mwanaharakati_msemahovyo
Member
- Oct 5, 2007
- 6
- 0
Tambwe Hiza ni moja kati ya wananchi wa jamhuri hii waliowahi kuibaka siasa.Ni kinuka mito.Ni mwanasiasa mbinafsi aliyethubutu kuweka maslahi binafsi mbele na kuweka ya taifa kando.Binafsi ninajuta kuwa mwananchi katika nchi ambayo ndugu huyu Tambwe Hiza ni mwananchi pia.
Tambwe ana hulka ya kuandika makala katika baadhi ya magazeti hapa nchini.Aina ya makala anayoyaandika huwa yana muelekeo wa kutaka kuonekana na wakubwa wa nchi hii ambao ni vigogo katika chama tawala ili mradi atupiwe mfupa na mkono wake uende kinywani.
Ukimtafakari kwa kina huyu ndugu,utashawishika kwamba anaweza kuandika makala ambayo yatatetea mtu mkubwa katika chama tawala ili mradi atupiwe mfupa mnono.Hku ni kufilisika kimawazo na ni kiwango cha juu kabisa cha usaliti wa nchi na pia ni kutukana taaluma ya uandishi wa habari.
Majuzi nilisoma makala yake ambayo alijaribu kuwashawishi watanzania ili Rais wa nchi atoe presidential decree kuwasamehe mafiadi walioiba fedha zetu BOT.Huyu ndugu amefikia kiasi cha kuchefua watanzania wenye uzalendo wa kweli na anajaribu kupandikiza mbegu ya ubaguzi na kutoheshimu utawala wa sheria nchini.
Katiba ya jamhuri ya Tanzania inasisitiza kuwa watu wote ni sawa mbele ya sheria.Hakuna mtu awaye yeyote aliyeko juu ya sheria.Tambwe Hiza analeta siasa katika utawala wa sheria.Huyu ndugu ni wa kuogopwa kama ukoma.Uzalendo ndani ya Tambwe Hiza Hauko.Siasa anazoendesha ni ya kulinda tumbo lake hata kama akiuza nchi.Ni siasa chafu ambazo mwaliu alizikataa!!
Tambwe ana hulka ya kuandika makala katika baadhi ya magazeti hapa nchini.Aina ya makala anayoyaandika huwa yana muelekeo wa kutaka kuonekana na wakubwa wa nchi hii ambao ni vigogo katika chama tawala ili mradi atupiwe mfupa na mkono wake uende kinywani.
Ukimtafakari kwa kina huyu ndugu,utashawishika kwamba anaweza kuandika makala ambayo yatatetea mtu mkubwa katika chama tawala ili mradi atupiwe mfupa mnono.Hku ni kufilisika kimawazo na ni kiwango cha juu kabisa cha usaliti wa nchi na pia ni kutukana taaluma ya uandishi wa habari.
Majuzi nilisoma makala yake ambayo alijaribu kuwashawishi watanzania ili Rais wa nchi atoe presidential decree kuwasamehe mafiadi walioiba fedha zetu BOT.Huyu ndugu amefikia kiasi cha kuchefua watanzania wenye uzalendo wa kweli na anajaribu kupandikiza mbegu ya ubaguzi na kutoheshimu utawala wa sheria nchini.
Katiba ya jamhuri ya Tanzania inasisitiza kuwa watu wote ni sawa mbele ya sheria.Hakuna mtu awaye yeyote aliyeko juu ya sheria.Tambwe Hiza analeta siasa katika utawala wa sheria.Huyu ndugu ni wa kuogopwa kama ukoma.Uzalendo ndani ya Tambwe Hiza Hauko.Siasa anazoendesha ni ya kulinda tumbo lake hata kama akiuza nchi.Ni siasa chafu ambazo mwaliu alizikataa!!