Naiona kasoro ya maandamano ya CHADEMA

Tulimumu

JF-Expert Member
Mar 11, 2013
14,304
12,965
CHADEMA imeitisha maandamano nchi nzima kupinga bunge la katiba kuendelea huku ikijulikana wazi kuwa katiba mpya haitapatikana. CHADEMA ni mojawapo ya vyama vinavyo unda umoja wa katiba mpya - UKAWA. Mimi naona kwa CHADEMA kuitisha maandamano peke yake ni kama kujitenga na vyama vingine vinavyounda UKAWA na hivyo kudhoofisha nguvu ya pamoja. Ingekuwa ni vizuri CHADEMA ikashirikiana na vyama vyenza vinavyounda umoja wa katiba ya wananchi - UKAWA. Kwa CHADEMA kutoka chenyewe ni kudhoofisha nguvu ya pamoja unless waseme kuwa wenzao wamekataa. Wakumbuke kuwa umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu. Ilitakiwa wafanye kwa pamoja na wenzao kama walivyotoka bungeni na viongozi wakuu wa vyama hivyo ndio wangeongoza maandamano hayo ingeleta impact kubwa kuliko hivi CDM walivyoamua kutoka kivyao vyao. Hii ni kama kusema CUF, NCCR, DP na wengineo watoke kivyao, sasa nini maana ya UKAWA??!!. Hiyo itakuwa sawa na kujenga mnara wa baberi
 
Maandamano ya CHADEMA ni batili
 

Attachments

  • image.jpg
    image.jpg
    598.6 KB · Views: 148
  • image.jpg
    image.jpg
    687.5 KB · Views: 139
  • image.jpg
    image.jpg
    573.5 KB · Views: 132
  • image.jpg
    image.jpg
    543.7 KB · Views: 126
Bunge limeahirishwa mpaka Jumatano tarehe 24 Septemba 2014 saa tatu asubuhi ambapo Rasimu ya Tatu itawasilishwa. Niwashukuru wale wote tuliokuwa pamoja kwa updates. Hadi siku hiyo, pamoja sana
 
Bunge limeahirishwa mpaka Jumatano tarehe 24 Septemba 2014 saa tatu asubuhi ambapo Rasimu ya Tatu itawasilishwa. Niwashukuru wale wote tuliokuwa pamoja kwa updates. Hadi siku hiyo, pamoja sana

Naona unaangaika sana leo. Mara maandamano, mara ratiba ya mwenyekiti, mara mbowe, mara chadema!! Bunge linalobadili kanuni ili kukidhi matakwa ya kutunga katiba ya chama sidhani kama ni sahihi. Japo hapo ulipo ni kama kipofu wa akili (ufahamu) baadae sana utakuja gundua kuwa haukuwa sahihi. Maana wengi wetu nao tuliwa kama wewe na baada ya kutafakari kwa kina tukaja gundua kuwa ni usaliti dhidi ya wananchi wengine!!
 
Kama Kweli umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu, kwa Hakika hata UKAWA isingeanzishwa maana msingi wake Ni wale CCM sisi UKAWA!
Mwalimu alisema dhambi ya Ubaguzi mbaya sana na inatabia ya kuendelea kuhukumu!

Jana CUF wakaja na la Kwao bila wenzao yaani ni mvurugano mbele kwa mbele!
 
wamekurupushana
Kama Kweli umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu, kwa Hakika hata UKAWA isingeanzishwa maana msingi wake Ni wale CCM sisi UKAWA!
Mwalimu alisema dhambi ya Ubaguzi mbaya sana na inatabia ya kuendelea kuhukumu!

Jana CUF wakaja na la Kwao bila wenzao yaani ni mvurugano mbele kwa mbele!
 
CHADEMA INA KADA,SASA HIZO NI VURUGU TU ZA KANDA,CHADEMA INAKOMAZA KANDA ZAKE,NA HII NDIO FAIDA YA CHADEMA NI MSINGI NA KANDA.Hongereni mko vizuri cdm
 
CHADEMA imeitisha maandamano nchi nzima kupinga bunge la katiba kuendelea huku ikijulikana wazi kuwa katiba mpya haitapatikana. CHADEMA ni mojawapo ya vyama vinavyo unda umoja wa katiba mpya - UKAWA. Mimi naona kwa CHADEMA kuitisha maandamano peke yake ni kama kujitenga na vyama vingine vinavyounda UKAWA na hivyo kudhoofisha nguvu ya pamoja. Ingekuwa ni vizuri CHADEMA ikashirikiana na vyama vyenza vinavyounda umoja wa katiba ya wananchi - UKAWA. Kwa CHADEMA kutoka chenyewe ni kudhoofisha nguvu ya pamoja unless waseme kuwa wenzao wamekataa. Wakumbuke kuwa umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu. Ilitakiwa wafanye kwa pamoja na wenzao kama walivyotoka bungeni na viongozi wakuu wa vyama hivyo ndio wangeongoza maandamano hayo ingeleta impact kubwa kuliko hivi CDM walivyoamua kutoka kivyao vyao. Hii ni kama kusema CUF, NCCR, DP na wengineo watoke kivyao, sasa nini maana ya UKAWA??!!. Hiyo itakuwa sawa na kujenga mnara wa baberi


Kisheria UKAWA hawawezi kuitisha maandamano sababu sio chama cha Siasa kilichosajiliwa! na kwa mujibu wa sheria za Polisi vyama vya upinzani haviruhusiwi kufanya maandamamano kwa mkupuo kwa sababu za kiulinzi! hivyo inabidi maandamano yafanyike kwa kupokezana!
 
Back
Top Bottom