Cotton pamba
JF-Expert Member
- Dec 16, 2020
- 303
- 208
Umeandika vema pongezi đź‘Źđź‘Ź
Pole sana kwa unayopitia ndugu!
Napenda tu nkupe ushauri huu kama utaona ni mzuri na unaweza kusaidia basi jaribu kufanya hivi
Umesema umeona Mwenyezi Mungu akitenda katika masomo yako ndio maana umekuja hapa JF kutoa ushuhuda eti? ndio ametenda sasa fanya hivi
Katika maombi yako ya kila siku mueleze Mungu kwamba unahitaji kuendelea na safari muonyeshe yakuwa unaye mtoto ambaye unampenda mwambie kuwa unahitaji kuona akiwa na furaha vivyo hivyo kwako. Basi yeye atakupatia faraja katika namna yake na atakuimalisha pia
Ombi langu ni kuwa usimweleze ya kuwa ni mtu gani wamuitaji nasema hivi kwa sababu yeye alishaandika stori nzuri ya maisha yako ata kabla ya wewe kuwepo hapa
Unachokiona kwa sasa huenda yasiwe mateso labda ni ukurasa tu katika kitabu cha maisha yako lipokee tu hili najua zipo bado kurasa nyingi tu zenye tumaini, faraja na ushindi .
Mwisho kabisa fanya ibada kwenye Mwenyezi Mungu mueleze kila hatua uliyopo mwonyeshe jitihada zako katika kukabili kila unalopitia na kuwa mwenye subra
Poleni sana na Asanteni!