Naibu Meya wa Jiji la Arusha awapa somo viongozi wa Chadema...!

Konakali

JF-Expert Member
Dec 15, 2009
1,533
263
NAIBU Meya wa Jiji la Arusha ambaye ni Diwani kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo
(Chadema), amewataka viongozi wa juu wa chama hicho kuacha kuwadanganya wakazi wa Jiji la Arusha kwamba watafanikiwa kumwondoa Meya wa Jiji hilo.

Diwani huyo wa Kata ya Kimandolu, Estomii Mallah, amemtaka Katibu Mkuu wa Chadema,
Dk. Willibrod Slaa na wenzake, kuacha kuwadanganya wananchi wa Arusha na Watanzania kuhusu sakata la umeya wa Arusha kwa kuwa hakuna tena njia ya kumtengua katika nafasi hiyo meya wa CCM aliyepo madarakani, Gaudance Lyimo.

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, Mallah alisema mbali na siku 30 za kisheria za kufungua shauri mahakamani la kumpinga meya huyo kupita, pia Dk. Slaa alikuwa na taarifa kuhusu muafaka uliofikiwa kati ya madiwani wa Chadema na CCM na aliubariki.

“Hivi jamani kuna njia gani tena ya kumuondoa Gaudance pale na kusema hakuchaguliwa kihalali maana siku 30 za kisheria zimemalizika baada ya wao wenyewe viongozi kuvutana vutana na ahadi zao hewa sasa leo unawadanganywa wananchi kuwa hamuungi mkono meya mpaka lini,” alisema Mallah.

Alisema amekuwa akipokea ujumbe mbalimbali kutoka kwa wananchi wa Jimbo la Arusha
kuhusu ushauri wa yeye kuufuata, lakini alitumia njia hiyo kuwaomba radhi kuwa hatoweza kufuata ushauri wao kwa kuwa kutairudisha Halmashauri katika mvutano.

Aidha, amewaonya vijana na wananchi mbalimbali wanaoshabikia jambo hilo kuwa pindi vurugu itakapotokea, hawatakuwa na mahali pa kukimbilia zaidi ya vijijini kwao walikotokea
kwa hofu ya kudhurika.

Pia aliwaonya wafanyabiashara wakubwa wanaoendelea kusaidia malumbano, akisema hayana faida kwao zaidi ya hasara ya kusababisha biashara za hoteli na utalii kushuka kutokana na wageni kuhofia hali ya usalama wao Arusha.

Alishauri wananchi wa Arusha kukaa na kutafakari wenyewe jinsi ya kuirejesha amani iliyopotea kwani haiwezekani kusubiri watu wa nje kuja kuwapatanisha na kuwarejeshea amani hiyo kwa kuwa wao hawaathiriki na lolote pindi amani hiyo inapokosekana.

Alisema yeye na madiwani wenzake wanne waliovuliwa uanachama Chadema, hawana
ugomvi na kiongozi ye yote wa Chadema na ndiyo maana pindi walipopatiwa taarifa ya kuvuliwa uanachama walikimbilia mahakamani ili kudai kurejeshewa uanachama wao.

Source: Habari Leo; by John Mhala, Arusha; Tarehe: 6th October 2011
 
Mjadala wa Arusha ulishafungwa na maamuzi makini na ya busara yalishafanywa na Viongozi hodari wa Chadema, sasa wewe kama unajipya kasimulie familia yako.
 
Jiji la Arusha halina naibu meya, sasa sijui huyu anayetajwa hapa gazeti la jamboleo wamemtoa wapi? Huu ni uandishi wa habari wa ajabu sana.
 
Huyo mwandishi nadhani hajui kinachoendelea hapa nchini! Mallah sio diwani tena! Kwahiyo anamtambulisha kimakosa.
Na huyu mallah anatafuta pa kujishika maana anaanguka. Aman gani imetoweka Arusha? Watalii wamepungua kwa kiasi gani! Leo anasema hana ugomvi na viongozi wa cdm! Kwann aliwapeleka mahakamani?
Huyu ni mnafiki mkubwa and he's the one behind kutimuliwa kwake na wenzake. Sasa anatapatapa na kujifanya kutoa ushauri. Kama alijua haiwezekani kumwondoa meya mbona aliingia muafaka kwa kuhongwa badala ya kutumia busara? Apeleke ujinga wake huko!
Wakazi wa Arusha wameshaamua kutokumtambua wala kumpa ushirikiano huyo mmea hadi sheria itakapofuatwa. That is the end of the story!
Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibarika Arusha!
 
NAIBU Meya wa Jiji la Arusha ambaye ni Diwani kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo
(Chadema), amewataka viongozi wa juu wa chama hicho kuacha kuwadanganya wakazi wa Jiji la Arusha kwamba watafanikiwa kumwondoa Meya wa Jiji hilo.

Diwani huyo wa Kata ya Kimandolu, Estomii Mallah, amemtaka Katibu Mkuu wa Chadema,
Dk. Willibrod Slaa na wenzake, kuacha kuwadanganya wananchi wa Arusha na Watanzania kuhusu sakata la umeya wa Arusha kwa kuwa hakuna tena njia ya kumtengua katika nafasi hiyo meya wa CCM aliyepo madarakani, Gaudance Lyimo.

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, Mallah alisema mbali na siku 30 za kisheria za kufungua shauri mahakamani la kumpinga meya huyo kupita, pia Dk. Slaa alikuwa na taarifa kuhusu muafaka uliofikiwa kati ya madiwani wa Chadema na CCM na aliubariki.

"Hivi jamani kuna njia gani tena ya kumuondoa Gaudance pale na kusema hakuchaguliwa kihalali maana siku 30 za kisheria zimemalizika baada ya wao wenyewe viongozi kuvutana vutana na ahadi zao hewa sasa leo unawadanganywa wananchi kuwa hamuungi mkono meya mpaka lini," alisema Mallah.

Alisema amekuwa akipokea ujumbe mbalimbali kutoka kwa wananchi wa Jimbo la Arusha
kuhusu ushauri wa yeye kuufuata, lakini alitumia njia hiyo kuwaomba radhi kuwa hatoweza kufuata ushauri wao kwa kuwa kutairudisha Halmashauri katika mvutano.

Aidha, amewaonya vijana na wananchi mbalimbali wanaoshabikia jambo hilo kuwa pindi vurugu itakapotokea, hawatakuwa na mahali pa kukimbilia zaidi ya vijijini kwao walikotokea
kwa hofu ya kudhurika.

Pia aliwaonya wafanyabiashara wakubwa wanaoendelea kusaidia malumbano, akisema hayana faida kwao zaidi ya hasara ya kusababisha biashara za hoteli na utalii kushuka kutokana na wageni kuhofia hali ya usalama wao Arusha.

Alishauri wananchi wa Arusha kukaa na kutafakari wenyewe jinsi ya kuirejesha amani iliyopotea kwani haiwezekani kusubiri watu wa nje kuja kuwapatanisha na kuwarejeshea amani hiyo kwa kuwa wao hawaathiriki na lolote pindi amani hiyo inapokosekana.

Alisema yeye na madiwani wenzake wanne waliovuliwa uanachama Chadema, hawana
ugomvi na kiongozi ye yote wa Chadema na ndiyo maana pindi walipopatiwa taarifa ya kuvuliwa uanachama walikimbilia mahakamani ili kudai kurejeshewa uanachama wao.

Source: Habari Leo; by John Mhala, Arusha; Tarehe: 6th October 2011

Well done kwa ufafanuzi kumbe hizi kelele za kina Slaa ni za mavuvuzela ambao wanaujua ukweli ila hawataki kuusema
 
Thinker msiwe sinkers tfadhali leteni mijadala yenye tija na si huu ujinga .Mwacheni huyu mpuuzi na wapuuzi wenzake wa magazeti wana hangaika tu .Kama hana ugomvi haya anayo sema si ugomvi ?Ana mchonganisha Slaa na wananchi siyo ?Atoe ushahidi kama anao juu ya madai yake .
 
Ndg Mala Ninakuheshimu sana, ningefurahi kama kwa sasa ungeamua kukaa kimya kabisa ili usisababishe machungu mioyoni mwetu. Sisi tunajua mpango mzima wa kuleta machafuko na vurugu zisizoisha hadi kipindi cha GodBless Lema kiishe bila maendeleo hapa Arusha. Lakini tuwaambie CCm kuwa hilo halitupi shida na CCM hatuitaki kabisa hapa Arusha, JK aendelee kuhamisha mikutano yetu muhimu huko Dar hilo pia hatujali, ila haya yote yanamwisho na siku moja atajibu!!!!!!!!!!
Serikali inauwezo wa kuleata muafaka wa kudumu lakini imebaki kufanya kuwa CDM ndiyo wenye matatizo huu ni uzushi mtupu.
 
Demkrasia na ndani ya vyama vya upinzani ni ndogo kuliko ccm

CCM ni chama pekee ambacho wanachama wake wana demokrasia.

Vyama vingine fuata amri kutoka uchagani hutaki kaa kimya ..
 
Sikapendi hako kagazeti kakina malinzi kwa kujikomba sikajisali kama nikagazeti ka ccm??kagazeti uchwara kanatoa habari uchwara kwakufaata siasa uchwara!!
 
Kama kwa kutamka kuwa huyu msaliti ni diwani, pengine ni kwa sababu akili zake zishahama huyo. Angoje tu kugombea tena kupitia chama kingine
 
NAIBU Meya wa Jiji la Arusha ambaye ni Diwani kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo
(Chadema), amewataka viongozi wa juu wa chama hicho kuacha kuwadanganya wakazi wa Jiji la Arusha kwamba watafanikiwa kumwondoa Meya wa Jiji hilo.

Diwani huyo wa Kata ya Kimandolu, Estomii Mallah, amemtaka Katibu Mkuu wa Chadema,
Dk. Willibrod Slaa na wenzake, kuacha kuwadanganya wananchi wa Arusha na Watanzania kuhusu sakata la umeya wa Arusha kwa kuwa hakuna tena njia ya kumtengua katika nafasi hiyo meya wa CCM aliyepo madarakani, Gaudance Lyimo.

Source: Habari Leo; by John Mhala, Arusha; Tarehe: 6th October 2011

huyu bado ni diwani?
 
Demkrasia na ndani ya vyama vya upinzani ni ndogo kuliko ccm

CCM ni chama pekee ambacho wanachama wake wana demokrasia.

Vyama vingine fuata amri kutoka uchagani hutaki kaa kimya ..

hakuna ulevi mbaya kama udini.maana upumbaza,upofusha na mwisho ni kujitoa mhanga!
 
Back
Top Bottom