akili yako haifanani na mtu mwenye wajukuu labda wewe ni mjukuu jaribu ku edit umejisaau
iki kitoto niaje,we ndo uedit akili yako, soma text uelewe.Kina-pu akili,af kinajaza nnya kichwani! Tapeli mkubwa we,ndomana Ka-shotiii..
karibu Saint Gasper hotel ushuhudie nikizungumza na *** kuhusu hili jambo,kama upo mwanza saa 1 nipo hapo kuzungumza na mwinine
najua unaniwekea bifu ila mimi hata kinyongo sina ndo maana nakukaribisha,hata msos wa mchana au jion ntakununulia uje ushuhudie
we dis tu lakini dili zinatiki
Lizzy samahan, nakupa heshima yako.
Lakin najua mvulana ni mwanaume mdogo a.k.a serengeti boy, wenyewe wanasema hawa Mabaloteli ni mafundi kweli kweli!
Hhehehe. . .AHSANTE ila mvulana ni mvulana tu bana mpaka pale atakapokuwa mwanaume.
Haya utakosa mautundu we ng'ang'ana tu na huyo mwanume wako!
we mkaka unajitambua kweli ndugu yangu
umesema wewe umelelewa na mama na hujawahi kumjua baba yako....
binafsi niliamin kuwa ungetamani sana ndani ya moyo wako mwanao asije kuwa kama wewe,ungetamani mwanao apate malezi ya wazazi wote wawili coz naamin utakubaliana na mimi kuwa pamoja na juhud zote alizofanya mama kukutimizia uliyoyahitaji, still ulitaman ungepata na malezi ya baba yako.....
sikupata bahat ya kulelewa na baba, nimelelewa na mama tu, hiyo ilinifanya nijiapize na niwe makini sana nyendo zangu ili nihakikishe watoto nitakaowazaa wanapata malezi ya pande zote mbili coz najua adha ya kukosa mapenz ya pande zote mbili......
FIkiria tena na tena....,binafsi naona kama hujafikiria vya kutosha kuhusu hili, nahisi unalifanya under pressure.............
ushauri mzur,hili laimeshapita na karibu dili linakubali na sio mtu wa kunizalia bali wamejitokeza wanaotaka ndoa so nisikilizie ikiwa ndoa ntaku pm upate kad.nimeshaongea na mmoja leo dom kesho nipo mwanza kuongea na mwingine,so mtoto ambaye Ntampata atapata malez ya pande mbili
Polen na majukumu ya kila siku
mimi ni kijana wa miaka 23 na bado nipo kimasomo katika chuo flani cha elimu ya juu ila nahitaji kuwa na mtoto m1 na hii nikutokana na shinikizo la mama kuniambia anahitaj mtoto kutoka kwangu kabla hajafa kwa kuwa mimi ndo mtoto wake wa pekee wakiume,hivyo kwa kumridhisha mama nikaona nitafute mwanamke atakayenizalia huyo mtoto kwasababu mchumba niliyekua naye na yeye ni mwanafunzi mwenzangu na amekataa kubeba mimba mpaka amalize masomo na ndo kwanza kaanza mwaka huu masomo ya udactar yatakayochukua miaka 5 na huu muda siwez kuusubiri,tuliposhindwa kuelewana ikabidi tusitishe mahusiano na kubaki kama marafiki tu though hakuwa tayar na ameridhia nitafute mwanamke atakaekubal kubeba mimba
MASHARTI YA MKATABA
1.nitakuwa tayar kupima HIV na yeye awe tayar
2.tutakubaliana kiasi nitakacho mlipa
3.tutakubaliana muda atakao kaa na mtoto baada ya kujifungua
4.ni lazima kupima DNA mtoto atakapozaliwa kudhibitisha uhalal wa mtoto
5.kama huyo binti atakuwa tayar kuish na mimi baada ya kujifungua kama mzaz mwenzie(baada ya mimi kumaliza masomo yangu)itaruhusiwa na mkataba utaeleza
6.Nitaudumia ujauzito kwanzia mwez wa kwanza mpaka ntakapomchukua mtoto
7.Atakua na uhuru wa kuja kumsalimia mtoto wakati wote
SIFA ZA MWANAMKE HUYO
1.Asiwe mke wa mtu
2.Awe na umri kuanzia miaka 18 - 25
3.Awe mweupe au maji ya kunde na asiwe mwembamba sana
kama upo tayar ni pm tuwasiliane
4.Kielimu awe amemaliza at least form 4
5.Asiwe mlevi na mvuta sigara
6.Awe hajawahi kuwa na toto hapo kabla
NOTE:
MKATABA UTAKUA KATI YA MIMI NA YEYE NA UTALINDA HAKI ZA KILA MMOJA.
Nipo serious
Pia unaweza ukaniuliza swali lolote au kunishauri
NAWASILISHA