kamati ya ufundi
JF-Expert Member
- Sep 30, 2014
- 416
- 438
Na Mwandishi Wetu
NAIBU Spika, Mussa Zungu, ambaye Mbunge wa Ilala ameanza kutumiwa na Imam wa Msikiti wa Madina, Sheikh Ally Mohammed Alidina, ambaye pia anajulikana kwa jina la Ally Mmanga ambaye ni msomaji maarufu wa milango maulidini ili kumeteta katika kesi ya kugushi wosia na kuuza nyumba ya wakfu.
Imamu huyo pamoja na baadhi ya ndugu zake, akiwemo Amini Alidina wanatuhumiwa kuuza nyumba ya baba yao Sheikh Mohammed Alidina , ambaye alikuwa Sheikh maarufu wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA).
Taarifa za kuaminika ilizozipata zinaeleza Sheikh Ali Mmanga amekuwa akiitumia ofisi ya Naibu Spika huyo kukwepa mkono wa sheria, baada ya wao kuuza nyumba yao yenye msikiti na madrasa kwa mfanyabiashara Michael Singano alioko Kariakoo, Dar es Salaam.
Nyumba hiyo yenye ghorofa sita, inadaiwa kuuzwa kwa zaidi ya bilioni 8, ambapo mfanyabiashara huyo kwa kushirikiana na Sheikh Ally Mmanga kuchukua zaidi ya bilioni 4 kama malimo ya awali.
Fedha hizo zimetolewa na kugawanya kwa watu mbalimbali, akiwemo mmoja wa watu wanaotajwa kushiriki katika mauzo hayo anaitwa Mswaki, ambaye ndio mtafuta mteja.
Hata hivyo, baada ya Jeshi la Polisi kuingilia kati na kumuhoji Sheikh Ali Mmanga pamoja na mdogo wake Amini na kuwatoa kwa dhamana, watu hao wameanza kumtumia Naibu Spika kuzima sakata hilo.
Taarifa zilizoaminika zinaeleza kuwa Sheikh Ali Mmanga baada ya kuhojiwa na kutoka kwa dhamana amekuwa akimtaka Zungu aingilie kati suala hilo ili kumuokoa kutokana na Polisi kusmama kidete.
“Amekuwa akija ofisini hapa Ilala mara kwa mara na muda mwingine akimpigia simu akitaka amsaidie ili kukwepa mkono wa sheria. Jambo ambalo sio haki na anapaswa kucha akiwa kamą kiongozi,’’ alisema mtoa taarifa wetu.
Alisema Rais Samia Suluhu Hassan amekuwa kiongozi anayejali wanyonge, viongozi wanaowasaidia matapeli wanapaswa kuelezwa kuacha na vyombo vya dola vichukue hatua.
‘’Huyu Sheikh anatumia vibaya Msikiti na waumini wa Msikiti wa Madina watambue wana sheikh asiyefuata maadili ya dini, amekuwa tapeli na mtu anayetumia kofia ya dini kujificha’’alisema.
Alisema hata vitabu vya dini ikiwemo Quraan inaeleza juu ya umuhimu wa wasia, lakini cha ajabu anauza nyumba hiyo ambayo marehemu baba yake alisema nyumba isiuzwe kwa kuwa kuna Msikiti na Madrasa.
Sheikh Mohammed Alidina aliandika wosia toka mwaka 2007 ikiwemo kugawa maduka kwa watoto wote, kuweka msikiti unaotumiwa kwa wafanyabiashara na madrasa ya watoto na kuala nyumba hiyo isiuzwe.
Hivyo, katika wosia huo, alisema nyumba hiyo haipaswi kuuzwa kwa mtu yeyote, ambapo Sheikh Ally Mmanga bila hofu na akiwa Imam wa Msikiti wa Madina ameshiriki katika kuuza nyumba hiyo pamoja na ndugu zake wengine ambao amekuwa akiwatisha mara kwa mara.View attachment 2458737
NAIBU Spika, Mussa Zungu, ambaye Mbunge wa Ilala ameanza kutumiwa na Imam wa Msikiti wa Madina, Sheikh Ally Mohammed Alidina, ambaye pia anajulikana kwa jina la Ally Mmanga ambaye ni msomaji maarufu wa milango maulidini ili kumeteta katika kesi ya kugushi wosia na kuuza nyumba ya wakfu.
Imamu huyo pamoja na baadhi ya ndugu zake, akiwemo Amini Alidina wanatuhumiwa kuuza nyumba ya baba yao Sheikh Mohammed Alidina , ambaye alikuwa Sheikh maarufu wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA).
Taarifa za kuaminika ilizozipata zinaeleza Sheikh Ali Mmanga amekuwa akiitumia ofisi ya Naibu Spika huyo kukwepa mkono wa sheria, baada ya wao kuuza nyumba yao yenye msikiti na madrasa kwa mfanyabiashara Michael Singano alioko Kariakoo, Dar es Salaam.
Nyumba hiyo yenye ghorofa sita, inadaiwa kuuzwa kwa zaidi ya bilioni 8, ambapo mfanyabiashara huyo kwa kushirikiana na Sheikh Ally Mmanga kuchukua zaidi ya bilioni 4 kama malimo ya awali.
Fedha hizo zimetolewa na kugawanya kwa watu mbalimbali, akiwemo mmoja wa watu wanaotajwa kushiriki katika mauzo hayo anaitwa Mswaki, ambaye ndio mtafuta mteja.
Hata hivyo, baada ya Jeshi la Polisi kuingilia kati na kumuhoji Sheikh Ali Mmanga pamoja na mdogo wake Amini na kuwatoa kwa dhamana, watu hao wameanza kumtumia Naibu Spika kuzima sakata hilo.
Taarifa zilizoaminika zinaeleza kuwa Sheikh Ali Mmanga baada ya kuhojiwa na kutoka kwa dhamana amekuwa akimtaka Zungu aingilie kati suala hilo ili kumuokoa kutokana na Polisi kusmama kidete.
“Amekuwa akija ofisini hapa Ilala mara kwa mara na muda mwingine akimpigia simu akitaka amsaidie ili kukwepa mkono wa sheria. Jambo ambalo sio haki na anapaswa kucha akiwa kamą kiongozi,’’ alisema mtoa taarifa wetu.
Alisema Rais Samia Suluhu Hassan amekuwa kiongozi anayejali wanyonge, viongozi wanaowasaidia matapeli wanapaswa kuelezwa kuacha na vyombo vya dola vichukue hatua.
‘’Huyu Sheikh anatumia vibaya Msikiti na waumini wa Msikiti wa Madina watambue wana sheikh asiyefuata maadili ya dini, amekuwa tapeli na mtu anayetumia kofia ya dini kujificha’’alisema.
Alisema hata vitabu vya dini ikiwemo Quraan inaeleza juu ya umuhimu wa wasia, lakini cha ajabu anauza nyumba hiyo ambayo marehemu baba yake alisema nyumba isiuzwe kwa kuwa kuna Msikiti na Madrasa.
Sheikh Mohammed Alidina aliandika wosia toka mwaka 2007 ikiwemo kugawa maduka kwa watoto wote, kuweka msikiti unaotumiwa kwa wafanyabiashara na madrasa ya watoto na kuala nyumba hiyo isiuzwe.
Hivyo, katika wosia huo, alisema nyumba hiyo haipaswi kuuzwa kwa mtu yeyote, ambapo Sheikh Ally Mmanga bila hofu na akiwa Imam wa Msikiti wa Madina ameshiriki katika kuuza nyumba hiyo pamoja na ndugu zake wengine ambao amekuwa akiwatisha mara kwa mara.View attachment 2458737