Naibu Waziri Awesso : " Wasoma mita za maji mnaongeza bili"

Mkogoti

TAPELI Mkubwa
May 3, 2020
2,416
3,911
Serikali imewaagiza Wakurugenzi wa Mamlaka zote za Maji nchini wahakikishe watumiaji wa maji wanashirikishwa kikamilifu katika usomaji mita ili kutambua gharama halisi wanazopaswa kulipa na kuepuka kubabikiziwa bili kubwa kuliko matumizi

Agizo hilo limetolewa na Naibu Waziri wa maji Jumaa Aweso akiwa kwenye ziara ya kikazi ya kukagua miradi ya maji katika Wilaya ya Chamwino Mkoani Dodoma.
 
Nilishawahi kuhoji hii kitu, utaratibu unaotumika kusoma meter za maji sio rafiki, kuna wafanyakazi wavivu/ wasiowaadilifu anaweza kujikadiria tu. Ilipaswa kuwe na rekodi kwa mtumiaji kuhakiki pale anapoletewa bil.

Pia hili tatizo lipo kwa wale wenye meter za umeme za zamani ambao hawana luku.
 
Back
Top Bottom