DidYouKnow
JF-Expert Member
- Jul 28, 2019
- 1,094
- 1,691
Najua tumepoteza wandugu wetu kadhaa kutokana na ugonjwa huu wa COVID-19. Mungu awarehemu marehemu na atupe faraja wafiwa.
Lakini najiuliza kwanini kila kifo kinachotokea sasa kinahusishwa na Coronavirus, hasahasa kikitokea kwa watu mashuhuri. Naamini watu wengi mashuhuri waliokufa kabla ya COVID-19 wangekuwa wamekufa kipindi hiki ingetajwa sababu ya kifo kuwa ni COVID-19.
Hivi ni lini saratani, kiharusi, kisukari, shinikizo la damu, magonjwa nyemelezi na magonjwa mengine mengi sugu na yasiyo sugu yalisimama kusababisha kifo?
Kuna kitu hakiko sawa.
Lakini najiuliza kwanini kila kifo kinachotokea sasa kinahusishwa na Coronavirus, hasahasa kikitokea kwa watu mashuhuri. Naamini watu wengi mashuhuri waliokufa kabla ya COVID-19 wangekuwa wamekufa kipindi hiki ingetajwa sababu ya kifo kuwa ni COVID-19.
Hivi ni lini saratani, kiharusi, kisukari, shinikizo la damu, magonjwa nyemelezi na magonjwa mengine mengi sugu na yasiyo sugu yalisimama kusababisha kifo?
Kuna kitu hakiko sawa.