Nahodha, Shamuhuna NA SHAHADA ZA MKONONI!!!

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,720
21,778
Habari zaidi!
Nahodha, Shamuhuna kuhitimu OUT
Theopista Nsanzugwanko
Daily News; Saturday,October 25, 2008 @00:03


Waziri Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Shamsi Vuai Nahodha pamoja na Naibu wake, Ali Juma Shamuhuna, ni miongoni mwa wanafunzi takriban 1,000 watakaotunukiwa vyeti vya kuhitimu Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT) katika mahafali yanayofanyika leo.

Viongozi hao wa juu katika SMZ walikuwa miongoni mwa wanafunzi wa chuo hicho wanaohitimu mwaka huu, waliohudhuria mkutano wa 18 wa wanazuoni uliofanyika chuoni Biafra, Dar es Salaam.

Nahodha atatunukiwa Shahada ya Uzamili katika Utawala na Biashara (MBA) wakati Shamuhuna ambaye pia ni Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, atatunukiwa Shahada ya Kwanza ya Uchumi.

Mbali na viongozi hao, pia Mkuu wa Wilaya ya Bahi mkoani Dodoma, Zainabu Kwikage atahitimu Shahada ya Kwanza katika mahafali hayo ya 20 yatakayofanyika katika viwanja vya Biafra Kinondoni. Akizungumza katika mkutano wa jana, Nahodha aliwataka wahitimu wenzake kufanya kazi kwa bidii na kwa utaratibu, ikiwa ni pamoja na kuendelea kusoma masuala mbalimbali.

Alisema ni vigumu kutawala katika nchi zinazoendelea hivyo baada ya kupata cheo hicho cha Waziri Kiongozi, ndipo alipoamua kujiunga na chuo hicho na kuwataka Watanzania kusoma ili kuongeza uelewa wa mambo mbalimbali kila wakati. Aidha, Nahodha aliwaasa Watanzania kutopenda kupata vyeti vya urahisi kwa kutafuta vyeti bandia au kusoma katika vyuo visivyoeleweka, bali wajiunge katika vyuo vinavyotambulika na serikali.
 
Habari zaidi!
Nahodha, Shamuhuna kuhitimu OUT
Theopista Nsanzugwanko
Daily News; Saturday,October 25, 2008 @00:03


Waziri Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Shamsi Vuai Nahodha pamoja na Naibu wake, Ali Juma Shamuhuna, ni miongoni mwa wanafunzi takriban 1,000 watakaotunukiwa vyeti vya kuhitimu Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT) katika mahafali yanayofanyika leo.

Viongozi hao wa juu katika SMZ walikuwa miongoni mwa wanafunzi wa chuo hicho wanaohitimu mwaka huu, waliohudhuria mkutano wa 18 wa wanazuoni uliofanyika chuoni Biafra, Dar es Salaam.

Nahodha atatunukiwa Shahada ya Uzamili katika Utawala na Biashara (MBA) wakati Shamuhuna ambaye pia ni Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, atatunukiwa Shahada ya Kwanza ya Uchumi.

Mbali na viongozi hao, pia Mkuu wa Wilaya ya Bahi mkoani Dodoma, Zainabu Kwikage atahitimu Shahada ya Kwanza katika mahafali hayo ya 20 yatakayofanyika katika viwanja vya Biafra Kinondoni. Akizungumza katika mkutano wa jana, Nahodha aliwataka wahitimu wenzake kufanya kazi kwa bidii na kwa utaratibu, ikiwa ni pamoja na kuendelea kusoma masuala mbalimbali.

Alisema ni vigumu kutawala katika nchi zinazoendelea hivyo baada ya kupata cheo hicho cha Waziri Kiongozi, ndipo alipoamua kujiunga na chuo hicho na kuwataka Watanzania kusoma ili kuongeza uelewa wa mambo mbalimbali kila wakati. Aidha, Nahodha aliwaasa Watanzania kutopenda kupata vyeti vya urahisi kwa kutafuta vyeti bandia au kusoma katika vyuo visivyoeleweka, bali wajiunge katika vyuo vinavyotambulika na serikali.

Nimefurahishwa na maelezo ya NAHODA lakini cha kuliza hapa kwanini kila mara akitakiwa kueleza elimu yake ameipatia wapi na chuo gani au( UNI)gani alisoma huwa hakupo tayari kutueleza cha kushangaza kwanini afiche shada zake kama anazo nakuombeni kwa wale wenye kumuelewa huyu Nahoda watueleze wapi elimu yake ameipatia na vyeti gani amekuwa navyo
 
Mkuu unaposema shahada za mkononi una maana kuwa ni za kupewa tu na hawastahiki kupata na hazina viwango?
 
Wengi mnakiona OUT kama chuo cha kilaini........hzo shahada ni halali au ulitaka wasome Udsm
 
Nimefurahishwa na maelezo ya NAHODA lakini cha kuliza hapa kwanini kila mara akitakiwa kueleza elimu yake ameipatia wapi na chuo gani au( UNI)gani alisoma huwa hakupo tayari kutueleza cha kushangaza kwanini afiche shada zake kama anazo nakuombeni kwa wale wenye kumuelewa huyu Nahoda watueleze wapi elimu yake ameipatia na vyeti gani amekuwa navyo
 
Nimefurahishwa na maelezo ya NAHODA lakini cha kuliza hapa kwanini kila mara akitakiwa kueleza elimu yake ameipatia wapi na chuo gani au( UNI)gani alisoma huwa hakupo tayari kutueleza cha kushangaza kwanini afiche shada zake kama anazo nakuombeni kwa wale wenye kumuelewa huyu Nahoda watueleze wapi elimu yake ameipatia na vyeti gani amekuwa navyo
Chuo cha usimamizi wa fedha IFM
 
Kuna katabia cha waliopita UD kujiona na kujisikia chuo chao ndio superior na vyuo vingine vyote ni vya vilaza.
OUT in itegrity. Karume alisota sana hapo kupata LL.B na sijui kama hatimaye alipata. Huu ni uthibitisho kuwa OUT ni chuo makini. Hivyo hiyo MBA ya Nahodha itakuwa ya ukweli. Hii haina maana viongozi hawana degree fake zipo.
 
Kuna katabia cha waliopita UD kujiona na kujisikia chuo chao ndio superior na vyuo vingine vyote ni vya vilaza.
OUT in itegrity. Karume alisota sana hapo kupata LL.B na sijui kama hatimaye alipata. Huu ni uthibitisho kuwa OUT ni chuo makini. Hivyo hiyo MBA ya Nahodha itakuwa ya ukweli. Hii haina maana viongozi hawana degree fake zipo.

Tuache utani ..kupita UD kuna 'raha' yake ..
 
Tuache utani ..kupita UD kuna 'raha' yake ..


Raha ipi (zipi) unazozungumzia mwenzetu??? Mie naona ni kero tupu. Sababu ninazo
1. Wanafunzi wanne mpaka sita wanalala kwenye chumba cha watu 2
2.Vyoo vya pale karibu na semina rooms sijui mnaita (ATB or ATA) vinanuka kinyesi sijui nifananishe na kitu gani!! Mahali tunapopika wasomi!! Aibu tupu.
3.Wanafunzi wanakaa chini kwenye lecture rooms
4.Wanafunzi wanachungulia kwenye madirisha kwenye seminar rooms
5.Wanafunzi zaidi ya 270 wanahudhuria lecture moja inayofundishwa na lecturer mmoja kwa wakati mmoja!!
5.Huko kwenye mabweni ndio usiseme. Wanafunzi wote ni "mama lishe" siku hizi!! Kila harufu ya chakula utanusa huko, biriani, kauzu, maharagwe, kisamvu, matembele, nyanya chungu, kitimoto, etc.
6.Kusoma hawasomi. Kazi kutegemea madesa tu.
7.Maprofesa wamefungua baa huko saveyi, wala hawana muda kuwapa elimu wanafunzi wao. Muda wanaotumia kuhudumia nguruwe ni mara 3 zaidi ya muda wanaotumia kuingia kwenye lecture room. Muda wanaotumia kufukuzia consultancies ni mara 4 zaidi ya muda wanaotumia kusoma "essays" za wanafunzi.


Hizo ndizo raha??? Ama kweli ukistaajabu ya musa utaona ya firauni.
 
Raha ipi (zipi) unazozungumzia mwenzetu??? Mie naona ni kero tupu. Sababu ninazo
1. Wanafunzi wanne mpaka sita wanalala kwenye chumba cha watu 2
2.Vyoo vya pale karibu na semina rooms sijui mnaita (ATB or ATA) vinanuka kinyesi sijui nifananishe na kitu gani!! Mahali tunapopika wasomi!! Aibu tupu.
3.Wanafunzi wanakaa chini kwenye lecture rooms
4.Wanafunzi wanachungulia kwenye madirisha kwenye seminar rooms
5.Wanafunzi zaidi ya 270 wanahudhuria lecture moja inayofundishwa na lecturer mmoja kwa wakati mmoja!!
5.Huko kwenye mabweni ndio usiseme. Wanafunzi wote ni "mama lishe" siku hizi!! Kila harufu ya chakula utanusa huko, biriani, kauzu, maharagwe, kisamvu, matembele, nyanya chungu, kitimoto, etc.
6.Kusoma hawasomi. Kazi kutegemea madesa tu.
7.Maprofesa wamefungua baa huko saveyi, wala hawana muda kuwapa elimu wanafunzi wao. Muda wanaotumia kuhudumia nguruwe ni mara 3 zaidi ya muda wanaotumia kuingia kwenye lecture room. Muda wanaotumia kufukuzia consultancies ni mara 4 zaidi ya muda wanaotumia kusoma "essays" za wanafunzi.


Hizo ndizo raha??? Ama kweli ukistaajabu ya musa utaona ya firauni.

...kupita UD kuna 'raha' yake

Sijui kama umenielewa.


Asante kwa ushirikiano, hata hivyo.
 
Ukweli haufichiki OUT ni dhaifu saana hata ukipitia safu ya waalimu wake 90% ni dhaifu ambao hawana qualification za kufundisha chuo kikuu. actually ukiitazama saana ni kule kule tunarudi kama kwenye UPE amayo kirefu chake pevu ni UALIMU PASIPO ELIMU. Kama KARUME ansoma na kufuzu then mtu yeyote anaweza kufuzu.
 
Hivi hawa wanasiasa mbona wanakimbilia OUT kwa nini wasijisajiri hata Part time mlimani au IFM au Mzumbe? wata disco asubuhisubuhi tu Believe it or not kazi zao zinaandikwa na kuresearchiwa na wasaidizi wao! ka-kiroboto kamenieleza. katika dissertation badala ya kukusanya they should present hadhani na washonwe maswali juu ya kazi zao(dissertations sio siasa) Utaona madudu yatakayotokea!!! kwi kwi
 
Mimi nadhani hata hiyo MBA is highly questionable inaweza kuwa ya kisiasa, maana hata members wa faculty ya FBM pale OUT wanadai hakuwa mwanafunzi wao labda kama alikuwa anatumia jina lingine
 
Habari zaidi!
Nahodha, Shamuhuna kuhitimu OUT
Theopista Nsanzugwanko
Daily News; Saturday,October 25, 2008 @00:03


Waziri Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Shamsi Vuai Nahodha pamoja na Naibu wake, Ali Juma Shamuhuna, ni miongoni mwa wanafunzi takriban 1,000 watakaotunukiwa vyeti vya kuhitimu Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT) katika mahafali yanayofanyika leo.

Viongozi hao wa juu katika SMZ walikuwa miongoni mwa wanafunzi wa chuo hicho wanaohitimu mwaka huu, waliohudhuria mkutano wa 18 wa wanazuoni uliofanyika chuoni Biafra, Dar es Salaam.

Nahodha atatunukiwa Shahada ya Uzamili katika Utawala na Biashara (MBA) wakati Shamuhuna ambaye pia ni Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, atatunukiwa Shahada ya Kwanza ya Uchumi.

Mbali na viongozi hao, pia Mkuu wa Wilaya ya Bahi mkoani Dodoma, Zainabu Kwikage atahitimu Shahada ya Kwanza katika mahafali hayo ya 20 yatakayofanyika katika viwanja vya Biafra Kinondoni. Akizungumza katika mkutano wa jana, Nahodha aliwataka wahitimu wenzake kufanya kazi kwa bidii na kwa utaratibu, ikiwa ni pamoja na kuendelea kusoma masuala mbalimbali.

Alisema ni vigumu kutawala katika nchi zinazoendelea hivyo baada ya kupata cheo hicho cha Waziri Kiongozi, ndipo alipoamua kujiunga na chuo hicho na kuwataka Watanzania kusoma ili kuongeza uelewa wa mambo mbalimbali kila wakati. Aidha, Nahodha aliwaasa Watanzania kutopenda kupata vyeti vya urahisi kwa kutafuta vyeti bandia au kusoma katika vyuo visivyoeleweka, bali wajiunge katika vyuo vinavyotambulika na serikali.

Ali juma shamuhuna hatukumuona kwani kumpa shahada kama hiyo ni kumpaka mafuta kwa nyuma ya chupa Nahoda kupewa haistajabishi hakuna asiejuwa kinachoendea (Mzungu wa ray wangu kalala wapi)USIMLAUMU DOBI KANIKI NI RANGI YAKE
 
Back
Top Bottom