KING DUBU
JF-Expert Member
- Mar 7, 2017
- 919
- 1,239
Kwa muda wa zaidi ya wiki mbili sasa Korosho za wakulima zimeshindwa kwenda mnadani katika vyama vya msingi vilivyo vingi kama si vyote.
Kinachoelezwa chanzo ni ukosefu wa Magunia ya kuhifadhia na kusafirishia Korosho. Hali hii inaharibu kama si kuua soko la Korosho ambalo linaingiza mapato makubwa hapa Tanzania.
Wananchi walio wengi mbumbumbu wanalalamika bila msaada wowote huku viongozi wa kisiasa nao wakionekana hawana msaada kwao.
Hivyo waziri wa kilimo shughulikia tatizo hili ili Korosho ziende sokoni na wakulima wapate sitahiki zao japo bei yenyewe ni chini ya 2500.
Ni vipi magunia yakosekane wakati wakulima wanakatwa zaidi ya Tsh 261 ambayo ndani yake fedha ya kununulia hayo magunia IPO?
Kinachoelezwa chanzo ni ukosefu wa Magunia ya kuhifadhia na kusafirishia Korosho. Hali hii inaharibu kama si kuua soko la Korosho ambalo linaingiza mapato makubwa hapa Tanzania.
Wananchi walio wengi mbumbumbu wanalalamika bila msaada wowote huku viongozi wa kisiasa nao wakionekana hawana msaada kwao.
Hivyo waziri wa kilimo shughulikia tatizo hili ili Korosho ziende sokoni na wakulima wapate sitahiki zao japo bei yenyewe ni chini ya 2500.
Ni vipi magunia yakosekane wakati wakulima wanakatwa zaidi ya Tsh 261 ambayo ndani yake fedha ya kununulia hayo magunia IPO?