Nakubaliana na Spika wa Bunge Job Yustino Ndugai lakini si katika yote aliyoyasema jana

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Dec 27, 2012
10,195
25,513
Nilibahatika kufuatilia mkutano wa Spika Ndugai na Waandishi wa Habari alioufanya jana jijini Dar es Salaam. Nilifuatilia kuanzia maelezo yake;maswali aliyoulizwa;majibu yake na maswali aliyowauliza wauliza maswali.

Lipo jambo la kikatiba ambalo Spika Ndugai amelizungumza ili kujenga hoja yake kuwa kauli ya Prof. Assad juu ya udhaifu wa Bunge imemgusa hadi Rais Magufuli. Spika alisema kuwa Rais ni sehemu ya Bunge. Hilo nakubaliana na Spika Ndugai.

Lakini, katika utendaji wa Bunge, Rais huwa sehemu ya Bunge katika masuala mawili tu: katika utungaji wa Sheria na katika masuala ya kibajeti. Katika masuala mengine kama kuisimamia Serikali, Rais 'si' sehemu ya Bunge. Rais hawezi 'kujisimamia' mwenyewe akiwa sehemu ya Bunge na mkuu wa Serikali kwa upande mwingine.

Kauli ya Prof. Assad, kwa uelewa wangu, ililenga kwenye wajibu wa Bunge katika kuisimamia Serikali hasa katika kuhakikisha matumizi yanakuwa sawa na ufisadi unadhibitiwa. Katika hilo, Rais hawi sehemu ya Bunge. Hivyobasi, kauli ya Prof. Assad haikumhusu Rais Magufuli kama Spika Ndugai anavyotaka kutuaminisha.

Nasema tena kuwa kauli ya Prof. Assad haikumhusu Rais, Waziri Mkuu au Baraza la Mawaziri. Ililihusu Bunge katika muktadha na sura ya kuisimamia Serikali kwa kuisimamia na kutekeleza mapendekezo ya CAG kwenye Ripoti zake.

Si vyema kumleta Rais, Waziri Mkuu na Mawaziri kwenye sakata hili ili ionekane kuwa Prof. Assad amewakosea hata wakuu wake. Halafu, lugha ya staha iwe inatumika wakati wa kuipinga lugha inayodaiwa kuwa ni ya kuudhi. Vijembe na kejeli hazijengi.

Hakukuwa na haja ya kumshauri Prof. Assad kujiuzulu au kwenda kwa Rais kuzungumza naye kwa sababu mbili. Kwanza, azimio la Bunge limeshamwadhibu kwa kutofanya naye kazi na si kumshauri ajiuzulu. Pili, Prof. Assad hana mgogoro wowote na Rais ili akazungumze naye kwa kuomba radhi. Katika kuisimamia Serikali,Rais 'si' sehemu ya Bunge.
 
... Ndugai anajaribu kila namna kumburuza (drag) Rais kwenye huu "mgogoro" usio na kichwa wala miguu! Anajaribu kutafuta support from the highest authority! Hebu aachane na hayo mambo; Bunge litekeleze jukumu lake la msingi la kuismamia Serikali. Na uzuri kila kitu kimo kwenye ripoti za CAG, kazi ya Bunge ni kutoa maagizo na kuhakikisha yanatekelezwa; as simple as that.
 
Nilibahatika kufuatilia mkutano wa Spika Ndugai na Waandishi wa Habari alioufanya jana jijini Dar es Salaam. Nilifuatulia kuanzia maelezo yake;maswali aliyoulizwa;majibu yake na maswali aliyowauliza wauliza maswali.

Lipo jambo la kikatiba ambalo Spika Ndugai amelizungumza ili kujenga hoja yake kuwa kauli ya Prof. Assad juu ya udhaifu wa Bunge imemgusa hadi Rais Magufuli. Spika alisema kuwa Rais ni sehemu ya Bunge. Hilo nakubaliana na Spika Ndugai.

Lakini, katika utendaji wa Bunge, Rais huwa sehemu ya Bunge katika masuala mawili tu: katika utungaji wa Sheria na katika masuala ya kibajeti. Katika masuala mengine kama kuisimamia Serikali, Rais 'si' sehemu ya Bunge. Rais hawezi 'kujisimamia' mwenyewe akiwa sehemu ya Bunge na mkuu wa Serikali kwa upande mwingine.

Kauli ya Prof. Assad, kwa uelewa wangu, ililenga kwenye wajibu wa Bunge katika kuisimamia Serikali hasa katika kuhakikisha matutumizi yanakuwa sawa na ufisadi unadhibitiwa. Katika hilo, Rais hawk sehemu ya Bunge. Hivyobasi, kauli ya Prof. Assad haikumhusu Rais Magufuli kama Spika Ndugai anavyotaka kutuaminisha.

Nasema tena kuwa kauli ya Prof. Assad haikumhusu Rais, Waziri Mkuu au Baraza la Mawaziri. Ililihusu Bunge katika muktadha na sura ya kuisimamia Serikali kwa kuisimamia na kutekeleza mapendekezo ya CAG kwenye Ripoti zake.

Si vyema kumleta Rais, Waziri Mkuu na Mawaziri kwenye sakata hili ili ionekane kuwa Prof. Assad amewakosea hata wakuu wake. Halafu, lugha ya staha iwe inatumika wakati wa kuipinga lugha inayodaiwa kuwa ni ya kuudhi. Vijembe na kejeli hazijengi.

Hakukuwa na haja ya kumshauri Prof. Assad kujiuzulu au kwenda kwa Rais kuzungumza naye kwa sababu mbili. Kwanza, azimio la Bunge limeshamwadhibu kwa kutofanya naye kazi na si kumshauri ajiuzulu. Pili, Prof. Assad hana mgogoro wowote na Rais ili akzungumze naye kwa kuomba radhi. Katika kuisimamia Serikali,Rais 'si' sehemu ya Bunge.

Speaker anatafuta kuungwa mkono na Rais. Ila tayari walishasuka mbinu ya kumng'oa CAG
 
Tuache utani hivi kati ya Ndugai na Prof Assad hatuoni Ndugai ni Liability tu?
Eti nayeye kakomaa kusema Prof ajiuzulu wakati yeye kama Spika sioni kazi anayofanya zaidi ya kula hela zetu.

Yaani Ndugai ameji-rate kama mtu muhimu sana kuendelea kuwepo pale wakati mi naona hana kazi yoyote anayofanya, kwa sasa nafasi ya spika na Humphrey Polepole hawatofautiani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Si vyema kumleta Rais, Waziri Mkuu na Mawaziri kwenye sakata hili ili ionekane kuwa Prof. Assad amewakosea hata wakuu wake.

Nilikua namsikiliza kwa umakini na kumsoma body language yake.. alipotamka hilo juu ya Rais ni kama kaelemewa sasa anahitaji msaada wa haya aliyofikiri wananchi hawatayafatilia.

Kumtaja Rais ni ameonyesha kwamba Rais ambaye tunaamini hana lolote katika hili kwamba yumo..

Inasikitisha kuona viongozi kama yeye anatumia mapaparazi kumfikishia CAG ujumbe wa kumtaka aende kwa Rais.. kwani hawaandikiani barua kiofisho hadi iwe anamrushia kama nenda huko akajieleze.. ya kitaka ajiudhuru.. yaani anasimamia sheria pia mbona hakutaja lolote!!!

Wakili nambie sasa hapa ni akajieleze nini eti? Ajiuzuru kwa lipi haswa? Kasema hataki kufanya nae kazi.. sasa si angekaa kimya.. haya mengine ya nini?

Ndio maana huwa nacheka pale ninapoona wengi hawajui kupanga.. hawafikirii dk 5 itakuwaje na waweje..
 
Nilibahatika kufuatilia mkutano wa Spika Ndugai na Waandishi wa Habari alioufanya jana jijini Dar es Salaam. Nilifuatilia kuanzia maelezo yake;maswali aliyoulizwa;majibu yake na maswali aliyowauliza wauliza maswali.

Lipo jambo la kikatiba ambalo Spika Ndugai amelizungumza ili kujenga hoja yake kuwa kauli ya Prof. Assad juu ya udhaifu wa Bunge imemgusa hadi Rais Magufuli. Spika alisema kuwa Rais ni sehemu ya Bunge. Hilo nakubaliana na Spika Ndugai.

Lakini, katika utendaji wa Bunge, Rais huwa sehemu ya Bunge katika masuala mawili tu: katika utungaji wa Sheria na katika masuala ya kibajeti. Katika masuala mengine kama kuisimamia Serikali, Rais 'si' sehemu ya Bunge. Rais hawezi 'kujisimamia' mwenyewe akiwa sehemu ya Bunge na mkuu wa Serikali kwa upande mwingine.

Kauli ya Prof. Assad, kwa uelewa wangu, ililenga kwenye wajibu wa Bunge katika kuisimamia Serikali hasa katika kuhakikisha matutumizi yanakuwa sawa na ufisadi unadhibitiwa. Katika hilo, Rais hawk sehemu ya Bunge. Hivyobasi, kauli ya Prof. Assad haikumhusu Rais Magufuli kama Spika Ndugai anavyotaka kutuaminisha.

Nasema tena kuwa kauli ya Prof. Assad haikumhusu Rais, Waziri Mkuu au Baraza la Mawaziri. Ililihusu Bunge katika muktadha na sura ya kuisimamia Serikali kwa kuisimamia na kutekeleza mapendekezo ya CAG kwenye Ripoti zake.

Si vyema kumleta Rais, Waziri Mkuu na Mawaziri kwenye sakata hili ili ionekane kuwa Prof. Assad amewakosea hata wakuu wake. Halafu, lugha ya staha iwe inatumika wakati wa kuipinga lugha inayodaiwa kuwa ni ya kuudhi. Vijembe na kejeli hazijengi.

Hakukuwa na haja ya kumshauri Prof. Assad kujiuzulu au kwenda kwa Rais kuzungumza naye kwa sababu mbili. Kwanza, azimio la Bunge limeshamwadhibu kwa kutofanya naye kazi na si kumshauri ajiuzulu. Pili, Prof. Assad hana mgogoro wowote na Rais ili akazungumze naye kwa kuomba radhi. Katika kuisimamia Serikali,Rais 'si' sehemu ya Bunge.
Halafu hata walipoazimia kutofanya kazi na CAG, mbona hakusema MAAZIMIO YA BUNGE NA RAISI..!!? Anamhusisha raisi ili CAG ajisikie kuwa ametenda ubaya Kwa raisi...!!!
 
Nilikua namsikiliza kwa umakini na kumsoma body language yake.. alipotamka hilo juu ya Rais ni kama kaelemewa sasa anahitaji msaada wa haya aliyofikiri wananchi hawatayafatilia.

Kumtaja Rais ni ameonyesha kwamba Rais ambaye tunaamini hana lolote katika hili kwamba yumo..

Inasikitisha kuona viongozi kama yeye anatumia mapaparazi kumfikishia CAG ujumbe wa kumtaka aende kwa Rais.. kwani hawaandikiani barua kiofisho hadi iwe anamrushia kama nenda huko akajieleze.. ya kitaka ajiudhuru.. yaani anasimamia sheria pia mbona hakutaja lolote!!!

Wakili nambie sasa hapa ni akajieleze nini eti? Ajiuzuru kwa lipi haswa? Kasema hataki kufanya nae kazi.. sasa si angekaa kimya.. haya mengine ya nini?

Ndio maana huwa nacheka pale ninapoona wengi hawajui kupanga.. hawafikirii dk 5 itakuwaje na waweje..
Mnaumbuka kumtetea huyo mtu wenu sasa kaankwa hadharani.
 
Mh. Job Ndugai kuna mahali alijichanganya, au alichanganyikiwa akaanza kuikosoa ripoti yenyewe (alitoa mfano kwamba aliyeenda kukagua alikaa siku moja badala ya tatu!)....akamchanganya na Mh. Rais kwenye hoja zake.

Alisema usiutukane mkono unaokulisha pia.
Hataki kuangalia ukweli kwamba katiba kwa makusudi imemlinda CAG ili asiogope kufanya kazi yake kwa kigezo cha anayemlisha (anayemlipa mshahara), kawekewa mazingira ya kutoogopa kuondolewa kwenye nafasi yake anapoona serikali ina matumizi mabaya.

Nilibahatika kufuatilia mkutano wa Spika Ndugai na Waandishi wa Habari alioufanya jana jijini Dar es Salaam. Nilifuatilia kuanzia maelezo yake;maswali aliyoulizwa;majibu yake na maswali aliyowauliza wauliza maswali.

.......

