Elections 2010 Nakaaya arudisha kadi ya CHADEMA

Uncle Rukus

JF-Expert Member
Jun 16, 2010
2,415
398
Nakaaya Sumari amerudisha kadi ya Chadema jioni ya leo na kumkabidhi JK kwenye mkutano wake ulio fanyika leo mkoani Arusha, JK amempongeza sana kwa kitendo hicho na kumwambia karibu mama CCM ndicho chama pekee Tanzania.
 
Safari njema,CHADEMA si mtu ni watu. Huyu likuja CHADEMA kwa maslahi binafsi ambayo hakuyapata .Ningesikitika kama ningesikia Halima Mdee kaenda CCM.
 
Safari njema,CHADEMA si mtu ni watu. Huyu likuja CHADEMA kwa maslahi binafsi ambayo hakuyapata .Ningesikitika kama ningesikia Halima Mdee kaenda CCM.

Kweli mkuu,

Nakaya ni msichana strong sana. Siwezi kuspeculate kilichopelekea yeye kuhama ila namtakia kila la heri kokote atakakokuwa. Leo nimesikia kama nilivyojisikia siku Masumbuko Lamwai alivyorudi CCM.
 
Msanii mwingine mwenye njaa. Ni wale wale waimbao mapambio mchana usiku kona za barakuda jufukuzia mshiko
 
Msanii mwingine mwenye njaa. Ni wale wale waimbao mapambio mchana usiku kona za barakuda jufukuzia mshiko

Hao ndio wana-demokrasia... du! kazi tunayo... subirini mwishoni mwa kampeni, watafululiza watu kwenda chama kinachokaribia kushinda... wanasiasa bwana wao kazi kuangalia upepo unavuma vipi.
 
Hii kuhama chama inaweza hata kumnyang'anya washabiki wa muziki wake. Labda awe ameamua kufanya siasa kazi na ahadi ya uDC
 
karibu duniani DADA NAKAYA! Finally umekuja mwangani toka Gizani....
 
Hao ndio wana-demokrasia... du! kazi tunayo... subirini mwishoni mwa kampeni, watafululiza watu kwenda chama kinachokaribia kushinda... wanasiasa bwana wao kazi kuangalia upepo unavuma vipi.

Hawa hatuwezi kuwaita wanasiasa hawa! Mi jana niliona pikipiki hizi sijui Tonda, Jeydee, sijui Jinyee nk wote walilipwa 10,000 kupamba Moshi. Hawa noa tutawaita wanasiasa? Ukilinganisha wimbo fulani wa Nakaya na huko alikokimbilia basi ujue huyu sio mwanamapinduzi wa kweli. Anajaribu kufurahisha tu na wala haliko moyoni mwake. Aliitafuta hii nafasi sana ya kusalimiana na Kaka JK. Nakaya anazijua SIFA za Kaka.
 
OOhh Nakaya umepotea watakutumia kama Co....m wakimaliza wanaachana na wewe! Yote maisha kila laheri
 
Sela ya ccm haipo bali kujaribu kuwanunua au usanii hatusikii chochote mbali ahadi hewa na nani karudisha kadi hii kwao wanaona tija aangalie kikwete asiwe ananadanganywa kama ilivyokua Mbeya.MUNGU IBARIKI TANZANIA
Msanii mwingine mwenye njaa. Ni wale wale waimbao mapambio mchana usiku kona za barakuda jufukuzia mshiko
 
Sidhani kama kuna makosa kwa Nakaaya kuhama. Mimi namtakia kila la heri.
Kama juzi alivyokuwa chadema nilimsapoti kwa maamuzi yake, nitaendelea pia kusapoti maamuzi yake ya kujiunga na mafisadi wa ccm.

Hii kazi ya kupingana na ccm yataka moyo. Nakaya bado ni binti mdogo, ngoja ajaribu pia maisha huko kwa mafisadi kwa raha zote.\

HOngera Nakaaya na kila la heri dada.
 
Nakaaya Sumari ameamua kujitosa katika kinyang"anyiro cha kuwania ubunge wa viti maalumu mkoani Arusha kupitia chama cha demokarisia na maendeleo (Chadema) kwa kuchukua fomu ya kugombea nafasi hiyo mjini Arusha.
nakaayasiasa.jpg
Nakaaya ambaye ni katibu mhamasishaji wa baraza la vijana la Chadema wilayani Arusha alichukua fomu ya kuwania kiti hicho juzi katika ofisi za chama hicho zilizopo maneeo ya Esso jengo la Meru Plaza mjini Arusha.
Akiwa ameongozana na mwenyekiti wa vijana wa Chadema wilaya ya Arsuha. Exaud Mamuya sanjari na katibu wa vijana, Arnold Kamnde, mgombea huyo alichukua fomu ya kuwania kiti hicho majira ya saa 3:30 asubuhi katika ofisi hizo.
Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa fomu ya kuwania kiti hicho Nakaaya alisema ya kuwa binafsi anahisi ya kuwa nafasi ya yeye kuwa mwakilishi wa wanawake wa mkoa wa Arusha katika bunge la jamhuri nchini kupitia chadema mkoani Arusha umewadia.
Nakaaya alisema ya kuwa lengo kubwa lililomsukuma kuwania nafasi hiyo ni kutokana na uchungu alionao hususani mateso wanayopata wakinamama katika masusla ya afya ya uzazi katika huku akihaidi kusimamia masula ya afya ya uzazi kwa wakianamama nchini.
"Nahisi muda umefika wa kutenda ninayoyahubiri siku zote,nataka nikasimamie matatizo ya uzazi kwa wakinamama hili linanipa uchungu katika maisha yangu siku zote.Nataka nikawawakilishe wanawake wa mkoa wa Arusha kupitia chama changu nina imani nitashinda nafasi hii kwasababu ninajiamini, hivyo naomba mniunge mkono wanawake'alisema Nakaaya.
Awali akimkabidhi fomu ya kuwania nafsi hiyo katibu wa Chadema wilayani Arusha,Bakari Kasembe aliwataka wanawake wote wa mkoa wa Arusha kupitia chama hicho kujitokeza kwa wingi kuwania nafasi hiyo.
Kasembe alisistiza ya kuwa awali chama chao hakikuwa na uwakilishi wa kiti hicho mkoani Arusha katika bunge la jamhuri nchini lakini wakati huu wamejipanga kutoa viti vitatu na kiti cha ubunge wa Arusha mjini.
Tayari joto la kuwania nafasi ya ubunge wa viti maalumu mkoani Arusha kupitia chama hicho limeanza kushika kasi ambapo hadi sasa tayari wagombea wawili wameshajitokeza kuwania kiti hicho ambao ni Magreth Olotu na Joyce Muya.

From: http://www.wahapahapa.com/index.php?modules=news&sub&op=read&id=493

VIPI UBUNGE ALIKWAMA? Pole sana mama....... Rudi ukale hela za kodi yetu na migodi. Ila angalia usije ukawa umekosea.
 
Miaka ya juzi juzi uliomba kura zeetu, ahadi tele lalalaaaaaaaaaa. Sasa ataimba nini. Hebu tuwekee kale kawimbo kake. Aibu sana tena na machalii wa pale Ar town walivy na hasira balaa analo
 
Miaka ya juzi juzi uliomba kura zeetu, ahadi tele lalalaaaaaaaaaa. Sasa ataimba nini. Hebu tuwekee kale kawimbo kake. Aibu sana tena na machalii wa pale Ar town walivy na hasira balaa analo

Huwezi kujua mkuu, labda anadhani kuwa akipewa ukuu wa wilaya atasaidia wanawake na watoto wale aliokuwa akiwapigania.

Again, kila la heri Nakaaya.
 
[video]http://www.weloveafricans.com/video_player/videoid/14284/nakaaya-feat-m1---mr-politician[/video]
 
Back
Top Bottom