Kalumbesa
JF-Expert Member
- Nov 24, 2010
- 1,013
- 356
Habari wanajukwaa;
Kama alivyoahidi BUKOBA BOY kwenye maelezo yake yaliyoambatana na video ya LWAKATARE kwamba atakuwa anatupa ushahidi mmoja baada ya mwingine, Amesharusha karatasi aliyokuwa anaitumia Lwakatare kuchukua Note/Summary wakati anatoa maelekezo kwa kijana wake kwenda kuandaa mazingira ya utekaji.
Inayoonekana juu kulia kwenye karatasi ni namba ya MSACKY, Mwandishi wa habari wa mwananchi ambaye ni target mojawapo katika kutekwa. Wale waliosema kwamba ile video ni ya uongo wajiridhishe sasa kwamba BUKOBA BOY ana full data na amejiimarisha.
Wakubali sasa kwamba huu ni mwandiko wa LWAKATARE NA HAYO NI BAADHI YA MANENO ALIYOYATAMKA KWENYE VIDEO YAKE.
Zaidi unaweza kutembelea youtube japo haionekani vizuri.. NAOMBA MODS WAIKUZE HAPA JF ILI WASOMAJI WASIPATE SHIDA. KARATASI YENYEWE HII HAPA CHINI
Wakuu kuwekwa kwa haya maandishi hapa ni Uthibitisho tosha kwamba hii inshu ni famba..Kwa nini?
1. Katika maelezo ya Lwakatare anaanza kwa kusema "Nilitaka kujua specifically gari anayotumia...sikia bwana...gari analotumia(hapa anaonekana akiandika sawa) Kwenda mbali zaidi kujua namba" Hapo kwenye bold kuna ujinga wa kimagamba..anamweleza jamaa wanapaswa kufanya juhudi kujua gari anayotumia na wasiishie hapo waendelee zaidi na kujua namba yake! Sasa kwa maelezo haya Lwakatare anajua namba ya mlengwa haijui? Kama haijui inaonekana vipi kuandikwa katika haya maelezo tunayoelezwa kaandika Lwakatare? Lwakatare haonekani kabisa kuandika hii namba.. Pia Great thinkers wenzangu sikilizeni hii video kwa makini,mkiwa sambamba na kutazama haya maandishi mtagundua kuna sehemu Lwakatare anaonekana kuandika maneno ambayo kwenye karatasi hii hayapo..Hivi upuuzi hii CCM mmeandaliwa na hawa madogo waliopata division zero?