Uchaguzi 2020 Naibu Msajili wa Vyama vya Siasa ataka Wagombea kuhakikisha kampeni zao hazivunji Sheria

beth

JF-Expert Member
Aug 19, 2012
3,877
6,326
Naibu Msajili wa Vyama vya Siasa, Sisty Nyahoza, amewataka wagombea wa vyama vya siasa kuhakikisha kampeni zao hazivunji sheria kwa kusema uongo dhidi ya chama au mgombea mwingine.

Nyahoza aliyasema hayo jana katika mahojiano na chombo kimoja cha habari na kueleza kuwa matumizi ya uongo yanaweza kusababisha madhara makubwa kwa chama kinachoongelewa vibaya.

“Kunapotokea uchochezi au matumizi ya maneno ya uongo au matusi, Msajili wa Vyama huchukua jukumu la kukemea vitendo vya aina hii pale wanapokuwa na uhakika wa kutendeka kwa vitendo hivyo,” alisema.

Pia alisema Msajili ana jukumu la kutoa onyo na adhabu kwa chama au mgombea endapo kutakuwa na ukiukaji wa aina yoyote wa sheria.

“Kwa kutenda kosa hilo pia kuna ulipaji wa faini kati ya Sh. milioni 10 na Sh. Milioni 50 na kukisimamisha chama kufanya shughuli za siasa kwa muda uliopangwa. Endapo mgombea atashinda uchaguzi ikiwa bado amesimamishwa atalazimika kusubiri muda ufike ndipo aendelee na majukumu yake ya kiofisi,” alisema.

Pia Nyahoza aliwakumbusha wanasiasa kufanya siasa za kistaarabu kwa kuzingatia sheria za vyama vya siasa na kufuata taratibu za usajili ili kulinda kanuni zote za uchaguzi.

Chanzo: IPP MEDIA
 
Lissu endelea kupiga spana,Magufuli ameshakiuka sana sheria za kampeni na hajachukuliwa hatua!Hii inakupa mwanya wa wew kuendelea kupiga spana!
 
Mbona magufuli anatoa maagizo kwa watendaji kama nani ?Mbona hatuoni akichukuliwa hatua za kisheria!!
Hayo ni mambo ya kichochezi au kiutendaji? Tumieni akiri zenu acheni ujinga.

Kama kuna sheria inayohusu hilo ilete hapa.
 
Jana nimemsikia mwigulu akiwaongopea wananchi mbona hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa.au vyama vya siasa ni vya upinzani pekee.
 
1600839925027.png

MAGUFULI NDIYE RAIS WA TLP WANA TLP TUMCHAGUE MAGUFULI
 
Back
Top Bottom