VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,802
Kimbelembele changu kimeniponza. Kimbelembele cha kumtembelea Lissu hospitalini jana kabla ya kurejea hapa nchini. Najuta kumtembelea Lissu. Afadhali nisingekwenda. Mara ya kwanza nilipomtembelea akiwa ICU alinipa salamu zenu na kuwataka kutonyamaza. Maswali magumu.
Jana,nilipomtembelea wodini nje ya ICU,alinimwagia maswali makali yatakayo majibu ya akili. Akaniuliza,nchi yetu ina demokrasia? Nikafurukuta kujibu. Nikasema,ndiyo. Kabla ya kueleza sababu,akanitupia swali lingine:demokrasia ni nini na inaonekanaje? Nikanyamaza. Nikasema natafakari.
Hakuniacha,akaniuliza tena: wewe kama mtanzania,umechangiaje kuimarisha au kufifisha demokrasia na unaridhika na mchango wako? Akaniongeza maswali: vipi kuhusu utawala wa sheria;upo? Unaonekana? Unaweza kuthibitisha? Katiba mpya je? Kwa mkwamo wake,tuanze upya au tukwamue tulikokwama?
Ndani ya dakika tano,wodi ikawa mahakama. Maswali na majibu. Mengi yakaninyamazisha. Nikajiona fisadi wa uoga na ukweli. Nikajiona zuzu kauzu niliyefuzu. Nikamtazama kwa makini. Kama kawaida yake,Lissu looks timamu,makini na to a point. Nikajaribu kubadili mada kama kutoka Ubungo kwenda Kibada. Akagoma,akanicheka kwa dhihaka. Akamalizia: jitafakari sana,Tanzania ni ya watanzania!
Bunduki za nini tena jamani katika kujenga hoja!?
Mzee Tupatupa wa Lumumba (safarini Kibiti,Pwani)
Jana,nilipomtembelea wodini nje ya ICU,alinimwagia maswali makali yatakayo majibu ya akili. Akaniuliza,nchi yetu ina demokrasia? Nikafurukuta kujibu. Nikasema,ndiyo. Kabla ya kueleza sababu,akanitupia swali lingine:demokrasia ni nini na inaonekanaje? Nikanyamaza. Nikasema natafakari.
Hakuniacha,akaniuliza tena: wewe kama mtanzania,umechangiaje kuimarisha au kufifisha demokrasia na unaridhika na mchango wako? Akaniongeza maswali: vipi kuhusu utawala wa sheria;upo? Unaonekana? Unaweza kuthibitisha? Katiba mpya je? Kwa mkwamo wake,tuanze upya au tukwamue tulikokwama?
Ndani ya dakika tano,wodi ikawa mahakama. Maswali na majibu. Mengi yakaninyamazisha. Nikajiona fisadi wa uoga na ukweli. Nikajiona zuzu kauzu niliyefuzu. Nikamtazama kwa makini. Kama kawaida yake,Lissu looks timamu,makini na to a point. Nikajaribu kubadili mada kama kutoka Ubungo kwenda Kibada. Akagoma,akanicheka kwa dhihaka. Akamalizia: jitafakari sana,Tanzania ni ya watanzania!
Bunduki za nini tena jamani katika kujenga hoja!?
Mzee Tupatupa wa Lumumba (safarini Kibiti,Pwani)