Paul Alex
JF-Expert Member
- Jul 14, 2012
- 4,240
- 9,527
Majuzi nilishawishiwa na nafsi yangu kutembelea ofisi ya chama angalau kutoa Hi!
Nilitafakari sana magumu ambayo viongozi wanayapitia;
* Ile kushawishiwa kila leo kuunga juhudi za mheshimiwa.
*Kushindwa kufanya mikutano ya kisiasa kuongea na wanachama.
*Zile kesi za kila leo mahakamani na kwenye vituo vya polisi.
*Ile hasira ya kuona viongozi wengine wakifika bei na kuunga mkono juhudi.
Haya na mengine mengi...
Nafsi ikaniambia niwasalimie tu viongozi, angalau niwaambie, Kuna wanachama tunaoelewa yanayoendelea.
Nilifikia kwanza restaurant iliyoko jirani sana na ofisi za chama, umbali wa kurusha jiwe la mkono, ili angalau nichangamshe tumbo. Ajabu ni kuwa, mhudumu wa ile restaurant alidai hafahamu ilipo ofisi ya CHADEMA ila anafahamu ilipo ofisi ya CCM ambayo kimsingi iko Kama umbali wa kilometer 2 kutoka kwenye hiyo restaurant.
Nilipomdadisi kidogo nikagundua ana hofu kuu, hofu ile ile inayowafanya watu wangu wa karibu wanikataze kujihusisha na siasa za CHADEMA wakidai eti ni hatari sana kwa Sasa.
Makamanda ni makamanda tu na ndio maana nawapenda bure.
Nilipoingia ofisini nilikutana na tabasamu, uchangamfu na kujiamini kulikoniacha mdomo wazi.Nadhani mimi ndiye niliyepewa faraja tofauti na wazo langu la kutoa faraja.
Basi, nikalipa madeni ya ada zangu za uanachama na kuwaaga makamanda nikiwa najiamini na mwenye furaha kuliko nilivyoingia.
Makamanda tupeane moyo na mbinu. Tupeane faraja Sasa, tena hasa Sasa ambako tunawindwa kama digidigi au pongo au mnyama mwingine wa porini.
Tupeane faraja sasa wakati ambao kila anayefanikiwa kutukanyaga shingoni anapewa cheo.
Makamanda wenzangu; Pamoja na yote yanayoendelea tumebaki peke yetu tu katika nchi hii Kama matumaini pekee ya demokrasia.
Dawa chungu ndio dawa nzuri- yeah! Nakumbuka- The bitter herb is the better one.
2020 ratio ya polisi kwa raia itakuwa 1:1700 Kama sikosei
Kushindwa Mara moja ni bahati mbaya ila kushindwa Mara ya pili ni upumbavu!
Nilitafakari sana magumu ambayo viongozi wanayapitia;
* Ile kushawishiwa kila leo kuunga juhudi za mheshimiwa.
*Kushindwa kufanya mikutano ya kisiasa kuongea na wanachama.
*Zile kesi za kila leo mahakamani na kwenye vituo vya polisi.
*Ile hasira ya kuona viongozi wengine wakifika bei na kuunga mkono juhudi.
Haya na mengine mengi...
Nafsi ikaniambia niwasalimie tu viongozi, angalau niwaambie, Kuna wanachama tunaoelewa yanayoendelea.
Nilifikia kwanza restaurant iliyoko jirani sana na ofisi za chama, umbali wa kurusha jiwe la mkono, ili angalau nichangamshe tumbo. Ajabu ni kuwa, mhudumu wa ile restaurant alidai hafahamu ilipo ofisi ya CHADEMA ila anafahamu ilipo ofisi ya CCM ambayo kimsingi iko Kama umbali wa kilometer 2 kutoka kwenye hiyo restaurant.
Nilipomdadisi kidogo nikagundua ana hofu kuu, hofu ile ile inayowafanya watu wangu wa karibu wanikataze kujihusisha na siasa za CHADEMA wakidai eti ni hatari sana kwa Sasa.
Makamanda ni makamanda tu na ndio maana nawapenda bure.
Nilipoingia ofisini nilikutana na tabasamu, uchangamfu na kujiamini kulikoniacha mdomo wazi.Nadhani mimi ndiye niliyepewa faraja tofauti na wazo langu la kutoa faraja.
Basi, nikalipa madeni ya ada zangu za uanachama na kuwaaga makamanda nikiwa najiamini na mwenye furaha kuliko nilivyoingia.
Makamanda tupeane moyo na mbinu. Tupeane faraja Sasa, tena hasa Sasa ambako tunawindwa kama digidigi au pongo au mnyama mwingine wa porini.
Tupeane faraja sasa wakati ambao kila anayefanikiwa kutukanyaga shingoni anapewa cheo.
Makamanda wenzangu; Pamoja na yote yanayoendelea tumebaki peke yetu tu katika nchi hii Kama matumaini pekee ya demokrasia.
Dawa chungu ndio dawa nzuri- yeah! Nakumbuka- The bitter herb is the better one.
2020 ratio ya polisi kwa raia itakuwa 1:1700 Kama sikosei
Kushindwa Mara moja ni bahati mbaya ila kushindwa Mara ya pili ni upumbavu!