Naibu Waziri: Timu zinapofungwa na Yanga zikubaliane na matokeo

beth

JF-Expert Member
Aug 19, 2012
3,877
6,326
i7mu6n.jpg

Naibu Waziri wa Utumishi na Utawala Bora, Deogratius Ndejembi, amesema kumekuwepo na tabia ya Viongozi wa timu mbalimbali Nchini kutoa kauli za kwamba walihongwa hususan wanapofungwa na Yanga.

Akiwa Bungeni Dodoma amesema, "Ifike wakati Viongozi wa Timu hizi na Watanzania kwa ujumla wakubali kwamba Yanga ndio Timu bingwa hapa Tanzania na bora Afrika, kwahiyo wanapofungwa wakubaliane na matokeo"

Aidha, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Innocent Bashungwa amesema Serikali haitofumbia macho wanaotumia Rushwa kujipatia ushindi.
 
tukutane kwa Mkapa 8/5/2021.......tutajua nani ni BORA zaidi....👏👏
 
Duuuu, kaongea kishabiki sana, Angejiuliza mbona timu hizo hizo zinapofungana zenyewe au kufungwa na Azam hamna malalamiko kama hayo?

NB: Kuweka ushabiki pembeni Yanga ni timu kubwa Tanzania na si bora kama asemavyo.
 
Naibu Waziri wa Utumishi na Utawala Bora, Deogratius Ndejembi, amesema kumekuwepo na tabia ya Viongozi wa timu mbalimbali Nchini kutoa kauli za kwamba walihongwa hususan wanapofungwa na Yanga.

Akiwa Bungeni Dodoma amesema, "Ifike wakati Viongozi wa Timu hizi na Watanzania kwa ujumla wakubali kwamba Yanga ndio Timu bingwa hapa Tanzania na bora Afrika, kwahiyo wanapofungwa wakubaliane na matokeo"

Aidha, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Innocent Bashungwa amesema Serikali haitofumbia macho wanaotumia Rushwa kujipatia ushindi.
NAKAZIAAAAAA
 
Back
Top Bottom