Donatila
JF-Expert Member
- Oct 23, 2014
- 7,557
- 21,497
NAIBU Waziri wa Madini, Dotto Biteko amelitaka Shirika la Taifa la Madini (Stamico) kujitathini kuhusu utendaji wao wa kazi kwa Taifa kutokana na kuwa deni kubwa kuliko uzalishaji wa shirika hilo.
Biteko ametoa kauli hiyo alipotembelea Shirika la Taifa la Madini (Stamico) leo, Dar es Salaam,ambapo amesema Stamico imekuwa na madeni yanayofanya kudidimiza shirika kutokana na miradi wanayoiendesha ya uchimbaji kushindwa kuzalisha faida.
Amesema baada ya watu kujua changamoto sasa ndio wameona sehemu kujengea hoja katika taarifa mbalimbali.Biteko amesema Stamico ilitakiwa kuwa sehemu ya kujifunzia kwa wachimbaji wadogo lakini wachimbaji wadogo hawawezi kufika Stamico kwa sababu hakuna cha kujifunza.
Stamico inadeni zaidi ya Sh.bilioni moja pamoja na deni la Stamigold la Sh.bilioni 54 na Serikali inatakiwa kulipa deni hilo na kuacha kununua madawati katika shule.Biteko amesema kuwa kunahitajika kuwepo ubunifu kwa Stamico kwa kujiona wana kazi ya ziada ya kusaidia Taifa kupiga hatua.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Stamico, Alex Rutagwelela amesema kuwa maagizo watayafanyia kazi katika uendeshaji wa shirika hilo.
Chanzo: Michuzi.
Biteko ametoa kauli hiyo alipotembelea Shirika la Taifa la Madini (Stamico) leo, Dar es Salaam,ambapo amesema Stamico imekuwa na madeni yanayofanya kudidimiza shirika kutokana na miradi wanayoiendesha ya uchimbaji kushindwa kuzalisha faida.
Amesema baada ya watu kujua changamoto sasa ndio wameona sehemu kujengea hoja katika taarifa mbalimbali.Biteko amesema Stamico ilitakiwa kuwa sehemu ya kujifunzia kwa wachimbaji wadogo lakini wachimbaji wadogo hawawezi kufika Stamico kwa sababu hakuna cha kujifunza.
Stamico inadeni zaidi ya Sh.bilioni moja pamoja na deni la Stamigold la Sh.bilioni 54 na Serikali inatakiwa kulipa deni hilo na kuacha kununua madawati katika shule.Biteko amesema kuwa kunahitajika kuwepo ubunifu kwa Stamico kwa kujiona wana kazi ya ziada ya kusaidia Taifa kupiga hatua.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Stamico, Alex Rutagwelela amesema kuwa maagizo watayafanyia kazi katika uendeshaji wa shirika hilo.
Chanzo: Michuzi.