Naishauri Serikali ya Tanzania, watu wasiruhusiwe kuingia wala kutoka Dar, Arusha na Mwanza

Solution ni watu wapimwe kwa gharama za serikali... Wa roll-out mass-testing mitaani hasa hizo sehemu mnazohisi maambukizi ni makubwa...
Wanaoonesha dalili ndo wapelekwe karantini...
Ukiwafungia watu ndani bila kujua nani ana hali gani sioni kama utakuwa umesaidia chochote...!
Unakumbuka yaliyotokea India?? Wahindi walilazimima kutembea kwa miguu kutoka mijini kukimbilia vijijini...
Mkilazimisha lockdowns hapa kwetu mtakuwa mmewakimbiza watu wengi sana kurudi vijijini katika hali isiyo ya kibinadamu kabisa!!

Mkuu kumbuka tunayo maabara moja tu yenye uwezo wa kufanya huu upimaji. Aliyekwisha pimwa anaweza ambukizwa dakika au sekunde chache baada ya kupimwa. Kwa maana ya kuwa validity ya matokeo ya kupimwa a few seconds baada ya kupimwa may be absolutely null and void.

Unaonaje hili, kwani linafanikiwa katika maeneo mengine kama yetu? Typical case ni Rwanda, nchi maskini na yenye raslimali duni kuliko sisi:

Huko Rwanda, uwezo tofauti wa kiuchumi wa wanajamii umezingatiwa katika kipindi chote cha lockdown (wako siku takribani ya 20 zinabakua 9):

1. Wanaohitaji msaada kabisa (in totality) wametambuliwa na wanasaidiwa.
2. Wanaohitaji msaada kiasi (partial) wametambuliwa na wanasaidiwa.
3. Wanaojitosheleza wametambuliwa.
4. Wenye ziada na nia kiasi cha kuweza kusaidia wengine wametambuliwa na wanakaribishwa kufanya hivyo.

Kama mfano Azam Rwanda imechangia tani 20 za chakula (juzi) kuunga mkono juhudi kule. Mifano iko mingi.

Lengo ni kuona watu wanasalia majumbani na waathirika wote wanatambulika kwa hatua stahiki. Ndiyo maana wao hadi sasa hata vifo vya Corona hamna. Wanaanza matunzo (care) mapema. Kasi ya maambukizi tayari wameidhibiti vilivyo.

Katika mazingira kama haya mkuu ningeshukuru kufahamu kwa nini bado tunadhani lockdown itakuwa na madhara.

Ni kweli kuwa hatutakula ambacho tungependa kula kwa kipindi hicho. Ila ni wazi kuwa tunaweza kujipanga asife mtu kwa njaa. Tukamaliza salama na ugonjwa ukadhibitiwa.

Mawazo yako mkuu yatakuwa ya msingi mno katika kuchangia kuona uelekeo upi ni bora kabisa hata kama wewe na mimi hatuna influence yoyote.

Au siyo mkuu?
 
  • Thanks
Reactions: VSM
Kwaanaetaka kujifungia ndani ajifungie tu, sisi wengine inabid tutoke ili tuishi

Sent using Jamii Forums mobile app

Ila hoja huna. Sawa tumekusikia.

Ila ungekuwa na hoja ingependeza zaidi ili angalau kama binadamu tukajua upo na mbadala gani. Hudhani hivyo mkuu?

Kuwa umehakikishiwa kuwa hutaathirika kwa njaa (wala kwa lolote maana lockdown haina maana ya kufungiwa chumbani) ila bado hutaki tu?

Ha haa ha, si hata ng'ombe yuko hivyo hivyo mkuu?
 
  • Thanks
Reactions: VSM
Huu ugonjwa unaweza kuzuilika kabisa. serikali kupitia jeshi wangetengeneza sanitizer gel yakutosha ambayo ingewekwa kwenye vifunganshio mbalimbali vya ujazo mdogo kuanzia ml 50 ambavyo vingeuzwa kwabei elekezi ambayo raia yoyote angeweza kuimudu.
Ndani ya wiki moja kuhakikisha kila mahali iwe imefika naiwe nilazima kwakila mtu atakae kua nje au barabarani nilazima awe nahio sanitizer gel.
Jeshi litumike kuhakikisha hizo sanitizer gel zinapatikana kila mahali kwa bei elekezi. litumike kuhakikisha kila atakae tumia usafir wa uma, machinga, bajaji, napikipik nabiashara yoyote bila kujali ukubwa wake nilazima awe nasanitizer gel.
Ifanyike promo kubwa kutumia wasanii watu maarufu na vyombo vyahabar nchi nzima kua nilazima uwe nahizo sanitizer gel namatumiz yake ilikuzuia maambukiz mapya

Sent using Jamii Forums mobile app
Eti jeshi khaaaa
 
Wazo zuri sana watu wasiruhusiwe kutoka nje ya mkoa, mabasi yazuiliwe yabaki magari ya mizigo tu. Watu watulie wanapoishi. Kwanza safari nyingi za wabongo ni kuhani misiba, kwenda kusalimia na wafanya biashara kufuata bidhaa. Hili la wafanyabiashara kufuata mzigo lifanyike kwa njia ya simu au mitandao hizo bidhaa zao zitaletwa na magari ya mizigo baada ya kulipa pesa kupitia mobile money au bank.
 
Mkuu kumbuka tunayo maabara moja tu yenye uwezo wa kufanya huu upimaji. Aliyekwisha pimwa anaweza ambukizwa dakika au sekunde chache baada ya kupimwa. Kwa maana ya kuwa validity ya matokeo ya kupimwa a few seconds baada ya kupimwa may be absolutely null and void.

Unaonaje hili, kwani linafanikiwa katika maeneo mengine kama yetu? Typical case ni Rwanda, nchi maskini na yenye raslimali duni kuliko sisi:

Huko Rwanda, uwezo tofauti wa kiuchumi wa wanajamii umezingatiwa katika kipindi chote cha lockdown (wako siku takribani ya 20 zinabakua 9):

1. Wanaohitaji msaada kabisa (in totality) wametambuliwa na wanasaidiwa.
2. Wanaohitaji msaada kiasi (partial) wametambuliwa na wanasaidiwa.
3. Wanaojitosheleza wametambuliwa.
4. Wenye ziada na nia kiasi cha kuweza kusaidia wengine wametambuliwa na wanakaribishwa kufanya hivyo.

Kama mfano Azam Rwanda imechangia tani 20 za chakula (juzi) kuunga mkono juhudi kule. Mifano iko mingi.

Lengo ni kuona watu wanasalia majumbani na waathirika wote wanatambulika kwa hatua stahiki. Ndiyo maana wao hadi sasa hata vifo vya Corona hamna. Wanaanza matunzo (care) mapema. Kasi ya maambukizi tayari wameidhibiti vilivyo.

Katika mazingira kama haya mkuu ningeshukuru kufahamu kwa nini bado tunadhani lockdown itakuwa na madhara.

Ni kweli kuwa hatutakula ambacho tungependa kula kwa kipindi hicho. Ila ni wazi kuwa tunaweza kujipanga asife mtu kwa njaa. Tukamaliza salama na ugonjwa ukadhibitiwa.

Mawazo yako mkuu yatakuwa ya msingi mno katika kuchangia kuona uelekeo upi ni bora kabisa hata kama wewe na mimi hatuna influence yoyote.

Au siyo mkuu?

Nakuelewa sana... Na haya yote tulishauri mpema sana... Uwezekano wa stimulus package ni suala nilianza kulipigia kelele toka kitambo...
Kuwafungia Watanzania kwa kuiga wazungu wanavofanya kutatuponza zaidi ya inavyowaponza...
Je serikali yetu ipo tayari kufanya walahu nusu ya hizo strategies ni swali kubwa sana...
 
Nakuelewa sana... Na haya yote tulishauri mpema sana... Uwezekano wa stimulus package ni suala nilianza kulipigia kelele toka kitambo...
Kuwafungia Watanzania kwa kuiga wazungu wanavofanya kutatuponza zaidi ya inavyowaponza...
Je serikali yetu ipo tayari kufanya walahu nusu ya hizo strategies ni swali kubwa sana...

Mkuu one thing at a time.

Kwingine watu wameelimishwa sana. Wanaelewa lockdown si fursa ya yeyote kujipatia lolote au kujinufaisha. Tunawajibika kuwa na mtizamo huo kwanza.

Kila mtu anajijua mwenyewe na anawajibika kujiweka wazi pasipo na kutia chumvi ili kuweza kuifanikisha hili.

Heri tukapita lockdown salama hata kwa kushindia uji at times kuliko ku perish na Corona.

Unaonaje hiyo approach kwanza. Ni wazi kuwa serikali itakuwa na sehemu yake.
 
Mkuu one thing at a time.

Kwingine watu wameelimishwa sana. Wanaelewa lockdown si fursa ya yeyote kujipatia lolote au kujinufaisha. Tunawajibika kuwa na mtizamo huo kwanza.

Kila mtu anajijua mwenyewe na anawajibika kujiweka wazi pasipo na kutia chimbo ili kuweza kuifanikisha hili.

Heri tukapita lockdown salama hata kwa kushindia uji at times kuliko ku perish na Corona.

Unaonaje hiyo approach kwanza. Ni wazi kuwa serikali itakuwa na sehemu yake.

Wasiwasi wangu ni kwenye utekelezaji na ufanisi wa hiyo lockdown model yako...
Kwa sasa hatuna watu serikalini wala kwenye vyombo vya dola wanaoweza kutekeleza lockdown isiyoumiza...
Mimi ni nani nizuie matakwa yenu??
Fanyeni tu lockdown nitakuwepo baadaye kutoa maoni yangu...
 
Wasiwasi wangu ni kwenye utekelezaji na ufanisi wa hiyo lockdown model yako...
Hatuna watu serikalini na kwenye vyombo vya dola wanaoweza kutekeleza lockdown isiyoumiza...
Mimi ni nani nizuie matakwa yenu??
Fanyeni tu lockdown nitakuwepo baadaye kutoa maoni yangu...

Mkuu hii siyo model yangu. Inafanyika hivyo kwenye nchi kama yetu. Rwanda wanafanya hivyo. Tunaweza kujifunza kwao.

Tuko katika vita. Vita inahitaji umoja. Ni kwa umoja wetu nduli Amin alilazimika kutimua mbiyo.

Hata huyu kirusi mchango wako hata wa mawazo tu utasaidia sana katika kumsambaratisha.

Tusikate tamaa mkuu.
 
Back
Top Bottom