Dogo Lao
Member
- Nov 2, 2011
- 94
- 38
Ndugu wana Jf, Asalamu aleykum, Tumsifu Yesu Kristo, Bwana Yesu asifiwe.
Baada ya salaam, nianze kwa kusema "ashikhum siyo matusi". Najua, tunao wasomi wengi sana, lakini ukweli ni kwamba idadi yao ni ndogo sana ukilinganisha na vilaza waliojaa.
Mbaya zaidi, vilaza hao ndio waliopewa dhamana ya kutuamulia maisha yetu ya baadaye. Na kwakuwa tupo katika mfumo wa wengi wape, basi kwa wingi wao wamekuwa ni washindi ktk kila jambo pale kura itakapopigwa. Hawa ndio wenye kuamua tuelekee wapi, hawa ndio wenye kuamua vipaombele vyetu, hawa ndio wa kuamua mustakabali wa maisha ya watoto wetu kwa miaka kadhaa ijayo.
Pamoja na umbumbumbu wao, ndio hawa utawakuta wakishikilia nafasi nyeti kabisa za uongozi, ndio hawa ambao wanategemewa kutunga sheria, kuandaa sera, kupitisha mipango ya mapato na matumizi, ndio hawa tunawategemea watuletee maendeleo endelevu.
Wasifu wao, maisha yao na uhalisia wao ni 'kukalili' yaliyosemwa na mtu mmoja wanayeamini kuwa ana akili zaidi yao. Utawajua tu kwa matendo yao, hawawezi kufikiri tofauti na yule wanayemwamini kuwa ndio genius, hawana mtazamo mbadala, wao kazi yao ni kuchekelea na kushabikia tu kile kinachosemwa na genius.
Daima huwa macho yao yamefumbwa na akili zao zimelala kiasi kwamba wapo tayari hata kuzikana jinsia zao ilimradi tu Genius kasema, na wanaamini na kusadiki.
Hawa ndio tumewapa dhamana ya uwakilishi/usimamizi wa rasilimali/utetezi wa maslahi ya wengi.
Kwa aina hii ya watu, wenye akili ndio wanaoumia. Ni bahati mbaya sana maumivu yao hayawezi kuonekana machoni pa vilaza, wala juhudi zao za kuikomboa jamii nzima haitatafsiriwa kama ni hatua muhimu ya maendeleo endelevu. Badala yake juhudi hizo zitavikwa kila aina ya uovu na uonevu, huku zikitafsiriwa kama uhujumu, uchochezi, usaliti na yote yafananayo na hayo.
Kundi hili la vilaza ni kubwa sana, hata JF wapo, na utawajua tu kwa comments zao, hata posts zao, maana huwa ni vigumu sana kuficha ujinga uliostawi kichwani mwa mtu.
Wazo mbadala kwao ni upinzani, na upinzani kwao ni uvunjifu wa amani. Hizo ndizo tafsiri zilizojaa ktk vichwa vyao. Hakika, bado tuna safari ndefu ya kujikomboa. Kujikomboa ninakosema mimi ni ule ukombozi wa fikra, ili hatimaye tafsiri sahihi zianze kufanya kazi sahihi kwa ajili ya matokeo sahihi.
Asanteni.
Baada ya salaam, nianze kwa kusema "ashikhum siyo matusi". Najua, tunao wasomi wengi sana, lakini ukweli ni kwamba idadi yao ni ndogo sana ukilinganisha na vilaza waliojaa.
Mbaya zaidi, vilaza hao ndio waliopewa dhamana ya kutuamulia maisha yetu ya baadaye. Na kwakuwa tupo katika mfumo wa wengi wape, basi kwa wingi wao wamekuwa ni washindi ktk kila jambo pale kura itakapopigwa. Hawa ndio wenye kuamua tuelekee wapi, hawa ndio wenye kuamua vipaombele vyetu, hawa ndio wa kuamua mustakabali wa maisha ya watoto wetu kwa miaka kadhaa ijayo.
Pamoja na umbumbumbu wao, ndio hawa utawakuta wakishikilia nafasi nyeti kabisa za uongozi, ndio hawa ambao wanategemewa kutunga sheria, kuandaa sera, kupitisha mipango ya mapato na matumizi, ndio hawa tunawategemea watuletee maendeleo endelevu.
Wasifu wao, maisha yao na uhalisia wao ni 'kukalili' yaliyosemwa na mtu mmoja wanayeamini kuwa ana akili zaidi yao. Utawajua tu kwa matendo yao, hawawezi kufikiri tofauti na yule wanayemwamini kuwa ndio genius, hawana mtazamo mbadala, wao kazi yao ni kuchekelea na kushabikia tu kile kinachosemwa na genius.
Daima huwa macho yao yamefumbwa na akili zao zimelala kiasi kwamba wapo tayari hata kuzikana jinsia zao ilimradi tu Genius kasema, na wanaamini na kusadiki.
Hawa ndio tumewapa dhamana ya uwakilishi/usimamizi wa rasilimali/utetezi wa maslahi ya wengi.
Kwa aina hii ya watu, wenye akili ndio wanaoumia. Ni bahati mbaya sana maumivu yao hayawezi kuonekana machoni pa vilaza, wala juhudi zao za kuikomboa jamii nzima haitatafsiriwa kama ni hatua muhimu ya maendeleo endelevu. Badala yake juhudi hizo zitavikwa kila aina ya uovu na uonevu, huku zikitafsiriwa kama uhujumu, uchochezi, usaliti na yote yafananayo na hayo.
Kundi hili la vilaza ni kubwa sana, hata JF wapo, na utawajua tu kwa comments zao, hata posts zao, maana huwa ni vigumu sana kuficha ujinga uliostawi kichwani mwa mtu.
Wazo mbadala kwao ni upinzani, na upinzani kwao ni uvunjifu wa amani. Hizo ndizo tafsiri zilizojaa ktk vichwa vyao. Hakika, bado tuna safari ndefu ya kujikomboa. Kujikomboa ninakosema mimi ni ule ukombozi wa fikra, ili hatimaye tafsiri sahihi zianze kufanya kazi sahihi kwa ajili ya matokeo sahihi.
Asanteni.