Nahitaji msaada wa kisheria kwa mfanyakazi ambae mkataba wake umesitishwa bila notice ya mwezi mmoja lakini amelipwa mshahara wa mwezi mmoja zaidi

Dec 13, 2012
67
352
Habari zenu wanajamvi.

Naulizia ili kufahamu kwa niaba ya rafiki yangu.

Rafiki yangu alikuwa ni mfanyakazi wa kampuni fulani hapa jijini Dar es Salaam na alikuwa akifanya kazi na hiyo kampuni kwa takriban miaka mitano.

Kwa kawaida kampuni ambayo alikuwa akifanya nayo kazi ilikuwa inawapatia wafanyakazi mkataba wa mwaka mmoja mmoja. Yani kama mfanyakazi ametumikia kampuni kwa miaka kumi, maana yake ni kwamba mfanyakazi huyo amesaini mikataba kumi katika kipindi hicho.

Kwa mwaka 2020 (kabla mripuko wa COVID-19), kampuni iliwapatia wafanyakazi mkataba wa miaka miwili kila mfanyakazi, ila kutokana na hofu ya mripuko wa COVID-19 kampuni iliamua kuwapa baadhi ya wafanyakazi likizo ya mwezi mmoja (Annual leave) ili kupunguza msongamano wa wafanyakazi ofisini hapo.

Bila kutarajia, baada ya wafanyakazi kumaliza likizo, kampuni ikaamua kuwaitisha kikao baadhi ya wafanyakazi wao na kuwapatia barua za kusitisha mikataba yao huku wakiwalipa mshahara wa mwezi mmoja baada ya mwezi wa kusitisha mikataba yao. Yani kama mfanyakazi alikwenda likizo kuanzia Tarehe 1 Aprili na kuripoti kazini tarehe 29 Mei, alilipwa mshahara wake wa mwezi Aprili (ambao alikuwa likizo, kisha baada ya kupatiwa taarifa ya kusitishwa kwa mkataba wake alipatiwa mshahara wa mwezi Mei).

Naomba msaada, je hapo mfanyakazi hawezi kisheria kudai malipo ya mkataba wake kuwa terminated bila ya kupatiwa notice?
Na kama alipatiwa mshahara wa mwezi mmoja zaidi, ni halali kuvunjwa kwa mkataba wa kazi bila kupatiwa notice?
 
Kwa mujibu wa sheria za ajira na mahusiano kazini ya mwaka 2004 na kanuni zake za mwaka 2007 nikihusishanisha na ulichokiandika nitafanua kwa uelewa wangu mdogo na mdau ataongezea pale ntakapo pungukiwa tunaanza kama hivi

Ni kosa kisheria kumfukuza mfanyakazi akiwa yupo kipindi cha likizo sasa hapa kampuni ilichokifanya ikasuburi mumalize likizo ndipo ifanye mchakato huo hapo walikuwa sahihi

Katika sababu 4 za kusitisha mkataba wamfanyakazi kwa mujibu wa sheria na kanuni za ajira ni kama ifutavyo

1. mwenendo mbaya 2. kutohitajika 3. kukosa uwezo 4. Sababunza kiundeshaji au mahitaji ya kiundeshaji , Kupunguza idadi ya watu * retrenchment au operation requirment

Muhimu: mkataba wa muda maalumu hukoma wenyewe pale muda wake unapofika mwisho na pia mkataba wa kazi maalumu nao hukoma pale kazi inapofika mwisho

Sasa basi umesema baada ya kurudi likizo kiliitishwa kikao kwa mujibu wa taratibu hapa hawa jamaa wenye kampuni walikuwa wanafanya kitu kinaitwa operation requirment maana yake kikao husika lazima kiliezea kwanini kinahitaji kupunguza wafanyakazi sasa basi nin haki za muhimu

1. likizo hii naona ililipwa kwa mujibu wa maelezo husika

2. Mshahara wa mwezi husika kabla ya zoezi kufanyika

3 Notes ya siku 28 kwa maelezo yako hicho sijakiona

4. kama unamalimbikizo yoyote ya malipo ya siku za nyuma kabla ya zoezi husika

5 Kiinua mgongo hii ni mshahara wa siku moja kwa siku saba jumla ya miaka uliyotumikia angalau ianze mwaka na isizidi miaka 10

6. Cheti cha utumishi

Nazan taratibu zinamapungufu kidogo, ila pia ni kijiridhisha baada ya kupewa hayo malipo walipewa barua zikiwa na kichwa kipi cha habari kutoka kwa kampuni. ile barua ya mwisho ndio itaonesha kitu ila wapo sahihi kwa hii kwa hatua zote kipengele cha malipo tu nazan ndio unatoa ulakini wa mlolongo kuonekana ni batili
 
Mwajiri yupo sahihi kama alikuachisha kazi kisha akakulipa mshahara wa mwezi mmoja ambao hukuufanyia kazi.

Kwa mujibu wa sheria za ajira na mahusiano kazini ya mwaka 2004 inampa ruhusa mwajiriwa au mwajiri kutoa notice ya mwezi mmoja ya kusudio la kuacha kazi/ kuachishwa kazi kisha utalipwa mshahara wako. Au upewe taarifa ya kuachishwa kazi 24hrs na kisha ulipwe mshara wa mwezi mmoja, au mwajiriwa ukiacha kazi kwa notice ya 24hrs utalazimika kumlipa mwajiri wako fedha zenye thamani ya mshahara wako wa mwezi mmoja.

Stahiki nyingine utakazolipwa hutegemea kama hiyo kampuni ilikuwa na mkataba wa hali bora na chama cha wafanyakazi mfano Tuico ndio inahusika na wafanyakazi wa viwandani.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom