Najiuliza, hivi wapinzani wakisema waanze sasa kupambana na serikali,CCM watatekeleza ilani yako lini?

MAHANJU

JF-Expert Member
Aug 26, 2014
5,244
7,966
Kuna kitu kinafanywa na serikali yetu na CCM kwa ujumla nadhani bila kufikiria mbali, hivi CCM na serikali yao wanaamini kweli wapinzani wameshindwa kupambana na huu unaoitwa uminnywaji wa demokrasia, uhuru wa kuongea na uvunjwaji holela wa katiba ya nchi?


Kama Upinzani kwa ujumla wana wanachama zaidi ya million 10, wakisema sasa hatutaki nchi nzima watatoka wapi hao polisi wa kuwakamata watu hao nchi nzima? Hizo mahabusu za kujaza wafuasi hao zitatokea wapi? Nafikiri kila maamuzi yanapofikiwa lazima kuwe na kipimo cha kujali utu na kutanguliza busara.

Ni wazi kua hata viongozi wengi wa dini hawajapemdezwa na mienendo ya watawala wa sasa, hivi tunadhani kua Upinani wakichukia watachukia peke yao? tunadhani kua watakosa uungwaji mkono?

Binafsi nafikiri ni viongozi wa upinzani wameamua kutumia busara walao kuepusha malumbano ili maendeleo yafanyike, lakini nina imani wakichukizwa hayo maendeleo itakua ni shida kuyafikia na wala ilani ya CCM haitatekelezwa.Na, hapa CCM watapoteana bila kujua ni wapi walikosea.

Siwezi kuamini kua vyama vilivyojaa wasomi na wanamikakati havijui nini nifanye ili kujinusuru, kufikiria hivyo ni ukosefu wa uelewa. Busara na hekima ni kitu cha msingi sana, kutumia nguvu kuwanyamazisha watu ambao wameamua kukaa kimya kwa busara zao kunaweza kuleta matokeo sio mazuri wakiamua kukataa.




Happy new year 2018!!
 
Hakuna mwanume wa kusimama kupambana na serkali ww mtoto ni hatari

Upo wapi ukuta.
Operations za kijinga sijui M4C ,sangali na nk

Nawaonea huruma sana wapinzani
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom