Naibili
JF-Expert Member
- Jan 24, 2011
- 1,730
- 519
familia yetu tumekuwa wateja wazuri saana wa tanesco tangu miaka ya 80, na tumekuwa tukilipa bili bila usumbufu, tatizo limekuja mwaka huu mwezi wa 5, nimeletewa bili ya mil 4, wakati sikuwa na deni lolote, na wastani wa units tulizokuwa tunatumia tangu 2005 ni 150 units, nilipohoji deni linatoka wapi, nimejibiwa kuwa msomaji wa mita wa tanesco alikuwa anasoma mita vibaya tangu 2009, wakasema huyo mfanyakazi watamwajibisha, nikahoji kama ndivyo ina maana katika matumizi yangu kabla ya 2009 yalikuwa sahihi, wakasema ndio. kama ndivyo iweje kusiwe na tofauti ya wastani wa matumizi ya bili, kwani ukiangalia wastani wa matumizi ya umeme 2008 na 2009 hakuna tofauti, ni unit 120 wastani wa miezi 5, nilienda makao makuu ya tanesco wakaniambia hayo mazungumzo uliyofanya na viongozi wa mkoa yawekeni kwa maandishi na wenyewe wakujibu kwa maandishi ndo uje huku, lakini viongozi wa mkoa wamegoma hata kupokea barua niliyoandika, ukienda wanasema lazima ulipe hili deni! naomba msaada wenu wa mawazo namna ninayoweza kufanya
natanguliza shukrani.
natanguliza shukrani.