Naibu Waziri wa Afya Dkt. Molel, si kila ziara lazima usimamishe mfanyakazi kazi ndiyo uonekane umefanya kazi. Kuwa mbunifu

kifupi kirefu

JF-Expert Member
Oct 29, 2018
539
3,507
Nimemsikiliza Naibu Waziri wa Afya akiwa Longido, Kwanza haeleweki ameenda kukagua nini. Haeleweki anavyozungumzia mapungufu katika ujenzi wa kituo cha afya tatizo ni mganga mkuu wa Wilaya, Mkurugenzi, Mkandarasi au ni kiumbe gani anapaswa kulaumiwa na kwa makosa gani.

Pamoja ukweli kwamba hata wanaomsikiliza hawamuelewi, ameenda mbali zaidi na kumsimamisha kazi Mganga Mkuu, sijui mganga mkuu ndiye anayekusanya fedha za ujenzi wa hospital kwa wananchi?

Haya mamlaka Mganga wa Wilaya anayatoa wapi? Mkurugenzi kazi yake nini? Je mkuu wa Wilaya wa eneo ilo alikuwa wapi asione tatizo hadi naibu wa Waziri aliyetumia chini ya masaa mawili aone tatizo, alifanyie uchunguzi na kutoa hukumu?

Kwa aina hii ya Mawaziri nadhani itatuchukua dahari na dahari kuendelea. Tuheshimu taaluma za watu na tutendee haki taaluma zetu.
 
Pamoja ukweli kwamba hata wanaomsikiliza awamwelewi, ameenda mbali zaid na kumsimamisha kazi Mganga mkuu, sijui mganga mkuu ndiye anayekusanya fedha za ujenzi wa hospital kwa wananchi? Haya mamlaka mganga wa Wilaya anayatoa wapi? Mkurugenz kazi yake nn? Je mkuu wa Wilaya wa eneo ilo alikuwa wapi asione tatizo Hadi naibu wa Waziri aliyetumia chini ya masaa mawili aone tatizo, alifanyue uchunguzi na kutoa hukumu?
Pitia kazi za mganga mkuu wa wilaya, angalia miradi ya afya inasimamiwa na nani halafu uje tena hapa
 
Nimemsikiliza Naibu Waziri wa Afya akiwa Longido, Kwanza haeleweki ameenda kukagua Nini? Aeleweki anavyozungumzia mapungufu katika ujenzi wa kituo Cha afya tatizo ni mganga mkuu wa Wilaya, Mkurugenzi, Mkandarasi au ni kiumbe gani anapaswa kulaumiwa na kwa makosa gani...
Mkuu umeongea vema, jana nami nilimuona NW akifokafoka kama vile anaongea na watoto wake, tatizo kubwa huo ndio mfumo ambao Rais aliyewateua anataka waufanyie kazi,

Unakumbuka alivyokuwa Kigwangala ? Lakini pia nimeona juzi hapa waziri mmoja anaagiza eti kazi ya ujenzi wa madarasa Nchi nzima uwe umekamilika kufikia mwisho wa mwezi huu, yaani hapa zimebaki siku kama 5 tu hivi, hapo ilikuwa tarehe 15/12/2020.

Hapa ninapoishi kuna madarasa yameanza kujengwa mwanzoni mwa mwaka huu na sioni dalili kama yatakamilika ujenzi wake kwa siku tano zilizosalia, (maana yake ni kwamba alikuwa anatoa maelekezo ambayo hayawezi kutekelezeka)
 
Mitano tena!
Watanzania wajiandae kutoa jasho la damu, maana washamba wameshika nchi tena.
Wabunge Wanapishana Majukwaani Kutaka Vijana Wajiajiri Hali yakua, Bunge Hili Hilo Lilipitisha Malipo Ya
1. YouTube-1,100,000
2. Blog-1,100,000
3. Mafunzo Ya Drone-1,980,000

Hivi kweli Mna dhamira Ya Kutaka Vijana Wajiajiri au madish huwa yakiyumba mnaropoka chochote.

Hivi Kijana Wa Kitanzania mwanaccm aliyekosa kibarua cha kujibu hoja za wapinzani anatoa Wapi Hizi Fedha?

Busara na majivuno havikai nyumba moja.
 
Sasa Kama amaeona Kuna tatizo?

kiufupi hospital za serikali huduma zao NI MBOVU NA WAMEJISAHAU. Pia wana dharau acha wapambane na Hali zao.

Au wewe Ni mfanyakazi wa hospital?

BADILIKENI
Kwa hiyo akitumbuwa tumbuwa ndo anaonekana mchapakazi?
 
Back
Top Bottom