Nahitaji msaada wa kisaikolojia

Akotia

JF-Expert Member
Dec 16, 2016
455
1,069
Habari wanajukwaa?

Kwa umri nina miaka 24, kama kichwa cha habari kinavojieleza matatizo yangu yalianza baada ya kumaliza form 4 2010.

Kipindi namaliza form 4 bado niko innocent and pure, sijawahi kuwa hata na gf wala sikuwahi kufanya ngono nikaajingiza katika janga la mitandao ya kijamii kutafuta mwanamke. Nilianza na mtandao wa eskimi ambao huo huo uliniletea balaa hili.

Nikiwa nishapata girls wawili watatu wa kuchat nao na kupigiana simu ila kuonana nao ilikua mbinde maana nlikua sina kitu, kukawa na mshkaji mmoja pia nachat nae huyo mshikaji akaanza kuniletea vishawishi kuhusu mambo ya kumla goti. Jamaa alitumia ushawishi wa hali ya juu kwa kuchat na mimi kunifanya niweze kutamani kumla goti bila hata kuonana, huku mazoea na wale girls yakapungua mi nikawa nachat na mshkaji daily.

Siku ya kwanza tulionana Morroco kwenye burger, jamaa ni shombeshombe umri kwenye 30s alikuja na gari. Baada ya kula burger na juisi nikaingia kwenye gari mpaka kwenye apartment yake Upanga, tukiwa njiani aliweza kunichezea nyeti zangu na kunitia mshawasha na baada ya kuingia huko ndani ndo ikawa siku yangu ya kwanza, kuzini, kula goti na kuingia katika dhambi kubwa kabisa.

Toka siku hiyo mshkaji ndo akawa kama mwanamke wangu, kwa kutumia ushawishi wake wa mali na utoto wangu alizidi kunitumia kwa kuniita kila akijiskia na kunifanyisha vitendo vichafu, nilienjoy sana pamoja na kusahau kabisa kuhusu wanawake na kuwa homosexual completely.

Baada ya matokeo kutoka na kuchaguliwa kuendelea A-level shule fulani hivi ya boarding, mawasiliano yalikata mimi na mshkaji kwakuwa nilikua sina simu ila kipindi cha likizo ilikua kama kawa. Tuliendelea na tabia hiyo chafu tena kwa ufanisi zaidi pale nliporudi Dar kuendelea na chuo hapo ndo nikahamia kwake kabisa tena na kujisahau kama mimi nimeumbwa kwa ajili ya mwanamke nikawa hata nkicheki porno basi ni za gays. Kwakuwa mshkaji pia alikua anafanya siri na huwezi kumjua kwa sura basi mambo yetu yakawa chinichini bila kujulikana.

Mpaka mwaka jana Mungu alipoamua kuniadhibu, chuo nlifeli nikashindwa kuendelea, rafiki wangu wa karibu alinistukia na akanitenga na kuntangazia, wazazi hawajui ila wamenichukia sana kwa kufeli chuo, mambo yangu yote yalikata nikawa nimefulia sina hata mia. Cha kusikitisha zaidi ni huyo mshkaji alieniiingiza kwenye haya yote alifariki kwa ajali mwaka jana pia, baada ya hayo yote nikaamua kumrudia Allah na kutubu na kulia sana na kujuta sana hatimaye mwaka huu nikapata kazi ya kujishikiza.

Tatizo nililonalo sasa hivi ni kuwa nimeshaathirika na uhomosexual. Nikiwaza chochote kuhusu ngono nawaza kumla mwanaume mwenzangu sababu sina memory ya kudo na msichana na kwa wasichana kusema kweli ni domo zege na wala sina mpango nao.

Nahitaji msaada niweze usahau kabisa uhomosexual na kuwa pure na niwe kama wanaume wa kawaida. Nahitaji msaada wenu wakuu sitaki nife mchafu.

Asanteni sana.
 
Duuh 2010-2015. Mkuu unahitaji msaada wa kisaikolojia. Maana haya mambo umeyaingia kwa gia zote,alafu umeyaingia vibaya.

Anyway,ngoja waje na wengine tuone wanasemaje.
 
pole sana mkuu...!

kwanza nakupongeza kwa kuonesha nia ya kuachana na homosexual..

Pili usijickie wa tofauti sana kuhusu kushindwa kujenga mazungumzo na wadada.
Hata madomo zege ambao huo mchezo hawajawahi kuucheza wapo pia,

Napenda nikushauri jambo moja kwanza,
Kabla ya kuanzisha mahusiano na binti yeyote.. Anza kutengeneza mazingira ya kuwazoea wadada,
Tengeneza marafiki wengi iwezekanavyo ambao mtakuwa mnabadilishana mawazo mara kwa mara,
Ukishakuwa na marafiki wengi wa kike hapo hautakuwa na woga wa kuzungumza na msichana tena.
Suala la mahusiano litakuja lenyewe tu, wala hata hautatumia nguvu nyingi.. Utakuwa una uhuru wakueleza hisia zako kirahisi kuliko saivi.

Nakutakia sikukuu njema..
 
Bwana anakuhitaji kwa kazi yake, tubu kisha omba Bwana akuondolee roho mchafu wa ufiraji ili uwe huru na kuwa na hisia juu ya jinsia ya kike tu.
 
pole sana mkuu...!

kwanza nakupongeza kwa kuonesha nia ya kuachana na homosexual..

Pili usijickie wa tofauti sana kuhusu kushindwa kujenga mazungumzo na wadada.
Hata madomo zege ambao huo mchezo hawajawahi kuucheza wapo pia,

Napenda nikushauri jambo moja kwanza,
Kabla ya kuanzisha mahusiano na binti yeyote.. Anza kutengeneza mazingira ya kuwazoea wadada,
Tengeneza marafiki wengi iwezekanavyo ambao mtakuwa mnabadilishana mawazo mara kwa mara,
Ukishakuwa na marafiki wengi wa kike hapo hautakuwa na woga wa kuzungumza na msichana tena.
Suala la mahusiano litakuja lenyewe tu, wala hata hautatumia nguvu nyingi.. Utakuwa una uhuru wakueleza hisia zako kirahisi kuliko saivi.

Nakutakia sikukuu njema..
Nashkuru Sana kwa ushauri wako.
 
Hongera sana. ..Kaa karibu na MOLA wako. ..sali sana maana amekutoa mbali na inaonekana hapendi ufanye mchezo huo ndiyo maana akamwangamiza mbaya wako. ..nyenyekea chini ya mkono wa MOLA naye atakupa nguvu ya kuachana na tabia hiyo na mawazo pia. ..usirudi nyuma lisije kupata jambo baya zaidi. ..ubarikiwe
 
Hongera sana. ..Kaa karibu na MOLA wako. ..sali sana maana amekutoa mbali na inaonekana hapendi ufanye mchezo huo ndiyo maana akamwangamiza mbaya wako. ..nyenyekea chini ya mkono wa MOLA naye atakupa nguvu ya kuachana na tabia hiyo na mawazo pia. ..usirudi nyuma lisije kupata jambo baya zaidi. ..ubarikiwe
Hata Mimi naamini mungu ameniokoa nisije haribikiwa zaidi,na namuomba asinirudishe Tena licha ya majaribu
 
Ukila nyama ya mtu utaendelea kula tu..ht ukioa binti utaendelea tu na shetani huyo...hapo Malaika hawakai wanakukimbia sasa ...pole sana..
 
Ukila nyama ya mtu utaendelea kula tu..ht ukioa binti utaendelea tu na shetani huyo...hapo Malaika hawakai wanakukimbia sasa ...pole sana..
Mungu azidi kuniepusha na majribu na mitihani ya sheytwan
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom