Nakosoa: Si sahihi kufuta kila posho na mafunzo kwa watumishi wa umma

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Nov 25, 2010
6,135
17,802
Kwa nchini kwetu Tanzania, kuwa mtumishi wa umma ni kuonesha uzalendo mkubwa. Hii ni kwakuwa, watumishi wa umma Tanzania wanalipwa mishahara kidogo kulinganisha na watumishi wa sekta binafsi.

Watumishi wa umma ni wazalendo kwelikweli. Hawarudishwi nyuma na mishahara na marupurupu yao kiduchu. Wanaendelea kujenga Taifa lao kupitia utumishi wao. Siyo siri, watumishi wa umma huishi kwa posho na mafunzo.

Watumishi wa umma huwa na amani moyoni wanapokuwa na 'viposho' vya hapa na pale. Hii ni kwakuwa, mishahara yao humezwa na mikopo,kodi za Serikali, michango katika mifuko ya hifadhi ya jamii,michango ya afya, michango ya vyama vya wafanyakazi na kadhalika.

Mtumishi anapopata 'kasafari' ka mafunzo ndani au nje ya Tanzania, huyasahau maumivu yake na kusonga mbele kuelekea kwenye kilele cha mafanikio yake. Kufutafuta kila posho au mafunzo kwa mtumishi wa umma ni kumuumiza maumivu yasiyoweza kupozwa.

Posho na mafunzo (visafarisafari) humpa chachu ya utendaji mtumishi wa umma. Mtumishi wa umma hastahili kuishi kama 'shetani'!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
 
Kwa nchini kwetu Tanzania, kuwa mtumishi wa umma ni kuonesha uzalendo mkubwa. Hii ni kwakuwa, watumishi wa umma Tanzania wanalipwa mishahara kidogo kulinganisha na watumishi wa sekta binafsi.

Watumishi wa umma ni wazalendo kwelikweli. Hawarudishwi nyuma na mishahara na marupurupu yao kiduchu. Wanaendelea kujenga Taifa lao kupitia utumishi wao. Siyo siri, watumishi wa umma huishi kwa posho na mafunzo.

Watumishi wa umma huwa na amani moyoni wanapokuwa na 'viposho' vya hapa na pale. Hii ni kwakuwa, mishahara yao humezwa na mikopo,kodi za Serikali, michango ya afya, michango ya vyama vya wafanyakazi na kadhalika.

Mtumishi anapopata 'kasafari' ka mafunzo ndani au nje ya Tanzania, huyasahau maumivu yake na kusonga mbele kuelekea kwenye kilele cha mafanikio yake. Kufutafuta kila posho au mafunzo kwa mtumishi wa umma ni kumuumiza maumivu yasiyoweza kupozwa.

Posho na mafunzo (visafarisafari) humpa chachu ya utendaji mtumishi wa umma. Mtumishi wa umma hastahili kuishi kama 'shetani'!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
Kwa serikali ya sasa mtumish wa umma hana faida kabisa kwa taifa lake anaonekana kama mtu anaye lipwa mshahara bila kazi ,hana thaman tena mtumish huyu amekuwa mtumwa aisye thaminiwa ,anathaminiwa kwa kupewa mshahara wakazi tu lakin si kuheshimiwa na kiithaminiwa kama chanzo cha mapato na maendeleo kwa serikali ,hakuna siku ya faraja kwa mtumishi wa umma ,yeye kila uchao nikusubiri leo nitatishiwa nini na nani atasema nini kumfukuza nani ,viongozi hawamjui wanae muongoza wamemtoa mtumishi wa umma kwenye kundi la watanzania
 
Chadema mtaacha lini kutetea ujinga?hizo posho wanalipana maafisa wachache ndani ya halmashauri ,watumishi wanaofanya kazi kama walimu,madaktari,manesi nk.hizo posho hawazipati posho ya Chai na vitafunwa inatafunwa kwenye majengo ya halmashauri tu hao watumishi wengine ambao ndiyo wengi hawazipati.
Ni bora wazitoe zikajenge madarasa,zahanati na Barabara.
 
Kwa utawala huu watumishi wa umma ni mafisadi, wezi, wazembe, wala rushwa, hii ndiyo dhana inayojengwa na utawala huu, sasa akae atulie asubiri retaliation ya watumishi wa umma na hasa intellectuals
 
Mkuu ameshasema wasomi wako wengi mitaani ana uwezo wa kufukuza wafanyakazi wote waliopo na akaajiri wengine bila nchi kutetereka!
 
Kwa serikali ya sasa mtumish wa umma hana faida kabisa kwa taifa lake anaonekana kama mtu anaye lipwa mshahara bila kazi ,hana thaman tena mtumish huyu amekuwa mtumwa aisye thaminiwa ,anathaminiwa kwa kupewa mshahara wakazi tu lakin si kuheshimiwa na kiithaminiwa kama chanzo cha mapato na maendeleo kwa serikali ,hakuna siku ya faraja kwa mtumishi wa umma ,yeye kila uchao nikusubiri leo nitatishiwa nini na nani atasema nini kumfukuza nani ,viongozi hawamjui wanae muongoza wamemtoa mtumishi wa umma kwenye kundi la watanzania
Hameni, kuna vijana kibao wanatafuta kazi na watafanya kwa uzalendo uliotukuka.
 
Chadema mtaacha lini kutetea ujinga?hizo posho wanalipana maafisa wachache ndani ya halmashauri ,watumishi wanaofanya kazi kama walimu,madaktari,manesi nk.hizo posho hawazipati posho ya Chai na vitafunwa inatafunwa kwenye majengo ya halmashauri tu hao watumishi wengine ambao ndiyo wengi hawazipati.
Ni bora wazitoe zikajenge madarasa,zahanati na Barabara.
Asante sana mkuu kwa mchango wako, hao jamaa ambao hawafiki hata ratio ya 7:100 eti ndio wanadai wataathiri kura za 2020! Hiyo posho wanaonufaika ni hao mabosi wa kwenye viyoyozi ndani ya ofisi za manispaa.
 
Kwa mwelekeo huu, watumishi wa umma hakika watajitambua na kuwa makini kuviishi vyama vya wafanyakazi na kuhakikisha vinakuwa relevant kwao. Huko nyuma watumishi wa umma hawakujali trade unionism, wakikejeli jitihada za vyama hivyo na viongozi wake kuwa ni kelele za wafanyakzi waliokosa marupurupu. Sasa taifa linaelekea kuimarika.
 
Ila mm nlimuelewa sana aliposema mapato yanakusanywa na wafanyakazi wengi lakini bajeti ya chai na vitafunwa ni kwa wachache wanaojiita wakubwa hili kweli ni tatizo kumekuwa na matabaka yaan wale wanaofanya kazi nzito mshahara kidogo na hakuna posho ila kwa hao wakubwa wenye mishahara mikubwa ndo kwenye chai na vitafunwa...
 
Nakuunga mkono, hawa watumishi waachane na serikali ama wamgomee mwajiri tu. Hapa ilikuwa huyu WM aulize na ahakikishe ile posho inatumika kama ilivyokusudiwa na siyo kuifuta. Bunge lilipitisha na yeye akiwemo, awaachie posho zao kama yeye anavyozipata ofisini kwake. Rais amesema siyo tu kwavile wewe una madaraka unaamua tu, unapandisha gharama ama unafuta posho (hii ipo kisheria; kumbuka kuwa bajeti inapita kama sheria bungeni na posho zilipita pale)
 
Kumbe hapo umeguswa eeeeh

Ile unaripoti kutoka huku sijui kule kwishney

Hapa kazi tu
 
Kwa hiyo mleta uzi unafurahia wachache kufaidi hizo posho na sie WAKATA NYASI hatupati hata hiyo chai! yaani sasa mnachofanya ni kubeza kila jambo linaloazimiwa na serikali ili kuwajengea watu au wananchi wawe na hasira juu ya serikali yao iliyoko madarakani!
 
Chadema mtaacha lini kutetea ujinga?hizo posho wanalipana maafisa wachache ndani ya halmashauri ,watumishi wanaofanya kazi kama walimu,madaktari,manesi nk.hizo posho hawazipati posho ya Chai na vitafunwa inatafunwa kwenye majengo ya halmashauri tu hao watumishi wengine ambao ndiyo wengi hawazipati.
Ni bora wazitoe zikajenge madarasa,zahanati na Barabara.
kwani waalimu wanalipwa? mbona kila siku wanalalamiika ?
 
Kwa hiyo mleta uzi unafurahia wachache kufaidi hizo posho na sie WAKATA NYASI hatupati hata hiyo chai! yaani sasa mnachofanya ni kubeza kila jambo linaloazimiwa na serikali ili kuwajengea watu au wananchi wawe na hasira juu ya serikali yao iliyoko madarakani!
mmmh
 
mzee tupatupa,hupendi tuishi kama mashetani??mkuu anapenda kuona tukiishi kama mashetani lakin yeye akiishi kama malaika mtoa roho.
 
Back
Top Bottom