Najuta kuhamia kwangu Kerege

hiyo nyumba picha zaidi zipo wapi nikuletee mteja kama bado unauza, ama nipe link ya zoom ulikopost nikacheki
 
Investment ya nyumba siielewi. Labda wajuvi watusaidie. Ukiacha maeneo premium kama Masaki, Obay, Mikocheni na Mbezi (ambako madon wa mji walishagawana) wengine huku kwetu ni kuumizana tuu. Unajenga nyumba standard ya 200M. Halafu uipangishe kwa laki tano....hiyo hesabu kwangu ni ngumu. Mtu unakuta kajipinda na ghorofa lake la maana Bunju au Mapinga..ukiangalia pesa ya kodi kwa mwezi unachoka. Hapo hujaweka wear and tear/uchakavu nk...

Hiyo biashara hapana ngoja tuwaachie wenyewe. Nyumba ambayo haiwezi kuniingizia 1M, minimum, kwa mwezi naona bado ni changamoto kubwa...
 
Hiyo nyumba tafuta mtu wa kukaa akulindie. Wewe panga mjini karibu na kazini kwako au karibu na shule ya watoto kama unao. Ikifika weekend kama ijumaa jioni hivi unaenda kwako unakaa mpaka jpili jioni unarudi town. Huko utakaa mambo yakibadilika au ukishastaafu.
Hongera kwa kujenga nyumba!
 
Wakuu enzi za Neema za Mkwere nilijenga maeneo ya Kerege sasa mambo yalipobana kodi ikanishinda Sinza nikahamia kwangu Kerege asee najuta maana hizo gharama za mafuta zinazidi kodi ya nyumba Sinza (400,000/=).

Kutokana na sasa hela kuwa ngumu nimeweka ukuta mfupi, vibaka kila mara wanavamia nikiwa kazini mjini nimejaribu kuuza nyumba kupitia kwa madalali na Zoom haiuziki wanunuzi wengi wanadai huku uswahilini sana.

Funzo: Vijana msikimbilie kujenga kama hamjajipanga.

Kerege mmekumbukwa na Bandari ya Bagamoyo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom