Kurzweil
JF-Expert Member
- May 25, 2011
- 6,622
- 8,397
Naibu waziri wa mambo ya ndani Mh. Hamad Yusuf Masauni amepiga marufuku askari wa jeshi la zimamoto na uokoaji kwenda sehemu zenye majanga ya moto bila kuwa na uhakika kwamba vitendea kazi pamoja na magari yenye maji ya kutosha, vinaweza kuhimili na kudhibiti maafa ya moto na kuonya kwamba ofisa wa jeshi hilo atakayeruhusu uzembe huo serikali haitasita kumuajibisha.
Naibu waziri huyo wa mambo ya ndani ya nchi, ameyasema hayo wakati akizungumza na askari wa jeshi la zimamoto na uokoaji wa wilaya za Nyamagana na Ilemela mkoani Mwanza.
Baadhi ya viongozi wa jeshi la zimamoto na uokoaji mkoani Mwanza wamemweleza naibu waziri Hamad Yusuf Masauni baadhi ya changamoto zinazolikabili jeshi hilo.
Jumla ya matukio 38 ya moto na mengine 23 ya uokozi yametokea katika mkoa wa Mwanza.
Wizara ya mambo ya ndani imeajiri askari 800 wa jeshi la zimamoto na uokoaji katika mwaka huu wa fedha ulioanza julai mosi ambao wanasubiri kupangwa katika vituo vyao vya kazi ikiwa ni hatua ya kukabiliana na changamoto za uhaba wa askari na vitendea kazi yakiwemo magari.
Naibu waziri huyo wa mambo ya ndani ya nchi, ameyasema hayo wakati akizungumza na askari wa jeshi la zimamoto na uokoaji wa wilaya za Nyamagana na Ilemela mkoani Mwanza.
Baadhi ya viongozi wa jeshi la zimamoto na uokoaji mkoani Mwanza wamemweleza naibu waziri Hamad Yusuf Masauni baadhi ya changamoto zinazolikabili jeshi hilo.
Jumla ya matukio 38 ya moto na mengine 23 ya uokozi yametokea katika mkoa wa Mwanza.
Wizara ya mambo ya ndani imeajiri askari 800 wa jeshi la zimamoto na uokoaji katika mwaka huu wa fedha ulioanza julai mosi ambao wanasubiri kupangwa katika vituo vyao vya kazi ikiwa ni hatua ya kukabiliana na changamoto za uhaba wa askari na vitendea kazi yakiwemo magari.