Hakukuwa na haja ya kumshauri Prof. Assad kujiuzulu au kwenda kwa Rais kuzungumza naye kwa sababu mbili. Kwanza, azimio la Bunge limeshamwadhibu kwa kutofanya naye kazi na si kumshauri ajiuzulu. Pili, Prof. Assad hana mgogoro wowote na Rais ili akazungumze naye kwa kuomba radhi. Katika kuisimamia Serikali,Rais 'si' sehemu ya Bunge.
 
Nilikua namsikiliza kwa umakini na kumsoma body language yake.. alipotamka hilo juu ya Rais ni kama kaelemewa sasa anahitaji msaada wa haya aliyofikiri wananchi hawatayafatilia.

Kumtaja Rais ni ameonyesha kwamba Rais ambaye tunaamini hana lolote katika hili kwamba yumo..

Inasikitisha kuona viongozi kama yeye anatumia mapaparazi kumfikishia CAG ujumbe wa kumtaka aende kwa Rais.. kwani hawaandikiani barua kiofisho hadi iwe anamrushia kama nenda huko akajieleze.. ya kitaka ajiudhuru.. yaani anasimamia sheria pia mbona hakutaja lolote!!!

Wakili nambie sasa hapa ni akajieleze nini eti? Ajiuzuru kwa lipi haswa? Kasema hataki kufanya nae kazi.. sasa si angekaa kimya.. haya mengine ya nini?

Ndio maana huwa nacheka pale ninapoona wengi hawajui kupanga.. hawafikirii dk 5 itakuwaje na waweje..
@cocochanel Kuna Watu wame hack account yako?

Wanalumumba kumbe Kuna muda mnakuwa na akili eeh?
 
Tuache utani hivi kati ya Ndugai na Prof Assad hatuoni Ndugai ni Liability tu?
Eti nayeye kakomaa kusema Prof ajiuzulu wakati yeye kama Spika sioni kazi anayofanya zaidi ya kula hela zetu.

Yaani Ndugai ameji-rate kama mtu muhimu sana kuendelea kuwepo pale wakati mi naona hana kazi yoyote anayofanya, kwa sasa nafasi ya spika na Humphrey Polepole hawatofautiani

Sent using Jamii Forums mobile app
halafu kejeli eti Asaad anependa kujiita profesa na kuona wengine ni wajinga wajinga. akasema Ulaya maprofesa hawapendi kuitwa maprofesa. hii ina maana gani! kwamba huo uprofesa si chochote au. naona kama ilikuwa personal attack. na waliosikiliza hawajatoa credit yoyote. conference ilikuwa ni faida kwa wasikilizaji kuliko kwa aliyeiitisha. watu wamejifunza mengi sana
 
Nilikua namsikiliza kwa umakini na kumsoma body language yake.. alipotamka hilo juu ya Rais ni kama kaelemewa sasa anahitaji msaada wa haya aliyofikiri wananchi hawatayafatilia.

Kumtaja Rais ni ameonyesha kwamba Rais ambaye tunaamini hana lolote katika hili kwamba yumo..

Inasikitisha kuona viongozi kama yeye anatumia mapaparazi kumfikishia CAG ujumbe wa kumtaka aende kwa Rais.. kwani hawaandikiani barua kiofisho hadi iwe anamrushia kama nenda huko akajieleze.. ya kitaka ajiudhuru.. yaani anasimamia sheria pia mbona hakutaja lolote!!!

Wakili nambie sasa hapa ni akajieleze nini eti? Ajiuzuru kwa lipi haswa? Kasema hataki kufanya nae kazi.. sasa si angekaa kimya.. haya mengine ya nini?

Ndio maana huwa nacheka pale ninapoona wengi hawajui kupanga.. hawafikirii dk 5 itakuwaje na waweje..
Well said Coco
 
... Ndugai anajaribu kila namna kumburuza (drag) Rais kwenye huu "mgogoro" usio na kichwa wala miguu! Anajaribu kutafuta support from the highest authority! Hebu aachane na hayo mambo; Bunge litekeleze jukumu lake la msingi la kuismamia Serikali. Na uzuri kila kitu kimo kwenye ripoti za CAG, kazi ya Bunge ni kutoa maagizo na kuhakikisha yanatekelezwa; as simple as that.
usichokijua ni dhahiri si azimio lake ila anawakilisha watu fulani wenye nia yao ovu wakati wanasifa ya utukufu!
 
Back
Top Bottom