Kichuguu
Platinum Member
- Oct 11, 2006
- 15,498
- 19,339
Mwaka 1980 katika sherehe za mashujaa kulikuwa na parade kali ya kijeshi mbele ya Raisi Nyerere hapo uwanja wa Taifa huku ikisindikizwa na airshow; hiyo ilikuwa ndiyo sherehe ya kwanza ya mashujaa Tanzania baada ya vita ya Kagera. Kulikuwa na ndege ambazo nadhani zilikuwa tatu za kivita zikiwa zinavinjari anga lile na kuonyesha mbwembwe za angani. Kwa bahati mbaya mojawapo ilipata hitilafu na kuanguka mbele ya macho ya Nyerere karibu sana na kilipo Chuo Kikuu cha Elimu cha Chang'ombe na kumwua rubani wake; ni pembeni kidogo na ulipo uwanja wa Taifa mpya.
Baada ya ajali ile, Nyerere hakusema mengi katika hotuba aliyokuwa ameandaa badala yake aliwakumbusha wanachi kwa sentensi moja tu, kuwa mashujaa wetu walikumbana matukio mengi ya aina hiyo wakati wa kumwondoa nduli Amini. Kuna wengi waliopoteza maisha yao kama huyu shujaa tuliyeshududia maisha yake yakipotea mbele yetu. Sina kumbukumbu ya maneno kamili yaliyotumiwa na Nyerere kutoa ujumbe huo mfupi.
Nimekumbuka tukio lile kwa sababu wiki chache zilizopita kulikuwa na taarifa za wapiganaji wetu kuangua na ndege ya kivita huko Handeni na kupoteza maisha yao, na tukio la leo ambapo ndege ya kivita ilianguka huko Kanada na rubani akajirusha angani na kusalimisha maisha yake Ni kawaida kuwa kunapotokea hitilafu kwenye ndege za kivita huwa rubani anaiachia ndege ikajiangukie na yeye mwenye kuruka salama kwa mwavuli. Swali langu je sisi ndege zetu za kivita tulizinunua wapi zisiwe na mechanism ya kuokoa maisha ya rubani namna hiyo?
Baada ya ajali ile, Nyerere hakusema mengi katika hotuba aliyokuwa ameandaa badala yake aliwakumbusha wanachi kwa sentensi moja tu, kuwa mashujaa wetu walikumbana matukio mengi ya aina hiyo wakati wa kumwondoa nduli Amini. Kuna wengi waliopoteza maisha yao kama huyu shujaa tuliyeshududia maisha yake yakipotea mbele yetu. Sina kumbukumbu ya maneno kamili yaliyotumiwa na Nyerere kutoa ujumbe huo mfupi.
Nimekumbuka tukio lile kwa sababu wiki chache zilizopita kulikuwa na taarifa za wapiganaji wetu kuangua na ndege ya kivita huko Handeni na kupoteza maisha yao, na tukio la leo ambapo ndege ya kivita ilianguka huko Kanada na rubani akajirusha angani na kusalimisha maisha yake Ni kawaida kuwa kunapotokea hitilafu kwenye ndege za kivita huwa rubani anaiachia ndege ikajiangukie na yeye mwenye kuruka salama kwa mwavuli. Swali langu je sisi ndege zetu za kivita tulizinunua wapi zisiwe na mechanism ya kuokoa maisha ya rubani namna hiyo?
Last edited by a moderator: