Naibu Waziri Wa Afya ameupongeza uongozi wa Wilaya ya Ileje Mkoa wa Songwe kwa kusimamia vyema fedha za ujenzi wa hospitali ya wilaya

Wizara ya Afya Tanzania

Official Account
Oct 1, 2020
58
124


Naibu Waziri Wa Afya, Maendeleo Ya Jamii, Jinsia, Wazee Na Watoto Dkt. Godwin Mollel ameupongeza uongozi wa Wilaya ya Ileje Mkoa wa Songwe kwa kusimamia vyema fedha za ujenzi wa hospitali ya wilaya kwa kujenga majengo ambayo thamani ya fedha inaonekana.

Dkt Mollel amesema hayo alipokwenda wilayani humo kukagua hatua za ujenzi wa hospitali hiyo ambapo Serikali imetoa kiasi cha tsh bilioni 1.8 kwa ajili ya ujenzi

Dkt. Mollel ameonyeshwa kushangazwa na wilaya ambazo zimepewa kiasi sawa cha fedha na kushindwa kukamilisha ujenzi na kuzikata Wilaya ambazo zinasua sua kukamilisha ujenzi kuiga mfano wa Wilaya ya Ileje.

Bofay hapa kuona video
 
Back
Top Bottom