Nahitaji mkopo ninunue bajaji

Bobdon

Senior Member
Jun 8, 2017
197
287
Habari za jioni wakuu.

Kama mada inavyojieleza hapo juu. Nahitaji kukopeshwa hela ninunue bajaji ili ipige kazi hapa mjini(Dar es salaam).Nitapambana kila mwezi niwe narudisha laki 600,000/-, Hivyo ndani ya mwaka mmoja nitakuwa nimemaliza deni lote.

Katika machakato wa kupambana kurejesha hiyo hela itakuwa kama ilivyoelekezwa hapa chini:

Kwa mwezi itakuwa:

150000×4 (weeks)= Tshs 600000/-

Kwa mwaka itakuwa hivi:

600000× 12 (months)= Tshs 7,200,000/-

Therefore, ndani ya mwaka mmoja nitakuwa nimekamilisha huo mkataba kwa kulipa deni lote ambalo ni laki 7,000,000( Principal amount) plus agreeable interest according to our agreement.

Pia baada ya kupata hiyo bajaji naamini itasaidia kuanzisha biashara ndogo ndogo kama,

a) Biashara ya kuuza mboga mboga
b) Biashara ya matunda
c) Mgahawa wa kuuza supu ya pweza na vyakula vingine na,
d) Banda la chips .

Napenda sana niwe tajiri mkubwa sana sema hela inakuwa kikwazo kwa upande wangu.

Nimewasilisha!

NOTE: Kuna marekebisho kidogo yamefanyika!

 
Habari za jioni wakuu.

Kama mada inavyojieleza hapo juu. Nahitaji kukopeshwa hela ninunue bajaji ili ipige kazi hapa mjini(Dar es salaam). Nitapambana kila wiki niwe narudisha elfu 40 mpaka mkopo utakapoisha.

Pia baada ya kupata hiyo bajaji naamini itasaidia kuanzisha biashara ndogo ndogo kama,

a) Biashara ya kuuza mboga mboga
b) Biashara ya matunda
c) Mgahawa wa kuuza supu ya pweza na vyakula vingine na,
d) Banda la chips .

Napenda sana niwe tajiri mkubwa sana sema hela inakuwa kikwazo kwa upande wangu.

Nimewasilisha!
Nenda pale shinyanga emporium ltd . wanatoa Mkopo wa bajaj.
 
Utaweka nini kama dhamana ya huo mkopo unao hitaji?
Dhamana itakuwa ni bajaji nitakayonunua Mkuu.

Hivyo katika mkataba tutaweka hilo sharti kwamba endapo nitashindwa kulipa bajaji niliyonunua itakuwa Mali yako.
 
Lakini pia kumbuka Bajaji kwasasa inabei ya walau 7milioni.
Na kimahesabu ikiwa utarudisha 40,000 per week.....
Maana yake kwa mwezi utakua unarejesha 160,000........
Hii maana yake kwa mwaka mmoja ambao ni miezi 12, utakua na rejesho la 1,920,000....
Sasa......
Ili uweze rejesha mkopo wako wa approximately 7,000,000/40,000 kila mwezi......
Jibu ni kwamba huo mkopo wa pesa / Bajaji utakuchukua karibu miaka minne ili uwe umekamilisha kuulipa walau 7,680,000/=

Kwa hesabu hii, naomba nibet kwamba hauwezi pata mkopo, labda badilisha heading iwe unaomba msaada ambao utakua ukirejesha walau 40,000 kwa kila wiki
 
Dhamana itakuwa ni bajaji nitakayonunua Mkuu.

Hivyo katika mkataba tutaweka hilo sharti kwamba endapo nitashindwa kulipa bajaji niliyonunua itakuwa Mali yako.
Ebu ngoja niwe msomaji tu hapa, niwapishe na wengine wenye kutazama mambo kwa jicho la tatu
 
Yaani elfu 40 a see aupo serious,.. Boda ni 70 mpaka 100...we ufany bajaj kwa 40!?
 
Aliyeweka thread ana wazo zuri... Ila hapo kwenye kurejesha ndo naona panaleta shida. Mi pia nahitaji connection kama kuna anayejua mahali ambapo naweza nikapewa bajaji kwa mkopo ila nitakuwa narudisha sh 600,000 kwa mwezi. Kama inawezekana kwa kigezo hicho tujulishane. Nipo Iringa.
 
Lakini pia kumbuka Bajaji kwasasa inabei ya walau 7milioni.
Na kimahesabu ikiwa utarudisha 40,000 per week.....
Maana yake kwa mwezi utakua unarejesha 160,000........
Hii maana yake kwa mwaka mmoja ambao ni miezi 12, utakua na rejesho la 1,920,000....
Sasa......
Ili uweze rejesha mkopo wako wa approximately 7,000,000/40,000 kila mwezi......
Jibu ni kwamba huo mkopo wa pesa / Bajaji utakuchukua karibu miaka minne ili uwe umekamilisha kuulipa walau 7,680,000/=

Kwa hesabu hii, naomba nibet kwamba hauwezi pata mkopo, labda badilisha heading iwe unaomba msaada ambao utakua ukirejesha walau 40,000 kwa kila wiki
Nimekuelewa sana Mkuu!

Ila msaada nao kwa maisha haya yaliyokaba mpaka shingoni itawezekana kweli kupata huo msaada?
 
Iko sehemu gani Mkuu?
d6af322f4b908c8e6af325ef35bae957.jpg

Iko sehemu gani Mkuu?
 
S
Lakini pia kumbuka Bajaji kwasasa inabei ya walau 7milioni.
Na kimahesabu ikiwa utarudisha 40,000 per week.....
Maana yake kwa mwezi utakua unarejesha 160,000........
Hii maana yake kwa mwaka mmoja ambao ni miezi 12, utakua na rejesho la 1,920,000....
Sasa......
Ili uweze rejesha mkopo wako wa approximately 7,000,000/40,000 kila mwezi......
Jibu ni kwamba huo mkopo wa pesa / Bajaji utakuchukua karibu miaka minne ili uwe umekamilisha kuulipa walau 7,680,000/=

Kwa hesabu hii, naomba nibet kwamba hauwezi pata mkopo, labda badilisha heading iwe unaomba msaada ambao utakua ukirejesha walau 40,000 kwa kila wiki
Sio kweli mkuu,unapotosha hapo
 
Back
Top Bottom