Nahitaji majibu kwa maswali yafuatayo.

Jeho

JF-Expert Member
Jul 2, 2011
5,053
5,503
Kwa muda mrefu, kumekuwepo na hoja kutoka kwa baadhi ya watu kuwa dini tunazozifuata ni matokeo ya kuletwa na meli, na hivyo wanadai kuwa kuzifuata ni sawa na kuwa mtumwa kwa waliozileta. Nina maswali kidogo kwa watu wanaodai hivyo. Na bila shaka wanapotoa madai hayo, wanatoa kutokana na kwamba ni watu wenye elimu, walioelimishwa vizuri darasani, sasa
1. Je, elimu tunayotumia hapa Tanzania, yenyewe haikuletwa kwa meli? Na je, lengo lake nayo haikuwa kulahisisha utawala kwa wakoloni kama wanavyodai kuwa dini zilikuwa chambo cha kurahisisha utawala wa kikoloni?.
2. Nguo tunazotumia, je kwa mara ya kwanza zilivumbuliwa Afrika? Je, kabla ya wenye meli kuja, hatukuwa na mavazi yetu? Mbona hata leo hii kuna baadhi ya nguo kama vile suti zinaagizwa hukohuko kwa waliotuletea dini kwa meli?.
3. Wale wanaodai kuwa Mungu hayupo(Atheists), je ni watanzania ndio walioibua hoja za kuwa Mungu hayupo? Au nadharia za kuwa Mungu hayupo nazo chanzo chake sio kwa waliotuletea dini kwa meli?.
4. Simu, kompyuta, gari na teknolojia nyingine nyingi, zenyewe zilianzishwa hapa Afrika? Au na zenyewe zililetwa kwa meli?.
5. Yapo mambo mengine mengi tunayoyafuata na chanzo chake ni ulaya, mfano mpira, n.k
Je, kuyafuata hayo nayo ni utumwa kama wanavyodai kuwa kufuata dini ni utumwa tulioachiwa na wazungu? Kwa nini kama hatutaki mambo yaliyoletwa na wazungu, tusiwe na mambo yetu wenyewe yaliyo tofauti na wao. Nawasilisha hoja.
 
Jibu ni ndio. Sababu ni kuwa tumedumazwa akili na kuona kila kitu chetu ni cha kipuuzi. kama tumelogwa vile.

Miafrika ndivyo tulivyo, source Nyani Ngabu
 
Last edited by a moderator:
Kwa muda mrefu,
kumekuwepo na hoja kutoka kwa baadhi ya watu kuwa dini tunazozifuata ni
matokeo ya kuletwa na meli, na hivyo wanadai kuwa kuzifuata ni sawa na
kuwa mtumwa kwa waliozileta. Nina maswali kidogo kwa watu wanaodai
hivyo. Na bila shaka wanapotoa madai hayo, wanatoa kutokana na kwamba ni
watu wenye elimu, walioelimishwa vizuri darasani, sasa
1. Je, elimu tunayotumia hapa Tanzania, yenyewe haikuletwa kwa
meli? Na je, lengo lake nayo haikuwa kulahisisha utawala kwa wakoloni
kama wanavyodai kuwa dini zilikuwa chambo cha kurahisisha utawala wa
kikoloni?.
2. Nguo tunazotumia, je kwa mara ya kwanza zilivumbuliwa Afrika?
Je, kabla ya wenye meli kuja, hatukuwa na mavazi yetu? Mbona hata leo
hii kuna baadhi ya nguo kama vile suti zinaagizwa hukohuko kwa
waliotuletea dini kwa meli?.
3. Wale wanaodai kuwa Mungu hayupo(Atheists), je ni watanzania
ndio walioibua hoja za kuwa Mungu hayupo? Au nadharia za kuwa Mungu
hayupo nazo chanzo chake sio kwa waliotuletea dini kwa meli?.
4. Simu, kompyuta, gari na teknolojia nyingine nyingi, zenyewe
zilianzishwa hapa Afrika? Au na zenyewe zililetwa kwa meli?.
5. Yapo mambo mengine mengi tunayoyafuata na chanzo chake ni
ulaya, mfano mpira, n.k
Je, kuyafuata hayo nayo ni utumwa kama wanavyodai kuwa kufuata dini ni
utumwa tulioachiwa na wazungu? Kwa nini kama hatutaki mambo yaliyoletwa
na wazungu, tusiwe na mambo yetu wenyewe yaliyo tofauti na wao.
Nawasilisha hoja.

Oops!
Swali Na. 3 sijuhi kama akina Kiranga na wenzake (Atheists) wanaweza kuleta majibu sahihi hapa.
 
Last edited by a moderator:
Imani ni nguvu itokayo moyoni mwa binadamu ambayo bila kujali kama ni mapokeo yeye hupigia muhuri kile aaminicho. Naomba kukuambia kuwa ni kweli MUNGU yuko.
 
Elimu na dini vilikuja na malengo mazuri tu,sema ktk nyakati hizo za ukoloni basi mabepari walitumia kama nguzo za kufanikisha matakwa yao yakikoloni. Ni kam CCM ya hayati nyerere kilikuwa ni chama cha wafanyakazi na wakulima.sasa hivi kinatumiwa na vibepari ukwara vya kihindi na kiarabu na vibaraka weusi na sasa kime kuwa chama cha mafisadi ma maharamia
 
Oops!
Swali Na. 3 sijuhi kama akina Kiranga na wenzake (Atheists) wanaweza kuleta majibu sahihi hapa.

Tanzania imeanza 1964, mababu zangu waliokuwa pantheists hawakuwa Watanzania. Mkwawa hakuwa Mtanzania.Tanzania yenyewe - kwa maana ya mipaka iliyo define mwanzo na mwisho wa Tanzania- imeletwa na wageni. Anayebeza vilivyoletwa na wageni kwa kuipaza Tanzania ana ji contradict.

Katafuteni speech ya Nyerere aliyoitoa bunge la South Africa muone huyo aliyeiasisi Tanzania mwenyewe kaipondaje in the light of bigger ideals.

What are you guys trying to say here?

Na what does it matter kama kitu kimeletwa na wageni - not that there is conclusive evidence that an indigenous African atheism did not exist, some forms of ancestor worship/ reverence are more atheism than theism - au hakijaletwa? I should think kwamba kinacho matter si kimeletwa na nani, bali ni kizuri au kibaya.

Umeme umeletwa na wageni, lakini hatuukatai kwa sababu umeletwa na wageni, tunaukubali kwa sababu ni kitu kizuri kwa maendeleo yetu.

Internet imeletwa na wageni, mbona hamuikatai nayo, mmeishia kutwa kucha kushinda JF?
 
Bwana Kiranga, unaweza kutueleza kwa kina hiyo existence ya pantheism, origin yake ilikuwa wapi hapa Afrika? Maana katika dini inajulikana mwanzo wa imani juu ya Mungu, na hata mwanzo wa mwanadamu.
 
Last edited by a moderator:
Bwana Kiranga, unaweza kutueleza kwa kina hiyo existence ya pantheism, origin yake ilikuwa wapi hapa Afrika? Maana katika dini inajulikana mwanzo wa imani juu ya Mungu, na hata mwanzo wa mwanadamu.

Kwanza kabla ya kukujibu swali lako, unaelewa pantheism ni nini?

Pantheism has been practiced in Africa since prehistoric times. Check the history of the Ashanti, check John Mbiti.

Na unapoandika "Maana katika dini inajulikana mwanzo wa imani juu ya Mungu, na hata mwanzo wa mwanadamu" unakusudia dini gani?

Unajua kuna dini nyingine zinasema hakuna mungu, na mwanadamu hana mwanzo, anazunguka katika mduara wa maisha tu?

Sasa kabla ya kusema "kwenye dini hivi na vile" kama vile dini zote zinasema kimoja, fafanua unamaanisha dini gani.

Mwanzo wa imani juu ya mungu ni lini? Kwa mujibu gani?
 
Nikiri kwa kauli ya "dini zote" niloyoitumia, nimekuwa too general badala ya kuwa specific, maswali yangu ya kwanza kumbuka yalilenga katika dini zinazodaiwa kuletwa kwa meli. Sasa ngoja nijikite katika dini ninayoijua yaani ukristo. Ukirejea ndani ya Biblia katika kitabu cha Mhubiri sura ya 3 mstari wa 11, ambayo inasomeka hivi "kila kitu amekifanya kizuri kwa wakati wake, tena ameiweka hiyo milele mfano ya mioyo yao; ila kwa jinsi mwanadamu asivyoweza kuivumbua kazi ya Mungu anayoifanya, tangu mwanzo hadi mwisho". Kumbe hali ya umilele aliumbwa nayo mwanadamu na akawekewa nia ya kumjua Mungu lakini si kwa undani zaidi, yaani tunapapasa kuhusu Mungu. Na ndio maana wakati mwingine tunapofichwa kuhusu Mungu, wanadamu tumekuwa tunatafuta kitu mbadala cha kukiabudu kama Mungu, hapo ndipo mungu jua, mwezi na kila namna ya miungu uliyopata kuisikia ilipoanza. Na hata hao unaodai pantheists kuwa wali exist tokea prehistoric nao walianza kuabudu kile walichoabudu baada ya kufichwa kuhusu Mungu wa kweli. Na ndio maana hata hao atheist hawakuibua tu hoja kuwa hakuna Mungu, bila kwanza ya kumuwaza huyo Mungu, na pale waliposhindwa kufahamu kwa undani kumhusu Mungu kwa sababu hajajifunua kwetu kwa namna yote, ndipo walipotoka na conclusion kuwa hakuna Mungu. So even the pantheism belief existed as a result of seeking something to worship as god. Karibu bwana Kiranga kwa chochote.
 
