikulalamikiwa Maana Nao Woote Wamekuwa Wakitoka Bara. Enywayz Kama Kuna Mzanzibari, Mmatumbi, Mpemba Mwenye Sifa Zinazohitajika Basi The Argument Might B Valid
 
Mtu wa Pwani, i dont think that is the right way of thinking, Matatizo ya Muungano hayatatuliwa kwa appointment of one person to be the governor of BOT, neither do i believe this should be given as a token to Zanzibar. Nashangaa hujui hata jina la aliyekuwa appointed yet his name is allover the papers!! how insensitive and prejudiced you are. i think hoja ingekuwa kama the person appointed has the intergrity to cleanly run the institution. let us not be affected by uzanzibari or ubara as we are all inclined towards the development of one nation
 
tusiwe so 'shallow minded persons'.kwani BOT ndio kitovu jamani,.tunataka watu wenye sifa za kutosha kushika nafasi husika,haya mambo ya kuangalia wapi unatoka hayasaidii
 
Nakuuliza mheshimiwa JK....JF members na wa-TZ wenzangu wote HAKUNA MZANZIBARI MWENYE SIFA YA KUCHAGULIWA KUWA GAVANA WA BoT???? haaaaaa ametoka,dr idrissa rashid(mtanganyika) amekuja BALALI(MTANGANYIKA) na huyo wa sasa Prof NANI HATA JINA SIMJUI anatoka TANGANYIKA also.

Mheshimiwa JK angalia na upande wa PILI WA SHILLINGI.

Yakhe, vipi tena Mhandisi. Tanganyika ndiyo nchi gani tena? Mbona kwenye ramani ya dunia haipo? Hiyo nchi ilikufa na kuzikwa siku nyingi sana na matanga yalifanyika kitambo.Kilichobaki ni kuiua Zanzibar na Pemba tu (ndiyo sera ya chama-kuwa na serikali moja)!
 
Ndo mshaanza, mkitoka kudai kwamba ni zamu ya mzanzibar kuwa gavana, mtaanza ooh mbona katoka mkristo, karudi tena mkristo(if its true according to their names, may be they are not even christian), waislam je? So, inabidi tuwe waangalifu, i think aina hii ya kufikiri tuwaachie laymen.
 
HAYA NDIO SEHEMU YA MATATIZO YA MUUNGANO VYOMBO MUHIMU SIKU ZOTE HUKAMATA WATU WA UPANDE MMOJA

MIE NNAONA UMEFIKA WAKATI WA UPANDE WA PILI KUPEWA HASA UKIZINGATIA
hakuna m-znz aloshika wizara ya muungano akaondoshwa kwa wizi au ubadhirifu

yaani mtu wa pwani wee acha tu.si unaona rekodi ya marehemu dr omer ali juma and hivi sasa ya dr ali mohd shein.
 
Dr. Omar Ali Juma "Chinja Chinja"? Dr. Shein naye amefanya nini zaidi ya kufumbia macho ufisadi?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom