Alex Xavery
JF-Expert Member
- Apr 19, 2015
- 230
- 196
Mimi ni muumini wa CHADEMA, nina ndugu, jamaa na marafiki wengi sana wa ccm.
Ombi langu, tumieni mamlaka mliyonayo hata kwa wingi wa wabunge mlionao mfute siasa za vyama vingi Tanzania, uhai ni bora kuliko utamu wa madaraka tunaougombea, rasilimali watu ni nyenzo mojawapo ya ustawi wa taifa lolote ikiwa patakuwa na umoja, upendo na mshikamano baina yao wote kama ambavyo mh. raisi wa awamu ya tano alivyowahi kutolea mfano taifa la China.
Kama mnaona pana utamu sana hapo kwenye madaraka na mngependa ccm itawale milele mnayo mamlaka ya kukibakisha chama kimoja ccm mpaka Yesu atakaporudi na mle na kunywa miguu juu ya meza bila mapambano, hira, chuki, fitna, ufilauni na vita katika hichi kinachoitwa siasa za vyama vingi.
Ikiwa si hiari yenu na mnalazimishwa na kubanwa mbavu na wenye utimamu wa akili mtekeleze siasa za vyama vingi basi ni vyema muwe tiyari kukipa chombo huru mamlaka ya kusimamia maamzi ya wananchi bila kuingiliwa na utashi wa wanaogombea, kura zipigwe waziwazi ikiwezekana nje kweupe na zihesabiwe wazi wazi nje kweupe na kwa sauti, na baada ya matokeo waumini tupeane mikono na kupongezana kwa furaha bila kuonyeshana chuki hata chembe kisha turudi kufanya kazi kwa pamoja tukicheka na kufurahia mchuano ulivyokua, na huu ndio ustawi wa demokrasia, uchumi wa taifa na watu wake.
Lakini hali ya kisiasa ikiachwa iendelee hivi ilivyo basi ni hatari kwa taifa hili na watu wake, imani za watu katika vyama haziwezi komeshwa kwa kuwajeruhi na kuwaua waumini, ni vyema sasa serikali ya chama cha mapinduzi mfanye maamzi ya busara kuifanya Tanzania kuendelea kuwa kisiwa cha amani duniani, chagua kuitekeleza demokrasia ya vyama vingi bila uhuni na ufilauni au kuifuta demokrasia ya vyama vingi, haya yote mawili yapo ndani ya uwezo wenu.
Ikiwa mna hofu ya Mungu ndani yenu basi mtaguswa kuyapenda maisha ya watu wa taifa hili kuliko ulafi wa madaraka. Kila mtu atakufa na hatoondoka wala kuzikwa na chochote anachokipigania kwa sasa juu ya uso wa dunia lakini kila mmoja atajibu kivyake mbele ya hukumu.
Narudia tena, mimi ni muumini wa CHADEMA lakini nina ndugu, jamaa na marafiki wengi ccm, nilitarajia tutachuana kwa uwazi na kupeana mikono baada ya matokeo ya wazi na huru kama ilivyotokea ndani ya jimbo letu la Bukoba mjini 2014-2015 lakini kwa kilichotokea uchaguzi wa marudio mpaka watu kupigana mapanga na wengine kuua kabisa ambavyo ni matokeo ya maagizo ya baadhi ya wanasiasa wenyewe majukwaani si dalili nzuri kwa taifa letu.
Tunajengeana chuki baina yetu wenyew bila sababu za msingi na chuki ikikomaa matokeo yake ni mabaya sana.
Serikali ya chama cha mapinduzi chagueni moja na litekelezwe kwa ukamilifu kwa ajili ya uhai wa watanzania wote. Ni imani yangu mtatekeleza.
Asanteni sana.
Alex Xavery
Ombi langu, tumieni mamlaka mliyonayo hata kwa wingi wa wabunge mlionao mfute siasa za vyama vingi Tanzania, uhai ni bora kuliko utamu wa madaraka tunaougombea, rasilimali watu ni nyenzo mojawapo ya ustawi wa taifa lolote ikiwa patakuwa na umoja, upendo na mshikamano baina yao wote kama ambavyo mh. raisi wa awamu ya tano alivyowahi kutolea mfano taifa la China.
Kama mnaona pana utamu sana hapo kwenye madaraka na mngependa ccm itawale milele mnayo mamlaka ya kukibakisha chama kimoja ccm mpaka Yesu atakaporudi na mle na kunywa miguu juu ya meza bila mapambano, hira, chuki, fitna, ufilauni na vita katika hichi kinachoitwa siasa za vyama vingi.
Ikiwa si hiari yenu na mnalazimishwa na kubanwa mbavu na wenye utimamu wa akili mtekeleze siasa za vyama vingi basi ni vyema muwe tiyari kukipa chombo huru mamlaka ya kusimamia maamzi ya wananchi bila kuingiliwa na utashi wa wanaogombea, kura zipigwe waziwazi ikiwezekana nje kweupe na zihesabiwe wazi wazi nje kweupe na kwa sauti, na baada ya matokeo waumini tupeane mikono na kupongezana kwa furaha bila kuonyeshana chuki hata chembe kisha turudi kufanya kazi kwa pamoja tukicheka na kufurahia mchuano ulivyokua, na huu ndio ustawi wa demokrasia, uchumi wa taifa na watu wake.
Lakini hali ya kisiasa ikiachwa iendelee hivi ilivyo basi ni hatari kwa taifa hili na watu wake, imani za watu katika vyama haziwezi komeshwa kwa kuwajeruhi na kuwaua waumini, ni vyema sasa serikali ya chama cha mapinduzi mfanye maamzi ya busara kuifanya Tanzania kuendelea kuwa kisiwa cha amani duniani, chagua kuitekeleza demokrasia ya vyama vingi bila uhuni na ufilauni au kuifuta demokrasia ya vyama vingi, haya yote mawili yapo ndani ya uwezo wenu.
Ikiwa mna hofu ya Mungu ndani yenu basi mtaguswa kuyapenda maisha ya watu wa taifa hili kuliko ulafi wa madaraka. Kila mtu atakufa na hatoondoka wala kuzikwa na chochote anachokipigania kwa sasa juu ya uso wa dunia lakini kila mmoja atajibu kivyake mbele ya hukumu.
Narudia tena, mimi ni muumini wa CHADEMA lakini nina ndugu, jamaa na marafiki wengi ccm, nilitarajia tutachuana kwa uwazi na kupeana mikono baada ya matokeo ya wazi na huru kama ilivyotokea ndani ya jimbo letu la Bukoba mjini 2014-2015 lakini kwa kilichotokea uchaguzi wa marudio mpaka watu kupigana mapanga na wengine kuua kabisa ambavyo ni matokeo ya maagizo ya baadhi ya wanasiasa wenyewe majukwaani si dalili nzuri kwa taifa letu.
Tunajengeana chuki baina yetu wenyew bila sababu za msingi na chuki ikikomaa matokeo yake ni mabaya sana.
Serikali ya chama cha mapinduzi chagueni moja na litekelezwe kwa ukamilifu kwa ajili ya uhai wa watanzania wote. Ni imani yangu mtatekeleza.
Asanteni sana.
Alex Xavery