Last edited by a moderator:
Nikiri kwa kauli ya "dini zote" niloyoitumia, nimekuwa too general badala ya kuwa specific, maswali yangu ya kwanza kumbuka yalilenga katika dini zinazodaiwa kuletwa kwa meli. Sasa ngoja nijikite katika dini ninayoijua yaani ukristo. Ukirejea ndani ya Biblia katika kitabu cha Mhubiri sura ya 3 mstari wa 11, ambayo inasomeka hivi "kila kitu amekifanya kizuri kwa wakati wake, tena ameiweka hiyo milele mfano ya mioyo yao; ila kwa jinsi mwanadamu asivyoweza kuivumbua kazi ya Mungu anayoifanya, tangu mwanzo hadi mwisho". Kumbe hali ya umilele aliumbwa nayo mwanadamu na akawekewa nia ya kumjua Mungu lakini si kwa undani zaidi, yaani tunapapasa kuhusu Mungu. Na ndio maana wakati mwingine tunapofichwa kuhusu Mungu, wanadamu tumekuwa tunatafuta kitu mbadala cha kukiabudu kama Mungu, hapo ndipo mungu jua, mwezi na kila namna ya miungu uliyopata kuisikia ilipoanza. Na hata hao unaodai pantheists kuwa wali exist tokea prehistoric nao walianza kuabudu kile walichoabudu baada ya kufichwa kuhusu Mungu wa kweli. Na ndio maana hata hao atheist hawakuibua tu hoja kuwa hakuna Mungu, bila kwanza ya kumuwaza huyo Mungu, na pale waliposhindwa kufahamu kwa undani kumhusu Mungu kwa sababu hajajifunua kwetu kwa namna yote, ndipo walipotoka na conclusion kuwa hakuna Mungu. So even the pantheism belief existed as a result of seeking something to worship as god. Karibu bwana Kiranga kwa chochote.

Kwa nini mungu muweza yote, mjuzi wa yote na mwenye upendo wote ajifiche kutoka kutaka kujulikana kwa uhakika wanakokufanya wanadamu?

Kwa nini mungu awe ni kitu cha kuamini, na si kitu cha kujua?
 
Tanzania imeanza 1964, mababu zangu waliokuwa pantheists hawakuwa Watanzania. Mkwawa hakuwa Mtanzania.Tanzania yenyewe - kwa maana ya mipaka iliyo define mwanzo na mwisho wa Tanzania- imeletwa na wageni. Anayebeza vilivyoletwa na wageni kwa kuipaza Tanzania ana ji contradict.

Katafuteni speech ya Nyerere aliyoitoa bunge la South Africa muone huyo aliyeiasisi Tanzania mwenyewe kaipondaje in the light of bigger ideals.

What are you guys trying to say here?

Na what does it matter kama kitu kimeletwa na wageni - not that there is conclusive evidence that an indigenous African atheism did not exist, some forms of ancestor worship/ reverence are more atheism than theism - au hakijaletwa? I should think kwamba kinacho matter si kimeletwa na nani, bali ni kizuri au kibaya.

Umeme umeletwa na wageni, lakini hatuukatai kwa sababu umeletwa na wageni, tunaukubali kwa sababu ni kitu kizuri kwa maendeleo yetu.

Internet imeletwa na wageni, mbona hamuikatai nayo, mmeishia kutwa kucha kushinda JF?

100/100.

We do not live in the world of nations any more

We live in the world of business... so as Relig...

Atheism is a non-prophet organization.
George Carlin

 
Kwa nini mungu muweza yote, mjuzi wa yote na mwenye upendo wote ajifiche kutoka kutaka kujulikana kwa uhakika wanakokufanya wanadamu?

Kwa nini mungu awe ni kitu cha kuamini, na si kitu cha kujua?
Asante kwa maswali mazuri, nami nikujibu kama ifuatavyo.
Ukweli ni kwamba, Mungu hajajificha, kilichotokea hadi Mungu akawa haonekani kwa wanadamu na hivyo kupelekea kujulikana kwa kina kuwe kugumu ni huku kufuatako Kisha wakasikia sauti ya BWANA Mungu, akitembea bustanini wakati wa jua kupunga; Adamu na mkewe wakajificha kati ya miti ya bustani, BWANA Mungu asiwaone(Mwanzo 3:8), hapa mwanadamu ndiye ambaye alianza kujificha na wakati akitafuta kujificha Mungu alikuwa bado anahitaji kuwa karibu naye. Kilichotokea ni sawa na motto amekosa mbele ya baba, huwa hata wakati mwingine anaweza atoroke nyumbani maana anahisi kwa kosa alilofanya atapata adhabu kubwa. Na kumbe basi kilichosababisha Mungu asionekane ni hiki kifuatacho lakini maovu yenu yamewafarikisha ninyi na Mungu wenu, na dhambi zenuzimeuficha uso wake msiuone, hata hataki kusikia(Isaya 59:2), labda swali hapa ni kwa nini basi dhambi za wanadamu zimeuficha uso wa Mungu kwa wanadamu? Sababu ni hii hutaniona uso wangu, maana mwanadamu hataniona akaishi(Kutoka 33:20), kumbe kinachofanya Mungu asionekane kwa wanadamu ni kwa kuwa wanadamu tumetenda dhambi, na ndio maana hata mtu akitenda dhambi leo hii atafanya hivi maana kila mtu atendaye mabaya huichukia nuru, wala haji kwenye nuru, matendo yake yasije yakakemewa(Yohana 3:20).
 
Asante kwa maswali mazuri, nami nikujibu kama ifuatavyo.
Ukweli ni kwamba, Mungu hajajificha, kilichotokea hadi Mungu akawa haonekani kwa wanadamu na hivyo kupelekea kujulikana kwa kina kuwe kugumu ni huku kufuatako Kisha wakasikia sauti ya BWANA Mungu, akitembea bustanini wakati wa jua kupunga; Adamu na mkewe wakajificha kati ya miti ya bustani, BWANA Mungu asiwaone(Mwanzo 3:8), hapa mwanadamu ndiye ambaye alianza kujificha na wakati akitafuta kujificha Mungu alikuwa bado anahitaji kuwa karibu naye. Kilichotokea ni sawa na motto amekosa mbele ya baba, huwa hata wakati mwingine anaweza atoroke nyumbani maana anahisi kwa kosa alilofanya atapata adhabu kubwa. Na kumbe basi kilichosababisha Mungu asionekane ni hiki kifuatacho lakini maovu yenu yamewafarikisha ninyi na Mungu wenu, na dhambi zenuzimeuficha uso wake msiuone, hata hataki kusikia(Isaya 59:2), labda swali hapa ni kwa nini basi dhambi za wanadamu zimeuficha uso wa Mungu kwa wanadamu? Sababu ni hii hutaniona uso wangu, maana mwanadamu hataniona akaishi(Kutoka 33:20), kumbe kinachofanya Mungu asionekane kwa wanadamu ni kwa kuwa wanadamu tumetenda dhambi, na ndio maana hata mtu akitenda dhambi leo hii atafanya hivi maana kila mtu atendaye mabaya huichukia nuru, wala haji kwenye nuru, matendo yake yasije yakakemewa(Yohana 3:20).

Kwa nini mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na mapenzi yote, anayeweza kuumba ulimwengu wa aina yoyote, aumbe ulimwengu huu ambayo mabaya yanawezekana?
 
Bwana Kiranga, unapoandika mungu unamaanisha Mungu? Maana unayemuandika si mjuzi wa yote, mjuzi wa yote ni Mungu.
 
Last edited by a moderator:
Jibu lako linajibika vizuri sana, shida ni kwamba mungu ni tofauti na Mungu. Ukiwa specific anahitaji majibu kwa yupi, kati ya mungu ama Mungu itapendeza zaidi.
 
Kwa nini mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na mapenzi yote, anayeweza kuumba ulimwengu wa aina yoyote, aumbe ulimwengu huu ambayo mabaya yanawezekana?

bado somo ni refu Mungu angeamua kila mtu asitende zambi hakuna ambaye angetenda ila alikupa uwezo wa kutambua jema na baya na hivyo akatupa uhuru wa kuchagua wapi pa kwenda kumfata yeye au kwa ibilisi. kwa sisi tulioshika njia yake tuna ushaidi wa kutosha ya kwamba Mungu yupo. sijui nimeeleweka mkuu?
 
Wanadamu hua tuna tabia ya kujisahau na kujiropokea hasa MwenyeziMungu anapotupa uzima wa afya.
 
Back
Top Bottom