Naibu waziri wa Tamisemi Suleiman Jafo awataka wakuu wa wilaya kutoburuzwa na wakurugenzi

real G

JF-Expert Member
Feb 7, 2013
5,227
5,287
Naibu waziri wa nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa ( TAMISEMI) Suleman Jafo amewataka wakuu wa wilaya zote nchi kutoburuzwa na wakurugenzi pamoja na baadhi ya watendaji katika kusimamia fedha za miradi ya serikali huku akiwataka wakurugenzi wa Halmashauri kuacha ubinafsi na badala yake wawashirikishe wakuu wa wilaya katika mipango yote ya maendeleo.

upload_2017-6-14_14-36-21.jpeg
 
Waziri Jafo usilazimishe mambo ktk utendaji wa TAMISEMI ngazi ya wilaya na Mkoa.

Mfumo wetu ndani ya Serikali kuu na Serikali za mitaa unachangia hali hiyo.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hawajibiki kwa Mkuu wa wilaya au mkuu wa mkoa wa mkoa moja kwa moja.
 
Huko kwenye halmashauri nako ni kama huku kwenye makinikia tofauti ni kwamba huku kwenye makinikia ni mkapa na JK wakati kule kwenye halmashauri ni RC na DC
 
Hv Huyu Jamaa Anaelewa Job Discription Yao?Mkuu Wa Wilaya Anatakiwa Awe Wa Kujua Kusoma Na Kuandika While Mkurungez Anapaswa Kuwa Na Degree 2 Wapi Na Wapi?
 
Kwa Elimu yao ya darasa la 7 kuburuzwa ni lazima, awe mpole tu huyo Jafo wa kisarawe
 
HAWA WAKURUGENZI WANAOWABURUZA WENZAO SIO POA KABISA,HASA KAMA BARABARA ZINA LAMI WATAKUWA WANACHUBUKA SANA ASEE
 
Back
Top Bottom