Naibu Waziri TAMISEMI, David Silinde aagiza vipindi vya Dini viwe vya lazima kwenye Shule kupunguza uovu

Cannabis

JF-Expert Member
Jan 20, 2014
8,938
25,279
Naibu Waziri TAMISEMI, David Silinde ameagiza vipindi vya Dini viwe vya lazima kwenye Shule zote ili kupunguza uovu sababu Wanafunzi wenye hofu ya Mungu hawawezi fanya utovu wa nidhamu kama kuchoma Shule “Atake asitake, ahudhurie hata kama hafanyii Mtihani”

 
Kama kufundishwa dini kunafanya usiwe muovu, jiwe asingekuwa muovu maana alikuwa anaenda kanisani na kujionyesha kuwa ni mcha Mungu.
 
Matamko yameanza Tena,kwani mitaala yetu inasemaje?Hawa watu wa matamko na hisia tuwe nao makini,yeye anaushahidi upi kuwa dini inapunguza maasi,mbona huko zilikoanzia hizi dini ndo Kuna maovu kuliko sisi huku.

Huyu jamaa Bure kabisa
 
Nchi ina mizigo mizito sana hii. Badala ya kufundishwa uzalendo na kujitambua!
 
Siyo kuchoma shule tu hata kuiba kura na kuingia madarakani bila ridhaa ya wananchi pia nao ni uovu.
 
Kwa sasa kumekuwa na mmomonyoko mkubwa sana wa MAADILI hapa NCHINI ikiwa ni pamoja na Matumizi mabaya ya mitandao Kama kuweka picha na video chafu mitandaoni, ukahaba, umalaya, Matumizi ya madawa ya kulevya,ukatili wa kijinsia, Matumizi mabaya ya madaraka,ubadhilifu, utakatishaji Fedha, uhujumu uchumi yote hayo na mengine yanasabaishwa na ukosefu wa MAADILI pamoja na ATHARI ZA UTANDAWAZI.

Licha ya hatua kadhaa zilizochukuliwa na SERIKALI ikiwa ni pamoja na kuweka Sheria za uhujumu uchumi,utakatishaji Fedha,Sheria za maudhui mitandaoni,uanzishwaji wa mahakama za mafisadi,uanzishwaji wa madawati ya kijinsia lakini bado bado matukio yamekuwa yakiendelea kutokea kila kukicha hapa nchini

Sasa wakati umefika wa Serikali kupambana na changamoto hizi Kiroho na Kisaikolojia kwa KUFANYA SOMO LA DINI KUWA NI LA LAZIMA KUANZIA SHULE ZA AWALI HADI VYUONI, hii itwajenga watoto na vijana kufahamu kwamba kufanya matukio au matendo mabaya ni DHAMBI NA MAKOSA MAKUBWA KWA MUNGU kuliko hata kwa SERIKALI, hivyo itaisaidia NCHI katika KUKABILIANA NA MATUKIO OVU hapa NCHINI, vijana wengi wamekuwa wanakuwa KISASA ZAIDI bila kuwa na hofu ya mungu KABISA, hii ndo inapelekea matukio MABAYA KUENDELEA kutokea hapa NCHINI

Naamini SERIKALI ikiweka MPANGO MKAKATI katika hili SUALA litaleta ufanisi mkubwa Sana katika siku za USONI Kama likianza kufanyiwa kazi hivisasa.
 
Kwa sasa kumekuwa na mmomonyoko mkubwa sana wa MAADILI hapa NCHINI ikiwa ni pamoja na Matumizi mabaya ya mitandao Kama kuweka picha na video chafu mitandaoni, ukahaba, umalaya, Matumizi ya madawa ya kulevya,ukatili wa kijinsia, Matumizi mabaya ya madaraka,ubadhilifu, utakatishaji Fedha, uhujumu uchumi yote hayo na mengine yanasabaishwa na ukosefu wa MAADILI pamoja na ATHARI ZA UTANDAWAZI.

Licha ya hatua kadhaa zilizochukuliwa na SERIKALI ikiwa ni pamoja na kuweka Sheria za uhujumu uchumi,utakatishaji Fedha,Sheria za maudhui mitandaoni,uanzishwaji wa mahakama za mafisadi,uanzishwaji wa madawati ya kijinsia lakini bado bado matukio yamekuwa yakiendelea kutokea kila kukicha hapa nchini

Sasa wakati umefika wa Serikali kupambana na changamoto hizi Kiroho na Kisaikolojia kwa KUFANYA SOMO LA DINI KUWA NI LA LAZIMA KUANZIA SHULE ZA AWALI HADI VYUONI, hii itwajenga watoto na vijana kufahamu kwamba kufanya matukio au matendo mabaya ni DHAMBI NA MAKOSA MAKUBWA KWA MUNGU kuliko hata kwa SERIKALI, hivyo itaisaidia NCHI katika KUKABILIANA NA MATUKIO OVU hapa NCHINI, vijana wengi wamekuwa wanakuwa KISASA ZAIDI bila kuwa na hofu ya mungu KABISA, hii ndo inapelekea matukio MABAYA KUENDELEA kutokea hapa NCHINI

Naamini SERIKALI ikiweka MPANGO MKAKATI katika hili SUALA litaleta ufanisi mkubwa Sana katika siku za USONI Kama likianza kufanyiwa kazi hivisasa.
agenda people, acha kupotosha community yako ww. kabla ya mkoloni ulikua unaabudu nn. unazingua
 
Back
Top Bottom