Msukuma Original
JF-Expert Member
- Oct 2, 2018
- 928
- 3,330
Nina imani hili jukwaa linasomwa na watu walio karibu na rais au hata rais mwenyewe. Nawaomba wanifikishie ombi langu kwa mheshimiwa rais wangu.
Nafikiri sio mimi peke yangu, nadhani kuna watanzania wengi wenye mawazo bora kabisa na ni wasomi waliobobea kwenye nyanja tofauti na wangependa kuiona nchi inapaa kupitia taalama zao, lakini kutokana na kutokuwa na majina au umaarufu hawawezi kuonekana kwa mheshimiwa.
Badala yake wanaoteuliwa ni makada wa CCM na maprofesa wanaojulikana. Kwa niaba ya wachumi wenzangu na wasomi wengine ambao hatujulikani naomba kuchukua nafasi hii kumuomba mheshimiwa rais anipe nafasi ya kumsaidia katika jitihada zake za kuipaisha hii nchi.
Kusema kweli rais anafanya mapinduzi makubwa sana ya kiuchumi hivyo anahitaji watu sahihi kuwa karibu yake kumsaidia mawazo mengine mazuri ya kuipeleka Tanzania sehemu anayoitaka. Mimi ni mtaalamu wa uchumi na ni mtaalamu wa fedha wa kiwango cha juu kabisa. Elimu yangu nimeipata nje ya mipaka ya Tanzania.
Hivyo mbali na elimu yangu pia nina exposure na practical experience ya nchi zilioendelea. Hivyo mchango wangu utakuwa wa kipractical zaidi kuliko kinadharia.
Naweza kuyaelezea mawazo yangu hapa na namna nitakavyomsaidia rais kuipaisha hii nchi lakini naona si jambo jema kuanika kila kitu hapa maana mambo ya kiuchumi ni mapana sana.
Naomba niishie hapa. Wahusika tafadhalini sana fikisheni ombi langu kwa mheshimiwa. Wengine hatuna majina ya kuonekana ili tuteuliwe, tunaweza kufa na ujuzi wetu.
Nafikiri sio mimi peke yangu, nadhani kuna watanzania wengi wenye mawazo bora kabisa na ni wasomi waliobobea kwenye nyanja tofauti na wangependa kuiona nchi inapaa kupitia taalama zao, lakini kutokana na kutokuwa na majina au umaarufu hawawezi kuonekana kwa mheshimiwa.
Badala yake wanaoteuliwa ni makada wa CCM na maprofesa wanaojulikana. Kwa niaba ya wachumi wenzangu na wasomi wengine ambao hatujulikani naomba kuchukua nafasi hii kumuomba mheshimiwa rais anipe nafasi ya kumsaidia katika jitihada zake za kuipaisha hii nchi.
Kusema kweli rais anafanya mapinduzi makubwa sana ya kiuchumi hivyo anahitaji watu sahihi kuwa karibu yake kumsaidia mawazo mengine mazuri ya kuipeleka Tanzania sehemu anayoitaka. Mimi ni mtaalamu wa uchumi na ni mtaalamu wa fedha wa kiwango cha juu kabisa. Elimu yangu nimeipata nje ya mipaka ya Tanzania.
Hivyo mbali na elimu yangu pia nina exposure na practical experience ya nchi zilioendelea. Hivyo mchango wangu utakuwa wa kipractical zaidi kuliko kinadharia.
Naweza kuyaelezea mawazo yangu hapa na namna nitakavyomsaidia rais kuipaisha hii nchi lakini naona si jambo jema kuanika kila kitu hapa maana mambo ya kiuchumi ni mapana sana.
Naomba niishie hapa. Wahusika tafadhalini sana fikisheni ombi langu kwa mheshimiwa. Wengine hatuna majina ya kuonekana ili tuteuliwe, tunaweza kufa na ujuzi wetu.