Nakumbuka ndege ya Kijeshi iliyoanguka mbele ya Nyerere

Rubani akiitwa SAIDI KARAMA, alizikwa siku ya jumatano katika makaburi ya Kisutu, maiti ilitokea mtaa wa Congo nyumba namba 40, mahali palipokuwa na ule mti mkubwa uliokuwa unatumiwa sasa na wanga wa mitaa ya Kariakoo,maarufu kama MTAMBANI maziko yaliongozwa na Mzee Kawawa,sina hakika by then alikuwa ni waziri mkuu au waziri wa ulinzi.

Ile ajali ya ndege imebaki kwenye kumbukumbu za wengi walioshuhudia na kusikia kwenye radio, enzi hizo hakukuwa na TV. Walikuwa marubani wawili, Capt. Said Karama na Capt. Abdallah (?) Kikunda. Inawezekana jina la kwanza la marehemu Kikunda likawa sio sahihi, lakini jina la ukoo ni Kikunda. Nadhani baada ya hapo ilipita miaka mingi bila kuwa na hizo air shows, sina hakika kama zimerudishwa miaka hii. Mungu Awalaze pema.

Jamani, hawa mashujaa mbona hatuweki habari zao kwa maandishi ili vizazi vingi zaidi vijue heshima kubwa iliyotolewa na watu hawa wachache waliotangulia mbele ya haki?


Tukio lile lilikuwa na sifa kadhaa mabazo uilitakiwe liwe la kihistoria ila basi ni sisi wachache tu tuliolishuhudia ndio tuna kumbukumbu.

(1) Ilikuwa ni ndege ya kwanza ya kivita kuanguka mbele ya umati wa watanzania tena wakati wa sherehe.

(2) Ilikuwa ni tukio mara tu baada ya vita pekee ambayo jeshi letu lilikuwa limetekeleza jukumu lake la la kulinda na kutetea mipata yetu: Vita ya Kagera

(3) Ni ajali iliyotokea mbele ya macho ya amiri jeshi mkuu

(4) Kipindi hicho tulikuwa na marubani wachache sana wenye ujuzi wa ndege za kivita, hivyo kupoteza marubani waiwili lilikuwa ni pigo kubwa sana kwa jeshi letu la anga ambalo lilikuwa bado changa.

Binafsi nilikuwa mwanafunzi wa form 6 wakati huo, na nilikuwa Dar kwa dharura fupi nikatumia nafasi hiyo kwenda uwanja wa taifa kujionea ndege zile kwa vile niliwahi kuziona kwenye mazoezi. Kwa bahati mbaya, ilikuwa ni experience mbaya sana kwangu kwani ilibadilisha nisipende tena kazi ya urubani niliyokuwa naota kwa PGM yangu. Mara ya mwisho nilipoondoka Dar es Salaama, sikuwahi kuona kumbukumbu yoyote ya tukio hilo. Wakati nikiwa JKT Mgulani nakumbuka kusikia mradi wa mnara huo lakini sina uhakika kama kweli ulijengwa wakati huo. To the best, wangeweka vipande (debris) vya ndege hiyo kule jumba la makumbusho ya taifa.
 
KICHUGUU,mnara wa kumbukumbu upo at the exact spot where the plane fell. MY then girlfreind alikuwa akitoroka usiku mgulani jkt akipitia kichochoro cha nyuma nadhani teachers college,me i used to sit by this remembarance statue waiting for her
 
Jamaa zangu waling'ang'ania sana twende siku ile mimi nikawatolea nje na kuwaambia kutakuwa na umati mkubwa wa watu na ndege za kivita zinaweza kabisa kuanguka na kusababisha maafa makubwa sana, hivyo hatukwenda. Ni kweli kama si juhudi za yule shujaa pilot kuhakikisha ile ndege inaangukia mbali na ule umati wa watu basi watu wengi sana wangepoteza maisha siku ile.



Pweza Paul???:bowl:
 
Hivi kwanini walibadilisha tarehe ya mashujaa toka 1 september kula july 25? naomba mnijuze
 
Hivi na wale wzee waliopigana vita vya mkoloni na wao kwetu sisi ni mashujaa? Au mashujaa wa wakoloni - UK and Germany?
 
KICHUGUU,mnara wa kumbukumbu upo at the exact spot where the plane fell. MY then girlfreind alikuwa akitoroka usiku mgulani jkt akipitia kichochoro cha nyuma nadhani teachers college,me i used to sit by this remembarance statue waiting for her

Mkuu huo ndio ulikua utaratibu wako wa kuwakumbuka wahanga wetu!?
au nawe ndio ulikua unajiona shujaa?
 
Mie wakati huo nilikuwa kinda kwelikweli,ila majuzi hapa TBC walionesha vita ya Kagera kupitia channeli yake ya TBC2. Tukio la ajali ya ndege ya kivita nililishuhudia runingani.Aisee iliniingie kweli akilini kwa kweli.
 
Mimi nakumbuka kuwepo uwanjani na mdogo wangu ambaye baada ya ndege kuanguka na kuwa na mtafaruku uwanjani, nakumbuka kwa usalama wake na kuogopa kukanyagwa na watu aliingia uwanjani napi niliogopa saana hasa kumpoteza mdogo wangu, lakini baada ya kumpata , ndio ikajja shauku ya kwenda kuangalia ilipo dondoka katika uwanja wa JKT au kitu kama hicho, nakumbuka tulipita uwanja wa ndani , kule magari ya mabaharia/mitumba ilipokuwa ina hifadhiwa, mpaka sehemu ya tukio tukakuta mti uliogongwa, mabaki ya ndege helmet ya moja wa marubani, na boot moja.
Inavyo semekana ni kwamba rubani alijitahidi kuimiliki ndege ile asilete madhara makubwa, pale uwanjani, na ilikuwa akaidondoshe bahari, ambapo angeweza kuruka /eject hicho kiti, nae ashuke salama, bahati mbaya hakufika mbali. Ni matumaini yangu serikali iliisaidia familia za hawa marubani, na ingekuwa vizuri tukawa na tabia ya kuandika majina ya mashuja wetu pale mnazi moja na ikiwezekana na walipo fia ikiwa msumbiji, uganda uwanja wa taifa nk.
 
Ni kumbukumbu nzuri na ya masikitiko. Ndege za kipindi hicho nina mashaka nazo, na hata ikitokea maonyesho ya jinsi hiyo Dar es salaam nitaomba ruhusa kazini na kwenda hata Lindi kusubiria hadi maonyesho hayo yapite.

Na nadhani imesha gundulika kwamba hazifai kufanya shows za jinsi ile mbele ya sehemu za mikusanyiko ya watu kutokana na hitilafu mbali mbali.

Hayo ma kombo ya zana za kale za kijeshi tuliyo nayo Tanzania ni vema yaka teketezwa na tukaachana na kununua silaha za kisasa kutokana na hali mbaya ya kiuchumi tuliyo nayo. Baadhi ya nchi zilizo endelea wameanza kupunguza ukubwa wa majeshi yake ili kulinda hali ya uchumi.

Nilishangaa kusoma taarifa toka Bungeni mkuu wa nchi anafikiria jinsi ya kuliongezea jeshi zana za kisasa katika uongozi wake. Kwa maisha bora kwa kila mtanzania sidhani kama hili ni la kulipa kipaumbele.

Hatukatai kwamba vita vinaweza kutokea, Lakini je ni miaka mingapi ilipita bila ya Jeshi letu kutumia zana ambazo zinanunuliwa kinyemela kwa mabilioni ya shilingi na kuliongezea Taifa hili umaskini?

Kujilinda kijeshi ni jambo jema lakini endapo utakuwa unawalinda watu wenye neema kimaisha. Ya nini kununua AK 47 kumlinda mtoto mwenye utapiamlo aliyebakiza siku 5 kuuona ufalme wa Mungu?

Ununuzi wa Silaha za Kijeshi unaambatana na ufisadi mkubwa, Na Kama Amiri Jeshi mkuu kweli anania ya kulikomboa Taifa na umaskini, Hiyo fedha ya kununulia
AH-64 Apache Helicopter ataitumia katika juhudi za vyanzo vya kuzalisha umeme ambao utatumika katika uwekezaji na uzalishaji wa viwandani na sehemu zingine zenye kuhitaji huduma hiyo ya umeme.

Mungu Ibariki Tanzania.
 
pamoja na matatizo ya ndege zetu lakini pia hata umri wa ndege zenyewe unakuwa umepitwa na wakati.achana na za kichina ambazo ni feki tu .kumbuka kuwa ndege za kirusi aina ya topolev zinaanguka kila leo hasa kongo sababu ya uzee.mig 17 ni old vision.ukizingatia na uchakachuaji wetu basi balaa tu
 
Mwaka 1980 katika sherehe za mashujaa kulikuwa na parade kali ya kijeshi mbele ya Raisi Nyerere hapo uwanja wa Taifa huku ikisindikizwa na airshow; hiyo ilikuwa ndiyo sherehe ya kwanza ya mashujaa Tanzania baada ya vita ya Kagera. Kulikuwa na ndege ambazo nadhani zilikuwa tatu za kivita zikiwa zinavinjari anga lile na kuonyesha mbwembwe za angani. Kwa bahati mbaya mojawapo ilipata hitilafu na kuanguka mbele ya macho ya Nyerere karibu sana na kilipo Chuo Kikuu cha Elimu cha Chang'ombe na kumwua rubani wake; ni pembeni kidogo na ulipo uwanja wa Taifa mpya.

Baada ya ajali ile, Nyerere hakusema mengi katika hotuba aliyokuwa ameandaa badala yake aliwakumbusha wanachi kwa sentensi moja tu, kuwa mashujaa wetu walikumbana matukio mengi ya aina hiyo wakati wa kumwondoa nduli Amini. Kuna wengi waliopoteza maisha yao kama huyu shujaa tuliyeshududia maisha yake yakipotea mbele yetu. Sina kumbukumbu ya maneno kamili yaliyotumiwa na Nyerere kutoa ujumbe huo mfupi.


Nimekumbuka tukio lile kwa sababu wiki chache zilizopita kulikuwa na taarifa za wapiganaji wetu kuangua na ndege ya kivita huko Handeni na kupoteza maisha yao, na tukio la leo ambapo ndege ya kivita ilianguka huko Kanada na rubani akajirusha angani na kusalimisha maisha yake Ni kawaida kuwa kunapotokea hitilafu kwenye ndege za kivita huwa rubani anaiachia ndege ikajiangukie na yeye mwenye kuruka salama kwa mwavuli. Swali langu je sisi ndege zetu za kivita tulizinunua wapi zisiwe na mechanism ya kuokoa maisha ya rubani namna hiyo?








Hilo tukio lilipaswa kuandikiwa kitabu.
 
Jamaa zangu waling'ang'ania sana twende siku ile mimi nikawatolea nje na kuwaambia kutakuwa na umati mkubwa wa watu na ndege za kivita zinaweza kabisa kuanguka na kusababisha maafa makubwa sana, hivyo hatukwenda. Ni kweli kama si juhudi za yule shujaa pilot kuhakikisha ile ndege inaangukia mbali na ule umati wa watu basi watu wengi sana wangepoteza maisha siku ile.
Where you ?
 
Last week I had a chance to see one of our birds flying from Aga khan Parking venue Upanga
 
Back
Top Bottom