Dr. Wansegamila
JF-Expert Member
- Feb 3, 2012
- 2,857
- 7,846
Na Thadei Ole Mushi.
Wakati Wananchi wa nyanda za Juu Kusini wakiozesha mahindi, Mwenezi wetu yupo Pale Lumumba anaandaa kipindi cha Kwenda kufundisha kuhusu Itikadi.
Wakati Zabibu zikiozea Shambani kule Dodoma, katibu wetu yupo Ofisini na Mtolea wanapanga namna ya kutumia Fedha za Mlalahoi kwenye Chaguzi ambazo hazina maana kabisa kwa wananchi hivi ndivyo anavyobana matumizi ya Serikali.
Wakati Vijana wakihangaika asubuhi na jioni Kutafuta Ajira watu wanasaini Posho za Kufundishana Itikadi za Chama kila kukicha.
Nataka kusema nini?
CCM tunabahati ya kubadisha safu za Uongozi lakini hatubadilishi namna ya kufikiria.
Binafsi sioni mantiki au Impact ya Madarasa ya Itikadi na mabonanza yanayoendeshwa na idara ya Uenezi wa Chama.
Sioni Mantiki au impact ya Sera yetu ya hamia kwetu na Gombea tena.
Kiutafiti tunasema hakuna uhusiano wowote kati ya matatizo ya wananchi na mambo yanayofanywa na viongozi wa chama. Ccm inaishi sayari nyingine na Wananchi wapo sayari nyingine.
Muda huu tunaopoteza na mambo kama haya ni bora tungeutumia kudeal na matatizo ya wananchi yaani kuyasemea kwa sauti ili Serikali ichukue hatua.
CCM inapaswa kuwa mdomo wa wananchi, sauti ya wanyonge. CCM inapaswa kuwa kinara wa kukataa sheria Kandamizi kwa wananchi.
Ile CCM iliyokuwa na uwezo wa Kuisimamia Serikali ipo wapi? Kwa sasa Serikali yetu inasimamiwa na watu individual kama kina Fatma na Zitto.
Uwezo wa CCM umepotea moja kwa moja katika kusimamia mambo ya msingi na Maslahi ya Wananchi.Wamemezwa na Serikali kabisa, hawana ubavu wa kukemea.
Ole Mushi.
0712702602
Wakati Wananchi wa nyanda za Juu Kusini wakiozesha mahindi, Mwenezi wetu yupo Pale Lumumba anaandaa kipindi cha Kwenda kufundisha kuhusu Itikadi.
Wakati Zabibu zikiozea Shambani kule Dodoma, katibu wetu yupo Ofisini na Mtolea wanapanga namna ya kutumia Fedha za Mlalahoi kwenye Chaguzi ambazo hazina maana kabisa kwa wananchi hivi ndivyo anavyobana matumizi ya Serikali.
Wakati Vijana wakihangaika asubuhi na jioni Kutafuta Ajira watu wanasaini Posho za Kufundishana Itikadi za Chama kila kukicha.
Nataka kusema nini?
CCM tunabahati ya kubadisha safu za Uongozi lakini hatubadilishi namna ya kufikiria.
Binafsi sioni mantiki au Impact ya Madarasa ya Itikadi na mabonanza yanayoendeshwa na idara ya Uenezi wa Chama.
Sioni Mantiki au impact ya Sera yetu ya hamia kwetu na Gombea tena.
Kiutafiti tunasema hakuna uhusiano wowote kati ya matatizo ya wananchi na mambo yanayofanywa na viongozi wa chama. Ccm inaishi sayari nyingine na Wananchi wapo sayari nyingine.
Muda huu tunaopoteza na mambo kama haya ni bora tungeutumia kudeal na matatizo ya wananchi yaani kuyasemea kwa sauti ili Serikali ichukue hatua.
CCM inapaswa kuwa mdomo wa wananchi, sauti ya wanyonge. CCM inapaswa kuwa kinara wa kukataa sheria Kandamizi kwa wananchi.
Ile CCM iliyokuwa na uwezo wa Kuisimamia Serikali ipo wapi? Kwa sasa Serikali yetu inasimamiwa na watu individual kama kina Fatma na Zitto.
Uwezo wa CCM umepotea moja kwa moja katika kusimamia mambo ya msingi na Maslahi ya Wananchi.Wamemezwa na Serikali kabisa, hawana ubavu wa kukemea.
Ole Mushi.
0712702602