Jinsi Habari Muhimu za Tanzania Zinavyopatikana kwa Bei Kubwa

Game Theory

JF-Expert Member
Sep 5, 2006
8,545
833
Kwa kuwa huwa nascan sana vyombo vya habari ambavyo vinaandika kuhusu TZ lakini hawa jamaa wa INDIAN OCEAN NEWSLETTER wananiacha hoi maana wao wanachaji kwa article badala ya subscription ya mwaka au miezi sita

sasa hivi wana "NYETI" kuhusu JK na Serikali lakini nashindwa ku access hizo habari kwani jamaa wanauza article ya maneno 180 kwa dola 8 sasa ndio jamaa wanasika kwa kuwa ma investigative journalists ambao ni credible lakini itabidi wana JF tusaidiane katika kupata news toka kwa hawa jamaa wa ION

Infact natamani na sisi humu JF tukawa kama hawa jamaa wa ION badala ya kuendeleza ubishi wa personalities wa CCM v/s CHADEMA wakati NYETI zinatupita hivi hivi


MFANO KUNA NEWS HIZI AMBAZO NADHANI ZINAUMUHIMU WA KUJADILI:

What's Zanzibar's Share?

Tanzania has issued a call for bids from consultants to help it find the right formula to share out oil revenue between the federal government and the regional administration of Zanzibar.(...).

President Kikwete's close guard

President Jakaya Kikwete has progressively surrounded himself with a team of loyal supporters: apparatchiks from the government party Chama cha Mapinduzi (CCM), former colleagues from when he was minister for foreign affairs, or journalists that he took with him on his election campaign in 2005.(...).


Power struggle to supply airport fuel
In 2005 the Tanzanian authorities wanted to open the market for supplying aviation fuel at Dar es-Salaam airport to competition, up to then a monopoly held by British Petroleum (BP).(...).


A leg up for Hillal Hamad Hillal

A 2,900 square metre plot of land in the commercial centre of Dar es-Salaam has been sold for the sum of 440 million shillings (€248,000) to the head of the Tanzanian mining company El Hillal Minerals Ltd (EHM), although its value had been estimated at
1.(...).

The Kikwete dynasty in the CCM
President Jakaya Kikwete will naturally be present at the Chama cha Mapinduzi (CCM) party conference because he is the chairman of the governing party.(...).

Benjamin Mkapa's Portfolio
With his wife Anna Mkapa , former president Benjamin Mkapa discreetly turned his hand to business dealings when he was in office between 1995-2005.(...).


Joseph Kahama

An adviser to the Tanzania Chamber of Energy and Minerals , Joseph Kahama , has been named vice president of the Canadian firm Tanzanian Royalty Exploration Corp .(...).

Africa Intelligence: exclusive news on Africa
 
Nadhani bora tusikilize maoni ya wengi then we will take it from there.

Kwa kuanza nadhani itabidi Admin awaban ma LURKERS ambao wamejiandikisha halafu hawajachangia kitu.Hiyo itakuwa ni njia nzuri ya kupata revenue. Itabidi wajiregister tena na kwa kulipa DOLA 10 ndio watapata full access ya JF otherwise wapewe limited access ya kuona Udaku na labda nyepesi nyepesi tu


Ndio maana ya desperate measures hiyo lakini hizo pesa inamaana JF inaweza ikawa na unlimited access ya articles toka Indian Ocean Newsletter

Mfano hiyo ya Mtoto wa KAHAMA naamini itakuwa very interesting kusoma lakini kwa kuanza nadhani bora tusikilize maoni ya wengi

 
Kama wewe ni mtu mvivu wa kufuatilia nyeti (najua wewe siyo), basi hao jamaa ni kama shortcut! Huwa wananusanusa vijihabari na kuunganisha na nyingine na kupata moja nzuri au inayovutia!

Magazeti ya Thisday, Kulikoni na Mwanahalisi... hata Mwananchi na Tanzania Daima huwa na habari kama za hao jamaa.

Wao huzichambua zaidi na kutafuta vyanzo vingine kidogo. Kwa hiyo, huwa hawana haraka ya kuandika habari! Ndio maana zao huonekana kuaminika zaidi!

Sasa, kwa bei hiyo, watawapata mabalozi, waandishi wa nje, mashushushu wa nje, ngo zenye maslahi ya kisiasa, nk! Hiyo bei ni kubwa! Labda kwa sababu nao wanazinunua!
 
Game,

Nafikiri kama nimeelewa ni kwamba unalipa euro 250,au £175 au 300 US Dollar kwa mwaka baada ya kuchagua "subscription" yako kwa channel(nchi husika).

Nenda sehemu ya "Subscription" na usome hayo.

Hata hivo pi nafikiri habari hizi ni very sensitive kama za taasisi zingine kama "Africa-Confidential" ambao nao huitaji malipo kwa msomaji na sidhani kama wataruhusu kuzifuja mahala kwingine.

Sasa nafikiri ni "sensitive" kwa sababu wanaozisoma ni watu wenye "interest" ya wizi wa mali katika nchi za watu na wale wanaotoa habari walioko Tanzania(na ni waTZ wenzetu) na "source" zao pia wote ni wamoja.

Pia nafikiri wao wanajua kila kitu kuhusu nani atakuwa rais "in advance" na huanza kumfuatilia kwa kutoa biography na "takataka" zingine.

Kwa hio wametengeneza mfumo mzuri wa habari pamoja na database hio ambayo ndio unaiona, lakini makao makuu ni ....Paris!

Lakini nami naunga mkono kwamba tuzidi kungoja maoni zaidi.

Ahsante.
 
..kama we ni mtu mvivu wa kufuatilia nyeti[najua wewe siye],basi hao jamaa ni kama shortcut!

..huwa wananusanusa vijihabari na kuunganisha na nyingine na kupata moja nzuri au inayovutia!

..magazeti ya thisday,kulikoni na mwanahalisi...hata mwananchi na tanzania daima huwa na news kama za hao jamaa.

..wao huzichambua zaidi na kutafuta sources nyingine kidogo. simply huwa hawana haraka ya kuandika habari!ndio maana zao huonekana credible zaidi!

..sasa,kwa bei hiyo watawapata mabalozi,waandishi wa nje,mashushushu wa nje,ngo zenye interest za kisiasa,n.k!

..hiyo bei ni kubwa!maybe kwa kuwa nao wanazinunua!

Lakini nadhani bora wao kuliko KULIKONI na THIS DAY ambao nao huja kunyonya humu JF mwanzoni walikuwa hawasemi source lakini naona hiyo ya BUZWAGI wameamua kusema kuwa hiyo contract ipo humu JF!

nevertheless nadhani kwa wanaotaka kufuatilia PORTFOLIO YA MKAPA wanaweza kufurahia hizo habari kama zitakwepo humu
 
Nilifikiri Mzee Mwanakijiji ndio pekee tu huwa anaomba msaada, kumbe tupo wengi.....Teh Teh TEh teh..................
 
Game,

Nafikiri kama nimeelewa ni kwamba unalipa euro 250,au £175 au 300 US Dollar kwa mwaka baada ya kuchagua "subscription" yako kwa channel(nchi husika).

Nenda sehemu ya "Subscription" na usome hayo.

Hata hivo pi nafikiri habari hizi ni very sensitive kama za taasisi zingine kama "Africa-Confidential" ambao nao huitaji malipo kwa msomaji na sidhani kama wataruhusu kuzifuja mahala kwingine.

Sasa nafikiri ni "sensitive" kwa sababu wanaozisoma ni watu wenye "interest" ya wizi wa mali katika nchi za watu na wale wanaotoa habari walioko Tanzania(na ni waTZ wenzetu) na "source" zao pia wote ni wamoja.

Pia nafikiri wao wanajua kila kitu kuhusu nani atakuwa rais "in advance" na huanza kumfuatilia kwa kutoa biography na "takataka" zingine.

Kwa hio wametengeneza mfumo mzuri wa habari pamoja na database hio ambayo ndio unaiona, lakini makao makuu ni ....Paris!

Lakini nami naunga mkono kwamba tuzidi kungoja maoni zaidi.

Ahsante.


Kuwa sensitive sidhani kama ni sensitive hivyo lakini wao kama ONLINE MAGAZINE au jarida inabidi warudishie expenses zao ndio maaana nika suggest JF wanaweza wakachukua same approach na kwa kuanza kuingiza revenue ni kwa kuwalipisha hawa LURKERS ambao wana kuja kusoma bila kuchangia hiyo dola 10 ambayo itabidi waregister.

JF wanaweza kuendelea na Forum kama kawaida lakini kama kuna mtu akipost article nzima then sidhani kama kuna tatizo. Personally nilishawakuchukua baadhi ya articles zao na nikazipost humu na kwenye TERMS & CONDITIONS zao hawajakataza kuredistrubute

Mfano mimi nina access na contents zaidi ya 100 ambazo nyingi huwa wanataka watu wachangie kupitia kibaruani kwangu lakini hiii ya Indian Ocean na wale Africa confidential hatuja subscribe
 
..hata wao wanaweza kuwa wanazichota humu pia!

..this forum has a lot of info...ila inabidi uchambue kama karanga!
 

Kuwa sensitive sidhani kama ni sensitive hivyo lakini wao kama ONLINE MAGAZINE au jarida inabidi warudishie expenses zao ndio maaana nika suggest JF wanaweza wakachukua same approach na kwa kuanza kuingiza revenue ni kwa kuwalipisha hawa LURKERS ambao wana kuja kusoma bila kuchangia hiyo dola 10 ambayo itabidi waregister.

JF wanaweza kuendelea na Forum kama kawaida lakini kama kuna mtu akipost article nzima then sidhani kama kuna tatizo. Personally nilishawakuchukua baadhi ya articles zao na nikazipost humu na kwenye TERMS & CONDITIONS zao hawajakataza kuredistrubute

Mfano mimi nina access na contents zaidi ya 100 ambazo nyingi huwa wanataka watu wachangie kupitia kibaruani kwangu lakini hiii ya Indian Ocean na wale Africa confidential hatuja subscribe

Nimekupata mkuu
 
jkk.jpg

Picha ya kwanza juu ni ni Rais jakaya kikwete akiwa atk pica ya pamoja na Al Noor Kassimu w pili kutoka kushoto,na wa kwanza kutoka kushoto ni Mrs janet Kahama, wa kwanza kulia ni Sir George Kahama na Mrs Alnoor Kassimu.

SASA KAHAMA JUZI ALIKUWA IKULU NA MUUNGWANA HUKU MWANAE ANAANDIKWA NA JAMAA WA ION ...BTW HUYU KAHAMA KWA NINI WANAMUITA SIR WAKATI SI RAIA WA UK? NA ALIKUWA KNIGHTED NA NANI KWA LIPI ALILOLIFANYA?

Joseph Kahama
An adviser to the Tanzania Chamber of Energy and Minerals , Joseph Kahama , has been named vice president of the Canadian firm Tanzanian Royalty Exploration Corp .(...).
[/QUOTE]
 
its a good idea kuchangia lakini nyie mliopo ughaibuni kumbuka lifi lilivyo tight huku mascan, yaani mtu anajikusanya kweli kweli kupata buku moja ili aingie internet cafe kupata habari au kutoa duku duku lake kwenye JF sasa ikija hiyo la dola 10 sijui itakuwa kwa mwaka au mwezi naona wanachama watazidi kupumbua bila wao kupenda ila hali halisi itawalazimisha. anyway labda iwe hiari kuchangia ili isije kuleta gap btn those who haves and those who have not kama serikali yetu inavyofanya. Nimejaribu kutembelea hiyo web ya www.africaintelligence.com naona imejikita zaidi kufanya biashara ambalo siyo lengo letu hapa JF. anyway tusubiri maoni ya wengine.
 
Nadhani bora tusikilize maoni ya wengi then we will take it from there.

Kwa kuanza nadhani itabidi Admin awaban ma LURKERS ambao wamejiandikisha halafu hawajachangia kitu.Hiyo itakuwa ni njia nzuri ya kupata revenue. Itabidi wajiregister tena na kwa kulipa DOLA 10 ndio watapata full access ya JF otherwise wapewe limited access ya kuona Udaku na labda nyepesi nyepesi tu


Ndio maana ya desperate measures hiyo lakini hizo pesa inamaana JF inaweza ikawa na unlimited access ya articles toka Indian Ocean Newsletter

Mfano hiyo ya Mtoto wa KAHAMA naamini itakuwa very interesting kusoma lakini kwa kuanza nadhani bora tusikilize maoni ya wengi

No kwa maoni yangu binafsi sidhani kama niwazo zuri la kuanza kuchangisha watu hapa JF, kama wewe unataka hizo habari hapa unaweza kuomba watu wakuchangie ukazipata!

Au uliza watu wenye vipesa kidogo wanunue hizo habari na wakaziweka hapa badala ya kuanza kuchangisha watu hapa JF ili pesa ipatikane kulipia newsletters.

haya ni maoni yangu binafsi, uchangiaji na upatikanaji wa habari utakuwa tu kwa wale pesa ingawa unasahau kuwa JF inalenga pia watu walioko nyumbani na kipato cha watz wa kawaida huko ni dola 50 - 100 kwa mwezi mmoja!
 
No kwa maoni yangu binafsi sidhani kama niwazo zuri la kuanza kuchangisha watu hapa JF, kama wewe unataka hizo habari hapa unaweza kuomba watu wakuchangie ukazipata!

Au uliza watu wenye vipesa kidogo wanunue hizo habari na wakaziweka hapa badala ya kuanza kuchangisha watu hapa JF ili pesa ipatikane kulipia newsletters.

haya ni maoni yangu binafsi, uchangiaji na upatikanaji wa habari utakuwa tu kwa wale pesa ingawa unasahau kuwa JF inalenga pia watu walioko nyumbani na kipato cha watz wa kawaida huko ni dola 50 - 100 kwa mwezi mmoja!

Sikatai ndio maana mwanzo nikasema bora tupate mawazo ya wengi. Lakini hiyo haiondoi ukweli kuwa wakati ushafika JF ijiendeshe kama business entity na kusema kweli jamaa hapa hawapati matangazo ya maan maana sidhani kama kuna watu wanaclick hata haya matangazo madogo ya Google lakini mfano kwa muda huu ambao wengi wanalog in kusoma nadhani its about time ikawepo business plan ya jinsi gani JF inaweza kujiendehsa kibiashara/ Members wako wengi na hii inaweza ikaielemea server sasa kufanya marekebisho na mambo mengineyo ya kiufundi nadhani zitahitajika pesa

sasa kama kuna mtu yuko tayari kununua magazeti au kulipa pesa kwa ajili ya starehe singinezo then sidhani kama itakuwa tabu kwa huyo mtu akiambiwa atoe mchango

dola kumi ilikuwa ni wazo tuuu na hiii haikuwalenga wachangiaji wa kila siku bali wale ma DORMANT members ambao kwa jina lingine wanaitwa ma lurkers ambao itabidi uanachama wao ufutwe, na wakitaka kuingia wapewe access ya forum nyingine ya labda michezo lakini hizi main forums kama siasa ni pale mpaka wawe wamelipia



Might sound harsh lakini hebu tuwafikirie wenzetu hawa afterall hii website haiwezi kujiendesha as a forum pekeyake inabidi iwe na Front page ambako akipatikana sponsor hata mmoja wa kununua banners kubwa tatu then nadhani jamaa watakuwa na ahueni kidogo

Suala la kupata news toka kwa ION naona bora niliwidhraw kwani itabidi hiyo iwe ni personal effort lakini nadhani bado wigo ni pana kwa ajili ya kuongeza mawazo zaidi na hii yote ni kuitakia hi website mema ndio maana tuna kuwa na mawazo tofauti
 
its a good idea kuchangia lakini nyie mliopo ughaibuni kumbuka lifi lilivyo tight huku mascan, yaani mtu anajikusanya kweli kweli kupata buku moja ili aingie internet cafe kupata habari au kutoa duku duku lake kwenye JF sasa ikija hiyo la dola 10 sijui itakuwa kwa mwaka au mwezi naona wanachama watazidi kupumbua bila wao kupenda ila hali halisi itawalazimisha. anyway labda iwe hiari kuchangia ili isije kuleta gap btn those who haves and those who have not kama serikali yetu inavyofanya. Nimejaribu kutembelea hiyo web ya www.africaintelligence.com naona imejikita zaidi kufanya biashara ambalo siyo lengo letu hapa JF. anyway tusubiri maoni ya wengine.

sikati mawazo yako lakini ukweli ni kuwa its about time huyu mtoto akatembea mwenyewe na kwa sasa muda wa kumshikilia ushapita

hivi kati ka members zaidi ya 300 ambao kila siku wanalog on kusoma humu ndani hawawezi kulipia hata dola 5?

lakini ni vizuri mawazo ya wengi yanakuja hivyo tuendeleee kupeana mawazo
 
Game Theory unaassume mambo mengi kweli kwenye hili. Tatizo ni kuwa watakaochangia watakuwa ni wale wale ambao wamekuwa wakichangia mambo mengine na wengine wataendelea kufurahia kupitia kwa wengine. Kama tunaamua kuifanya JF ni ya kulipia basi SOTE tulipie hakuna free ride! Nitakuwa wa kwanza kabisa kujiandikisha kwa kulipia.

Tunachoweza kufanya ni kuhakikisha kuwa Forum kuu kama Siasa hapa zinafungwa na wanaoingia ni wale waliojiandikisha na kulipia, kama wanataka kuchangia au la hilo jingine! Na michango hiyo ya kujiandikisha itatumika kuendeshea Forum kwani hadi hivi sasa bado hatuko free as we want to be..

Hata hivyo tatizo la kuchangia ni kuwa italazimisha watu kudisclose their identinty in a certain way na hivyo itaondoa utamu wa forum yenyewe!

Njia nzuri ni wewe mwenyewe kujitolea kununua gazeti hilo kwa matumizi yako binafsi na basi unatumegea megea, vinginevyo watu wachache wanaweza kusaidia.

Learn from me, kuna vitu vingine you better do urself na usingojee wengine!
 
Mzee Theory,

Heshima mbele ndugu yangu, mawazo yako ni mazuri tena sana, lakini JF is bigger than that, yaani hizo info,

Check this out, Mkulu Ditto, alipoua dereva wa dala dala, ilitoka hapa JF, in the next two hours, tulifanya kazi kubwa ya kuwafahamisha wakulu karibu 75% wa bongo, kupitia hii forum kuwa ni kweli na imetokea,

Usije shangaa kuwa hao nao wanakuaja kuchukua vitu vingine hapa, habari za hela za kampeni za Muungwana, na Iran zilikuwa hapa mwezi mmoja kabla gazeti la London, halijasema, I can go on and on,

I am sorry mkuu wangu, JF we are bigger than that, Mkuu Mahita, aliukuta mustakabali wake hapa kuhusu kupumzishwa kwake na Muungwana, kwa kushinikizwa na CC, hapa JF kwanza kabla hajasikia popote pengine,

Again, habari za Kahama, Al-Noor Kassoum, Mama Mkapa, Mama Maria, na Muungwana kukutana majuzi kwenye kuzindua kitabu cha Kassoum, hatukuziona kuwa muhimu ndio maana hatukuziweka hapa, tukaipasia forum moja huko pembeni, ndiko hao walikozichukua, I mean ni kweli kuna some info ambazo hao wakuu wanazo, lakini ni ndogo sana mkuu, na value less kulinganisha hapa JF,

hapa Giladi, kwa kilingala panaitwa Koko-banga na Koko Banga, yaani mwisho na mwanzo wa yote, waziri mmoja wa bongo aliyeshinikizwa kuchungulia hapa, majuzi alilalamika kwa wenziwe kuwa hapa ni addiction, sasa hata kazi inamshinda, maana nataka kuchungulia hapa kuna nini jipya, Tanzania nzima mkuu wangu, magazeti yameurifaaa mkataba wa Buzwagi hapa JF, what else do you want mkuu?

Breaking Newzzz, ziko hapa JF, otherwise sio Newzzz hizo! Wakuu tujifunze kuwa masikini jeuri, kizuri ni chetu tu kingine chochote kinanuka!

Ahsanteni!
 
asante mzee.. ndio maana tunataka kuonesha kuwa unaweza ukallipia lakini kusubiri hadi habari ziandikwe kwa kiingereza inachukua miezi.. wakati wao wanaripoti kuhusu shilingi Bilioni 10 za Karamagi, sisi hiyo mada hapa yaani sijui iko ukurasa wa ngapi... Wakati wao wanasubiri vipakuliwe mezani kule Tanzania, sisi tunavishuhudia vikipikwa hapa!! Kudos mzee..

NB: Nadhani ulimaanisha mzee Mahita siyo Mahundi...
 
FMES

Mkome nyani giladi hapa hapa hakuna kumwonea aibu.
 
lutoa sio kulazimisha, hivyo kama mtachangisha watakaoamua kutoa kutoaka moyoni mwao then waache wafanye hivyo na wasioweza kutoa nao wapate fursa kamili kama ya waliolipa kwa maoni yangu !

again, kutoa ni moyo !
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom