Patriote
JF-Expert Member
- Jul 13, 2011
- 1,718
- 1,047
NAIBU Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo amewasihi wanafunzi wa elimu ya juu nchini kuandamana ili kushinikiza waliokopeshwa fedha za elimu miaka ya nyuma walipe ili wapewe wengine. Amesema wahitimu wengi walikopeshwa zaidi ya Sh21 bilioni ili kusoma kwenye vyuo mbalimbali, lakini baada ya kupata kazi wanakwepa kulipa mikopo hiyo. Mlugo alisema wanaosoma vyuoni sasa hawana budi kuandamana ili kuwashinikiza waliotangulia walipe fedha hizo ili ziweze kukopeshwa kwa wanafunzi wengine zaidi. "Fedha hizo zilikopeshwa kwa wanafunzi wa elimu ya juu tangu utoaji wa mikopo ulipoanza mwaka wa masomo wa 2004/05 na kama zitapatikana zitaiwezesha Serikali kukopesha wahitaji wengi zaidi kuliko idadi ya sasa", alisisitiza. Naibu Waziri Mulugo alisema hayo alipozungumza kwenye sherehe za mahafali ya Saba ya Chuo Kikuu cha Mount Meru eneo la Ngaramtoni, nje kidogo ya mji wa Arusha. Nionavyo mimi Waziri huyu wa JK amekiri kushindwa kazi aliyopewa na bosi wake na hivyo kuwataka wanafunzi wa elimu ya juu kupitia maandamano wamsaidie kushinikiza waliokopeshwa fedha hizo wazirejeshe. Nimeshtushwa na kauli hii ya waziri mwenye dhamana ya kuhakikisha hayo madeni yanarudi akigawa kazi kwa wanafunzi ili wanafunzi wakishindwa kuandamana "vizuri" ionekane wanafunzi ndio wameshindwa kushinikizwa zirejeshwe. Ni utendaji wa aina hii hii wa Mawaziri/watendaji wetu wameifikisha nchi yetu hapa ilipo, hali ni hivi hivi TIB, EPA, na maeneo mbalimbali ambayo Serikali imekopesha. Je hii maana yake ni kwamba Waziri hana takwimu za waliokopeshwa???Huu utaratibu wa kutaka walokopeshwa warejeshe pesa hizo kwa maandamano ya wanafunzi umeanza lini?? Kama ni utaratibu mpya wa kudai mbona hamjatuambia tuandamane kudai 40 Bil za Kagoda na zaid ya 130 Bil za Deep Green na ndugu zake???Au zile hazifai kusomesha wanafunzi wetu au zile huna uchungu nazo kwa vile mmekula ninyi viongozi???Uchungu huo Waziri wa Serikali hii umeupata wapi wakati kila kukicha mnafanya ufisadi??unatutaka tuandamane wakati mmesema Al Shabaab wanatuvizia lengo lako ni nini????au Al shabaab wameshatoweka???? Huoni kufanya maandamano ya kipuuzi kama hayo ni kulishushia Taifa hadhi kwa kushindwa kwako kufanyakazi????Kama kunaugumu wa kupata fedha hizo kutoka kwa wanafunzi waliokopeshwa, kweli majizi ya EPA yalirejesha fedha zetu au sanaa tu???? Mi nadhani unataka kuficha uzembe wa Serikali kwa kuwatupia lawama waliokopeshwa. Hakuna asiyejua kuwa Serikali ni legelege. Hivyo kwa kuwa mshashindwa kufwatilia Kagoda, Deep Green na Tangold zenye zaidi ya 200Bil zilizoliwa na majizi, nashauri hata hizi mlizokopesha wanafunzi mtemane nazo kwani zimerudi kwa walipa kodi wenyewe. Mwisho, kwa kukiri kushindwa kulifanyia kazi suala dogo kama hili, nadhani umepoteza sifa ya kuendelea madarakani mana hujui ulifanyalo na ninashauri ujiuzuru mara moja mana inaonekana unalipwa mshahara wa bure na kulitia Taifa hasara. Wanajamvi naliwasilisha kwenu ili tujadili kama Tanzania hii choka mbaya inahitaji Waziri mwenye utendaji wa kibabaishaji kama wa aina hii wa kutaka marejesho kwa maandamano????? Source: Mwananchi Sunday, 06 November, 2011 |