Naibu Katibu Mkuu wa CUF-Maalim, Nassoro Mazrui, asisitiza kuwa, Maalim Seif hawezi kujiunga na CHADEMA. Adai Ana wafuasi wengi CUF.

Daimler

JF-Expert Member
Sep 11, 2018
556
973
IMG_8172.JPG


Naibu Katibu Mkuu wa CUF - Maalim, Nassoro Mazrui, akiongea na Mwananchi jana, alieleza imani yake kuwa, mgogoro wa Chama chao utamalizika na Maalim kuendelea kuwa Katibu Mkuu na kwamba suala la kuwania urais kupitia Chama kingine halipo. "Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif hawezi kukubali kuwania urais kupitia CHADEMA hata siku moja."
Mazrui aliongeza kuwa: Maalim hawezi kabisa kuhamia chama kingine kwa sababu ana wafuasi wake huku na wanaujua msimamo wake hivyo kinachotakiwa ni kuomba hatima ya mgogoro wa Chama ufikie mwisho tu lakini Maalim kuwania urais kupitia huko."
Aidha, msemaji wa Chama hicho, Mbarala Maharagande alisema kuwa, hilo la CHADEMA ni wazo zuri lakini uamuzi mgumu kama huo unatakiwa kutolewa na Vikao vya Baraza Kuu la CUF. "Ni kweli tumepokea ombi hilo ingawa sijajua wamekaa na Maalim wakaongea kuhusu hili. Muda ukifika Baraza litafanya uamuzi."
Mbarangande alimalizia kuwa: "Mgogoro wa Chama hicho utamalizika Oktoba."
IMG_8167.JPG

Hata hivya, mnamo Mei 2017, Katibu Mkuu, Maalim Seif alikaririwa na Mwananchi akisema kuwa, hawezi kuhamia CHADEMA hata kama Chama hicho kitaendelea kuwa na mgogoro hadi wakati wa Uchaguzi Mkuu ujao."
IMG_8167.JPG
 

Attachments

  • IMG_8170.JPG
    IMG_8170.JPG
    320.8 KB · Views: 22
Mchambuzi wa masuala ya kisiasa nchini, Prof. Gaudence Mpangala wa Chuo Kikuu cha RUCU, amemshauri Maalum Seif kuondoa CUF na kwenda kuanziasha Chama chake na kwamba Chama hicho kitapata nguvu na Chama hicho kitatoa ushindani mkubwa kwa CUF na CHADEMA kwa kuwa Maalum ana mtaji mkubwa wa wafuasi.
 
Naona ishu ya kuhamia maalim inashangiliwa sana na watu wa chama flani hivi, ni wanafiki wa kushededea, kwani akihamia ni zambi? Mtu hata awe na wafuasi wengi kiasi gani hilo haliwezi kumzuia kuhama, mgogoro wao unapigwa tarahe ndefu, 2020 inaweza kuwakuta hawajamaliza kesi, yanini kung'ang'ania lichama lenye mgogoro na mtu binafsi anaesaidiwa na serikali?
 
Wenye akili walishajua sababu ya cdm kushadadia mgogoro ndani ya cuf. Sasa hivi yale tuliyoyasema yameanza kudhihirika
 
Back
Top Bottom