Wadau wakati mwingine katika maisha tunafanya mambo ambayo ukikaa utulie unajiona mpumbavu na kutoamini kama kweli ni wewe umefanya au ulirukwa na akili.
Mkasa ulio nikuta ni matokeo ya uzembe wangu ambao naujutia hakuna mfano, so naomba ushauri wako badala ya kuendelea kunihukumu kwani tayari nimejifunza
Mwaka juzi tulienda kwenye shughuli fulani mkoani kwetu kwa wiki mbili, na katika katiza katiza za hapa na pale nikapata kabinti kamoja nikaanza nako uhusiano huku nikiwa na mke wangu na watoto wawili ambao niliwaacha Dar,
Kibaya zaidi mazingira tuliyokuwepo kondom zikawa hakuna na nikafanya kosa la mwaka kwa kujamiiana naye bila kinga.
Baada ya shughuli kwisha nikarudi Dar na kuendelea na maisha na nikawa sina tena mawasiliano na yule binti kwani alikuwa hana simu,hata hivyo ilikuwa ni kama hit and run
Sasa mwezi machi nikaenda likizo mkoa na familia, tukiwa katika wiki ya mwisho kama bahati nikakutana na yule binti akiwa na rafiki yake wote wamebeba watoto, basi yule binti kuniona tu alishtuka na kupiga kelele almanusura anguke na kuzirai, akaja akanikumbatia na kunishikilia kwanguvu huku akilia na kuongea maneno yaliyonichangaya kabisa.
Ikabidi tutafute sehemu tukae atulie kisha akamtoa mtoto mgongoni na yule wa rafiki yake akasema wanao hawa wako mapacha.
Kiukweli nilipo waona tu roho ilipasuka maana kitu fotokopi,huitaji hata mtaalamu kubaini kama wale watoto ni wangu kwani tumefanana nao mno.
Baada ya maongezi marefu nikajiridhisha kuwa watoto kweli ni wangu kwa mujibu wa maelezo yake na mfanano wa watoto.
Na akanieleza jinsi alivyohangaika kunitafuta kwani hakuwa hata anajua ninapokaa nikiwa mkoa na jina nilimpa la uongo hivyo na watoto kawapa jina hilo kama ubini wao.
Ilibidi nimpatie pesa ya matumizi kwanza palepale na nikachukua tax na kuwapeleka kwao kwa ahadi kuwa nikapajue kwao kisha kesho yake ntakwenda na wazee kujitambulisha kama mimi ni baba wa watoto wale,akanipa namba zake za simu alikuwa nayo nikazuga nita mbeep nkiweka vocha kisha nikaondoka bila kushuka na kusalimia kwao na nikamwambia asiseme kitu kwanza nijipange kwani anaishi na wazazi wake.
Niliporudi home nikajiuliza usiku kucha sikupata majibu,
Nampenda mke wangu na ananiamini sana kila nikifikiaria akijua akili haikubali, nahisi nitaharibu familia yangu
Baada ya tafakuri ya muda mrefu nikafanya maamuzi ambayo nayo naona yanaanza kunishinda ndio maana nipo hapa kwa ushauri wenu.
Nilichoamua ni kuhakikisha natunza siri hii peke yangu, nikaamua kesho yake nikanunua line mpya ya simu na kuisajili jina lile feki nikampigia simu kuwa nimepata dharura nimeondoka alfajiri na nikamtumia pesa laki3 kwaajili ya matumizi na kuahidi nitarudi soon.
Baada ya hapo nikamaliza wiki yangu mkoa nikiwa nashinda home tu hadi nilipoondoka na familia kurudi Dar.
Huu ni mwezi wa 6 sasa ninachofanya ni kila mwezi natuma laki moja ya matumizi kwa ile line na kama anataka kunitaarifu kitu labda watoto wanaumwa basi atatuma meseji na mimi kila siku jioni huwa naweka line ile kwa muda mchache na kuangalia kama kuna ujumbe au nataka kujua jambo then naitoa.
Nafanya haya yote kujaribu kuprotect familia yangu lakini pia kuhakikisha watoto wale wanapata huduma kama watoto wengine.
Siku za karibuni presure toka kwa wazazi wa yule binti imekuwa kubwa, wanataka kunijua na kubeba jukumu kama baba kweli na si kutuma tu pesa wakati hawamjui mzazi mwenza wa binti yao, wamejaribu sana kuni trace bila mafanikio maana kila nikiwasha ile line jioni nakutana na sms kali kali kuto kwa wazazi wake, wanaongea maneno makali hadi kufikia kunitisha.
Hakuna ndugu yangu anajua maana niliogopa angeweza kusababisha mimi kujulikana kitu ambacho sipo tayari kitokee kwani mke wangu akijua nahofu ya kupoteza furaha ya familia yangu
Lakini pia wakati mwingine nawafikiria wale watoto wanahitaji baba anayeoneka hata kama sita ishi nao .
