Nairobi: Bodigadi wa Spika wa Bunge la Meru auawa

Zurie

JF-Expert Member
Jul 6, 2014
1,743
4,272
Mlinzi wa Spika wa bunge la kaunti ya Meru Joseph Kaberia ameuawa jijini Nairobi.

Duru za polisi zisema mlinzi huyo alipigwa risasi Jumapili, Julai 21, katika eneo la Kamiti Corner.

Kulingana na polisi, mlinzi huyo alikuwa pamoja na dereva wa Spika wakati ambapo kisa hicho kilitokea.

Tayari, derevea huyo amekamatwa ili kusaidia maafisa wa polisi na uchunguzi zaidi kuhusiana na kisa hicho huku polisi wakishuku pia huenda alihusika kwa njia fulani.

Kulingana na polisi, wawili hao walipatikana katika eneo la mkasa baada ya wakazi kuwaita polisi waliposkia milio ya risasi mida ya saa tisa usiku.

Mkuu wa polisi jijini Nairobi Philip Ndolo alisema wawili hao walikuwa wamejihami kwa bunduki huku dereva akiwa ametumia risasi 20 za bastola yake naye mlinzi hakuwa ametumia hata risasi moja.

Ndolo alisema baada ya polisi kufika katika eneo la mkasa, waliwapata wawili hao huku mlinzi akiwa amepigwa risasi kifuani na dereva kwenye mguu wake.
“Walikimbizwa hospitalini na mlinzi huyo kufariki akipokea matibabu,” Ndolo alisema.
Baadhi ya majirani walisema waliamshwa na mabishano kati ya wawili hao kabla ya kuskia milio ya risasi.

Ndolo alisema uchunguzi zaidi utafanyiwa bunduki ya dereva huyo ili kubaini iwapo ndio ilitumika kummaliza mwendazake.

Spika hakuwa na wawili hao wakati wa kisa hicho.

=========

A bodyguard attached to Meru County Assembly speaker Joseph Kaberia was Sunday morning shot dead at Kamiti Corner area in Nairobi.

The officer; Constable Samuel Munga, is believed to have been killed by the speaker’s driver, Andrew Nabea following an alleged argument.

The speaker, who was not present during the 3am shootout, confirmed the incident saying: “…We lost our dedicated security officer. My driver Andrew Mwithalii got injured but is admitted at the hospital.”

“Relevant national security organs have taken charge and have commenced investigations,” said Kaberia in a statement.

Reports indicate that the driver was dropping off the bodyguard at his sister’s house at Kamiti Corner when a scuffle ensued between them outside the gate.

Police sources indicate that neighbours reported hearing the two arguing before gun shots rent the air.

The driver sustained a gunshot wound and is admitted at the Ruaraka Neema Hospital in Kasarani area, where the bodyguard, who had been shot several times in the chest, was confirmed dead.

Police sources indicate that a total of 17 spent cartridges were recovered at the scene.

Preliminary investigations, however, indicate that all the fired bullets came from the driver’s gun as the bodyguard’s firearm had all 15 rounds of ammunition intact.

Source: Citizen
 
Back
Top Bottom