Naitafakari sana kauli nzito ya Celina Kombani "hujafa hujaumbika"

AMA wewe unazaliwa wapi? waziri asiye na wizara maalumu "minister without portfolio" mbona hiki ni kitu cha zamani sana tangu enzi mwalimu enzi hizo Hayati R.M. Kawawa aliwahi kuwa waziri asiye na wizara maalum, wakati wa mkapa Dr. Hasy Kitine pia aliwahi kuwa waziri asiye na wizara maalum. labda kama unasema hiki ni kitu cha kipekee kwa Tanzania, lakini sio eti hujawahi kuona. wewe umezaliwa lini. naona ama umri unakusumbua au wewe ni bongolala
 
Hii ni kauli ambayo aliitoa kwenye bunge la bajeti linaloendelea siku chache zilizopita.Wengi tuliichukulia kauli ile kuwa ni ya aina yake hasa kwa jinsi ilivyowasilishwa.Wapo baadhi waliyoipuuza na kuiacha ipite.

Hivi ni nini kilichojificha kwenye uwaziri wa Prof. Mark Mwandosya hadi tunaambiwa "hujafa hujaumbika?" Mwandosya ni waziri pekee asiye na wizara niliyewahi kusikia duniani! Ama kweli "hujafa hujaumbika"

Wakati mawaziri wengine wanapanga bajeti za kuwatumikia wananchi kwa kutumia kodi zetu, yeye Mwandosya anapanga bajeti ya kula, kunywa na kutembea kwa kutumia kodi zetu watanzania.Ndiyo, ana haki ya kupanga bajeti! Si ni waziri? Mimi najiuliza sana mpaka napata hasira! Ni kwa nini Kikwete alimteua waziri anayetumia kodi za watanzania kujipangia bajeti ya kutumia yeye mwenyewe?

Kweli Kikwete kwa hili nilijikuta nazidi kumtafakari ni rais wa aina yake! Kuna nini kati ya Kikwete na Mwandosya hadi tunaambiwa kuwa hujafa hujaumbika? Ni fadhila gani na kwa jambo lipi zinazolipwa? Kuna mambo kama watanzania tunayachukulia kawaida lakini yanatupatia taswira ya ajabu sana duniani!

Ina maana kwa kauli ya Celina Kombani Kikwete anamuumba Mwandosya kwa kumpa uwaziri, shangingi na bajeti huku kukiwa hamna analofanya kama waziri kwa ajili ya watanzania? Hizi ni kodi zetu na mimi ni miongoni mwa walipa kodi nina haki ya kulalamika! Tuangalie matatizo lukuki yanayotukabili huku kukiwa na mawaziri wasio na wizara wanaopangiwa bajeti na kupewa mashangingi, walinzi na hadhi zote kama waziri!

Ama kweli "hujafa hujaumbika" Mimi mlala hoi nani ataniumba?

Pumzika kwa amani baba wa taifa la Tanzania...uliyakemea haya kwa uzalendo wa hali ya juu!

Uzi wako haueleweki kwa mtiririko mbovu! Unadhani kila unachokickia ww kila mtu anakickia? Tuambie kwanza Celine Kombani ilikuwaje akasema hujafa hujaumbika? Alisema wapi na baada ya nini? Unatiririka tu bila kunfafanulia msomaji heading yako inamahusiano gani na kilichomo?
 
Tafadhali usipotoshe historia; Salim Ahmed Salim hajawahi kuwa naibu waziri mkuu bali waziri mkuu!!!

Alikuwa Naibu Waziri Mkuu chini ya Waziri Mkuu Joseph Warioba.
Na hapo hapo akawa Waziri wa Ulinzi (na Jeshi la Kujenga Taifa)...
 
AMA wewe unazaliwa wapi? waziri asiye na wizara maalumu "minister without portfolio" mbona hiki ni kitu cha zamani sana tangu enzi mwalimu enzi hizo Hayati R.M. Kawawa aliwahi kuwa waziri asiye na wizara maalum, wakati wa mkapa Dr. Hasy Kitine pia aliwahi kuwa waziri asiye na wizara maalum. labda kama unasema hiki ni kitu cha kipekee kwa Tanzania, lakini sio eti hujawahi kuona. wewe umezaliwa lini. naona ama umri unakusumbua au wewe ni bongolala

Watu wanakurupuka tu bila kufanya rejea hata moja! Hata historia hawana! Generally uwaziri nao hauna maana hawana tofauti na wakuu wa mikoa!
 
Rashid Kawawa pia amewahi kuwa waziri asiye na wizara maalum enzi za Mwinyi.
 
AMA wewe unazaliwa wapi? waziri asiye na wizara maalumu "minister without portfolio" mbona hiki ni kitu cha zamani sana tangu enzi mwalimu enzi hizo Hayati R.M. Kawawa aliwahi kuwa waziri asiye na wizara maalum, wakati wa mkapa Dr. Hasy Kitine pia aliwahi kuwa waziri asiye na wizara maalum. labda kama unasema hiki ni kitu cha kipekee kwa Tanzania, lakini sio eti hujawahi kuona. wewe umezaliwa lini. naona ama umri unakusumbua au wewe ni bongolala

At least hao hawakuwa wagonjwa ................ HUJAFA HUJAUMBIKA! The bottom line is two wrongs do not make right! Serikali za awamu hizo hazikushindwa kutoa OC kwenye Idara na Taasisi zake. Lakini awamu hii haiwezi kutoa OC kwenye Idara na Taasisi zake, halafu eti katika mazuri yote yaliyofanywa na awamu zilizopita, awamu hii IMEONA ZURI MOJA TU LA KUTEUA MAWAZIRI WASIO NA WIZARA MAALUMU! But to add salt to the wound, yenyewe imekwenda mbali zaidi, kwa kuteuwa WAGONJWA kuwa mawaziri wasio kuwa na wizara maalumu. haya ndiyo mambo yanayotetewa na SPIN DR(?) wa awamu hii!!
 
At least hao hawakuwa wagonjwa ................ HUJAFA HUJAUMBIKA! The bottom line is two wrongs do not make right! Serikali za awamu hizo hazikushindwa kutoa OC kwenye Idara na Taasisi zake. Lakini awamu hii haiwezi kutoa OC kwenye Idara na Taasisi zake, halafu eti katika mazuri yote yaliyofanywa na awamu zilizopita, awamu hii IMEONA ZURI MOJA TU LA KUTEUA MAWAZIRI WASIO NA WIZARA MAALUMU! But to add salt to the wound, yenyewe imekwenda mbali zaidi, kwa kuteuwa WAGONJWA kuwa mawaziri wasio kuwa na wizara maalumu. haya ndiyo mambo yanayotetewa na SPIN DR(?) wa awamu hii!!


Kama ugonjwa ndio unadhani ndio disqualification ya mtu kuwa waziri basi wabunge wengi ni wagonjwa ambao hawastahili kuteuliwa!!! Angalia tu jinsi bajeti yao ya wabunge wanaoongozana kwenda India; na hiyo ni siri yao wasioyoitaka ijadiliwe hadharani!!! Hakuna hata memba mmoja wa cabinet ambaye sio mgonjwa!!!! Huyo Celina Kombani mwenyewe ana maradhi yasiyotibika.
 
Kama ugonjwa ndio unadhani ndio disqualification ya mtu kuwa waziri basi wabunge wengi ni wagonjwa ambao hawastahili kuteuliwa!!! Angalia tu jinsi bajeti yao ya wabunge wanaoongozana kwenda India; na hiyo ni siri yao wasioyoitaka ijadiliwe hadharani!!! Hakuna hata memba mmoja wa cabinet ambaye sio mgonjwa!!!! Huyo Celina Kombani mwenyewe ana maradhi yasiyotibika.
The look of her lips confirm your assertion.
 
Mimi binfsi ninakushangaa wewe kwa KUZISHANGAA kauli za CCM! Kuna mwingine mnamuita Spika aliwahi kusema hivi Kama yeye angekuwa na uwezo wa Kimungu basi angemchagua Mtanzania mwingine afe badala ya Dr. Mgimwa (former Minster of finance). Wakati hii serikali ya awamu ya nne ikishindwa kabisa kutoa OC kwa idara na Taasisi zake (ziko hoi bin taabani haziwezi hata kulipa utilities bills). Bado Rais anamteua mtu kuwa waziri asiye na wizara maalumu kwasababu eti HUJA HUJAUMBIKA! This can only be found in Tanzania. Kama huyu Rais ana huruma kiasi basi awateue wagonjwa wote waliopo mahospitalini kuwa mawaziri wasio kuwa na wizara maalumu, maana hawajafa, hawajaumbika!

Aisee, hiyo sijawahi kuisikia, bila shaka alitamka wakati wa mazishi kujipa promo kwa ndugu na jamaa ya marehemu wamwone ana mapenzi makuu na marehemu huyo mnafiki mkubwa. Amchague mtanzania yupi? Mbona hata sisi watanzania kama Mungu angekuwa anachukua kura tungewalisti na Mungu angeshawaondoa kitambo! Akiwepo yeye spika, si basi tu Mungu hajatoa hiyo chance, tena Mungu alivyo wa ajabu kiumbe ambaye hatakiwi ndiye anayeachwa muda mrefu, bila shaka ili atubu, huku wenyewe hawawezi hata kufikiria kutubu
 
Mbona kunachama kinachoitwa ukawa na hakina usajilli lakini husemi
 
Tanzania kwa vipindi mbalimbali imekuwa na mawaziri wasio na wizara maalum. Miongoni mwao ni marehemu Kawawa.

Pia nchi nyingine nyingi zina mawaziri wasio na wizara maalum. Miongoni mwa hizo nchi ni Uingereza ambayo kwa vipindi mbalimbali imekuwa na mawaziri kama hao. Serikali ya sasa ina mzee Ken Clarke.

Lengo hasa la hii nafasi ni kuwapa wale watu ambao uzoefu wao unaweza kulisaidia baraza la mawaziri kufanya maamuzi ya maana, lakini wakati huo huo, wahusika wanaweza kuwa ni wazee au wanaumwa na hivyo hawawezi kuwa kwenye hekaheka za kila siku za kuongoza wizara kamili.

Kwa case ya prof. Mwandosya ni kwamba anaumwa. Kikawaida ungetegemea JK asimweke tena kwenye baraza la mawaziri. Lakini huenda kaona bado wanahitaji busara zake lakini pia hawawezi kumpa wizara kamili kwasababu bado hajapona.
Hii ni kauli ambayo aliitoa kwenye bunge la bajeti linaloendelea siku chache zilizopita.Wengi tuliichukulia kauli ile kuwa ni ya aina yake hasa kwa jinsi ilivyowasilishwa.Wapo baadhi waliyoipuuza na kuiacha ipite.

Hivi ni nini kilichojificha kwenye uwaziri wa Prof. Mark Mwandosya hadi tunaambiwa "hujafa hujaumbika?" Mwandosya ni waziri pekee asiye na wizara niliyewahi kusikia duniani! Ama kweli "hujafa hujaumbika"

Wakati mawaziri wengine wanapanga bajeti za kuwatumikia wananchi kwa kutumia kodi zetu, yeye Mwandosya anapanga bajeti ya kula, kunywa na kutembea kwa kutumia kodi zetu watanzania.Ndiyo, ana haki ya kupanga bajeti! Si ni waziri? Mimi najiuliza sana mpaka napata hasira! Ni kwa nini Kikwete alimteua waziri anayetumia kodi za watanzania kujipangia bajeti ya kutumia yeye mwenyewe?

Kweli Kikwete kwa hili nilijikuta nazidi kumtafakari ni rais wa aina yake! Kuna nini kati ya Kikwete na Mwandosya hadi tunaambiwa kuwa hujafa hujaumbika? Ni fadhila gani na kwa jambo lipi zinazolipwa? Kuna mambo kama watanzania tunayachukulia kawaida lakini yanatupatia taswira ya ajabu sana duniani!

Ina maana kwa kauli ya Celina Kombani Kikwete anamuumba Mwandosya kwa kumpa uwaziri, shangingi na bajeti huku kukiwa hamna analofanya kama waziri kwa ajili ya watanzania? Hizi ni kodi zetu na mimi ni miongoni mwa walipa kodi nina haki ya kulalamika! Tuangalie matatizo lukuki yanayotukabili huku kukiwa na mawaziri wasio na wizara wanaopangiwa bajeti na kupewa mashangingi, walinzi na hadhi zote kama waziri!

Ama kweli "hujafa hujaumbika" Mimi mlala hoi nani ataniumba?

Pumzika kwa amani baba wa taifa la Tanzania...uliyakemea haya kwa uzalendo wa hali ya juu!
 
Tanzania kwa vipindi mbalimbali imekuwa na mawaziri wasio na wizara maalum. Miongoni mwao ni marehemu Kawawa.

Pia nchi nyingine nyingi zina mawaziri wasio na wizara maalum. Miongoni mwa hizo nchi ni Uingereza ambayo kwa vipindi mbalimbali imekuwa na mawaziri kama hao. Serikali ya sasa ina mzee Ken Clarke.

Lengo hasa la hii nafasi ni kuwapa wale watu ambao uzoefu wao unaweza kulisaidia baraza la mawaziri kufanya maamuzi ya maana, lakini wakati huo huo, wahusika wanaweza kuwa ni wazee au wanaumwa na hivyo hawawezi kuwa kwenye hekaheka za kila siku za kuongoza wizara kamili.

Kwa case ya prof. Mwandosya ni kwamba anaumwa. Kikawaida ungetegemea JK asimweke tena kwenye baraza la mawaziri. Lakini huenda kaona bado wanahitaji busara zake lakini pia hawawezi kumpa wizara kamili kwasababu bado hajapona.

Asante kwa ufafanuzi. Yaani vijana wa JF wengi vichwa maji. Hii inaonesha jinsi taifa lilivyokosa vijana wenye weledi wa kuchambua mambo kabla ya kutoa comments. JK amekuwa rais bora mwenye huruma sana na mchapa kazi.
 
Kama ugonjwa ndio unadhani ndio disqualification ya mtu kuwa waziri basi wabunge wengi ni wagonjwa ambao hawastahili kuteuliwa!!! Angalia tu jinsi bajeti yao ya wabunge wanaoongozana kwenda India; na hiyo ni siri yao wasioyoitaka ijadiliwe hadharani!!! Hakuna hata memba mmoja wa cabinet ambaye sio mgonjwa!!!! Huyo Celina Kombani mwenyewe ana maradhi yasiyotibika.

Kuna vitu viwili hapa unachanganya. Kuwa mgonjwa na ukawa capable kufanya kazi (kutumiza majukuma yako). Pili kuwa mgonjwa na ukawa incapable kutimiza majukumu yako. Sheria za utumishi wa umma ziko wazi kabisa, mtumishi yeyote yule ambaye ni mgonjwa na hawezi kutimiza majukumu yake, mwajiri anapaswa kumuachisha kazi na kumlipa sitahiki zake zote. Hakuna mahala ambapo kunamtaka mwajiri ampangie kazi zisizokuwa maalamu mfanyakazi anayeumwa aliyeshindwa kutimiza majukumu yake. (Ref Waziri asiyekuwa na wizara maalumu).
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom