Nilibahatika kufuatilia mkutano wa Spika Ndugai na Waandishi wa Habari alioufanya jana jijini Dar es Salaam. Nilifuatilia kuanzia maelezo yake;maswali aliyoulizwa;majibu yake na maswali aliyowauliza wauliza maswali.
Lipo jambo la kikatiba ambalo Spika Ndugai amelizungumza ili kujenga hoja yake kuwa kauli ya Prof. Assad juu ya udhaifu wa Bunge imemgusa hadi Rais Magufuli. Spika alisema kuwa Rais ni sehemu ya Bunge. Hilo nakubaliana na Spika Ndugai.
Lakini, katika utendaji wa Bunge, Rais huwa sehemu ya Bunge katika masuala mawili tu: katika utungaji wa Sheria na katika masuala ya kibajeti. Katika masuala mengine kama kuisimamia Serikali, Rais 'si' sehemu ya Bunge. Rais hawezi 'kujisimamia' mwenyewe akiwa sehemu ya Bunge na mkuu wa Serikali kwa upande mwingine.
Kauli ya Prof. Assad, kwa uelewa wangu, ililenga kwenye wajibu wa Bunge katika kuisimamia Serikali hasa katika kuhakikisha matumizi yanakuwa sawa na ufisadi unadhibitiwa. Katika hilo, Rais hawi sehemu ya Bunge. Hivyobasi, kauli ya Prof. Assad haikumhusu Rais Magufuli kama Spika Ndugai anavyotaka kutuaminisha.
Nasema tena kuwa kauli ya Prof. Assad haikumhusu Rais, Waziri Mkuu au Baraza la Mawaziri. Ililihusu Bunge katika muktadha na sura ya kuisimamia Serikali kwa kuisimamia na kutekeleza mapendekezo ya CAG kwenye Ripoti zake.
Si vyema kumleta Rais, Waziri Mkuu na Mawaziri kwenye sakata hili ili ionekane kuwa Prof. Assad amewakosea hata wakuu wake. Halafu, lugha ya staha iwe inatumika wakati wa kuipinga lugha inayodaiwa kuwa ni ya kuudhi. Vijembe na kejeli hazijengi.
Hakukuwa na haja ya kumshauri Prof. Assad kujiuzulu au kwenda kwa Rais kuzungumza naye kwa sababu mbili. Kwanza, azimio la Bunge limeshamwadhibu kwa kutofanya naye kazi na si kumshauri ajiuzulu. Pili, Prof. Assad hana mgogoro wowote na Rais ili akazungumze naye kwa kuomba radhi. Katika kuisimamia Serikali,Rais 'si' sehemu ya Bunge.
Si kweli Rais ni sehemu ya Bunge ila si mbunge..sasa CAG alifanya kazi ya sehem ya Rais ila si vinginevyoMkuu japo bunge ni dhaifu na spika ni dhaifu sana lakini kwenye hoja ya kumwingiza Rais, hajakosea wala hakumwingiza kwa bahati mbaya. Hivi jambo kama hili lingeweza tokea kipindi cha Mwl JK? Hivi jambo kama hili lingetokea wakati wa Ben? Conflict kama hizi zinatokea sasa kwa sababu ni wakati wake kwa kuwa mazingira yana mbolea!
Huyu supika Inaonekana hata anachofanya Kama mwakilishi wa wagogo wenzake na Kama supika hakijuiWanalipwa na Mhe. Rais (kwa mujibu wa Mhe. Spika)
Kumng'oa CAG sio kirahisi na mh Spika anajua ndo maana alishauri tu CAG ajihuzuru. Sasa prof haoni kosa so why ajiuzuru?Speaker anatafuta kuungwa mkono na Rais. Ila tayari walishasuka mbinu ya kumng'oa CAG
Never HUYU hawez kufanya haya Bila baraka za raisiKinachofanyika...Speaker anataka kumkosanisha C.A.G na rais ila huenda pia ni mpango maalumu na kuna mmoja yuko nyuma ya pazia ila mmoja ndio anatumwa..hapa kuna utata
Wa sangara
Bahati mbaya siyo Spika pekee, ni watanzania wengi wanaamini hivyo.Wanalipwa na Mhe. Rais (kwa mujibu wa Mhe. Spika)
Tatizo siyo Spika. Tatizo ni hao waliomvika kofia hiyo.