Idugunde
JF-Expert Member
- May 21, 2020
- 6,273
- 6,637
Kama ilivyo kwa treni kichwa kikipoteza uelekeo basi mabehewa yote yanakuwa yamepoteza uelekeo.
Ndivyo ilivyosasa ile hali ya taifa kutengemaa kidogo sasa inakwenda kupotea kabisa. Nidhamu kwa watumishi wa umma, nidhamu ya wananchi kutii sheria inakwenda kupotea. Ufisadi nao utarudi kwa kasi mithiri ya baruti imeripuka.
Jiulize kama jeshi la Polisi ni lilelile na makamanda ni walewale kwa nini wizi na mauaji yamerudi kwa kasi? Dar es salaam ni pa kutilia mfano tu lakini hata mikoani waharifu wanajiachia. Pitia vyombo vya habari utapata majibu.
Mbaya zaidi mkuu wa vyombo vya usalama analalama kuwa anasoma mitandao ya kijamii juu ya kuongezeka uhalifu.
Kwa ufupi kama taifa hatuna jinsi lakini tukubali kuwa sasa hatuna muelekeo thabiti.
Ndivyo ilivyosasa ile hali ya taifa kutengemaa kidogo sasa inakwenda kupotea kabisa. Nidhamu kwa watumishi wa umma, nidhamu ya wananchi kutii sheria inakwenda kupotea. Ufisadi nao utarudi kwa kasi mithiri ya baruti imeripuka.
Jiulize kama jeshi la Polisi ni lilelile na makamanda ni walewale kwa nini wizi na mauaji yamerudi kwa kasi? Dar es salaam ni pa kutilia mfano tu lakini hata mikoani waharifu wanajiachia. Pitia vyombo vya habari utapata majibu.
Mbaya zaidi mkuu wa vyombo vya usalama analalama kuwa anasoma mitandao ya kijamii juu ya kuongezeka uhalifu.
Kwa ufupi kama taifa hatuna jinsi lakini tukubali kuwa sasa hatuna muelekeo thabiti.