Pia najiuliza ni kwa muda gani nitaweza kukaa na jambo hili peke yangu huku likinipa hofu na kuniondolea furaha ambayo ndio naogopa kuipoteza kwenye familia yangu
Wakuu naombeni mawazo yenu tafadhali, kama ni kosa limeisha fanyika lakini I feel like I can't hold it anymore, but when I think about my family I got stuck
Mkasa ulio nikuta ni matokeo ya uzembe wangu ambao naujutia hakuna mfano, so naomba ushauri wako badala ya kuendelea kunihukumu kwani tayari nimejifunza
Mwaka juzi tulienda kwenye shughuli fulani mkoani kwetu kwa wiki mbili, na katika katiza katiza za hapa na pale nikapata kabinti kamoja nikaanza nako uhusiano huku nikiwa na mke wangu na watoto wawili ambao niliwaacha Dar,
Kibaya zaidi mazingira tuliyokuwepo kondom zikawa hakuna na nikafanya kosa la mwaka kwa kujamiiana naye bila kinga.
Baada ya shughuli kwisha nikarudi Dar na kuendelea na maisha na nikawa sina tena mawasiliano na yule binti kwani alikuwa hana simu,hata hivyo ilikuwa ni kama hit and run
Sasa mwezi machi nikaenda likizo mkoa na familia, tukiwa katika wiki ya mwisho kama bahati nikakutana na yule binti akiwa na rafiki yake wote wamebeba watoto, basi yule binti kuniona tu alishtuka na kupiga kelele almanusura anguke na kuzirai, akaja akanikumbatia na kunishikilia kwanguvu huku akilia na kuongea maneno yaliyonichangaya kabisa.
Ikabidi tutafute sehemu tukae atulie kisha akamtoa mtoto mgongoni na yule wa rafiki yake akasema wanao hawa wako mapacha.
Kiukweli nilipo waona tu roho ilipasuka maana kitu fotokopi,huitaji hata mtaalamu kubaini kama wale watoto ni wangu kwani tumefanana nao mno.
Baada ya maongezi marefu nikajiridhisha kuwa watoto kweli ni wangu kwa mujibu wa maelezo yake na mfanano wa watoto.
Na akanieleza jinsi alivyohangaika kunitafuta kwani hakuwa hata anajua ninapokaa nikiwa mkoa na jina nilimpa la uongo hivyo na watoto kawapa jina hilo kama ubini wao.
Ilibidi nimpatie pesa ya matumizi kwanza palepale na nikachukua tax na kuwapeleka kwao kwa ahadi kuwa nikapajue kwao kisha kesho yake ntakwenda na wazee kujitambulisha kama mimi ni baba wa watoto wale,akanipa namba zake za simu alikuwa nayo nikazuga nita mbeep nkiweka vocha kisha nikaondoka bila kushuka na kusalimia kwao na nikamwambia asiseme kitu kwanza nijipange kwani anaishi na wazazi wake.
Niliporudi home nikajiuliza usiku kucha sikupata majibu,
Nampenda mke wangu na ananiamini sana kila nikifikiaria akijua akili haikubali, nahisi nitaharibu familia yangu
Baada ya tafakuri ya muda mrefu nikafanya maamuzi ambayo nayo naona yanaanza kunishinda ndio maana nipo hapa kwa ushauri wenu.
Nilichoamua ni kuhakikisha natunza siri hii peke yangu, nikaamua kesho yake nikanunua line mpya ya simu na kuisajili jina lile feki nikampigia simu kuwa nimepata dharura nimeondoka alfajiri na nikamtumia pesa laki3 kwaajili ya matumizi na kuahidi nitarudi soon.
Baada ya hapo nikamaliza wiki yangu mkoa nikiwa nashinda home tu hadi nilipoondoka na familia kurudi Dar.
Huu ni mwezi wa 6 sasa ninachofanya ni kila mwezi natuma laki moja ya matumizi kwa ile line na kama anataka kunitaarifu kitu labda watoto wanaumwa basi atatuma meseji na mimi kila siku jioni huwa naweka line ile kwa muda mchache na kuangalia kama kuna ujumbe au nataka kujua jambo then naitoa.
Nafanya haya yote kujaribu kuprotect familia yangu lakini pia kuhakikisha watoto wale wanapata huduma kama watoto wengine.
Siku za karibuni presure toka kwa wazazi wa yule binti imekuwa kubwa, wanataka kunijua na kubeba jukumu kama baba kweli na si kutuma tu pesa wakati hawamjui mzazi mwenza wa binti yao, wamejaribu sana kuni trace bila mafanikio maana kila nikiwasha ile line jioni nakutana na sms kali kali kuto kwa wazazi wake, wanaongea maneno makali hadi kufikia kunitisha.
Hakuna ndugu yangu anajua maana niliogopa angeweza kusababisha mimi kujulikana kitu ambacho sipo tayari kitokee kwani mke wangu akijua nahofu ya kupoteza furaha ya familia yangu
Lakini pia wakati mwingine nawafikiria wale watoto wanahitaji baba anayeoneka hata kama sita ishi nao .
Pia najiuliza ni kwa muda gani nitaweza kukaa na jambo hili peke yangu huku likinipa hofu na kuniondolea furaha ambayo ndio naogopa kuipoteza kwenye familia yangu
Wakuu naombeni mawazo yenu tafadhali, kama ni kosa limeisha fanyika lakini I feel like I can't hold it anymore, but when I think about my family I got stuck