Nahitaji kusafirisha pikipiki yangu kutoka Dar kwenda Karatu

Badru26

Member
Oct 3, 2017
47
17
Je, usafiri gan utakuwa mzuri zaidi na wa bei nafuu kusafirisha pikipiki kutokea Dar kwenda Karatu?
 
Malori ya Mizigo yanayorudi Baada ya kupeleka Mizigo hasa ya mazao Dar.

Yanaondokaga jioni, kwahio ukipakia leo Tafuta mtu akupokelee kesho asubuhi au waambie wasafirishe kesho upokee mwenyewe keshokutwa...

Piga picha risiti ya manunuzi na documents zote muhimu, waachie na hakikisha wamekupa risiti ya usafirishaji.
 
Niliwahi kisafirisha kwa bus japo kuna changamoto ya kuikubali maana hairuhusiwi bus kubeba ila malori ndiyo kazi yake.

But kwanza nilienda ubungo kufanya research kama kuna uwezekano na baadaye nilifanikiwa kuipeleka ubungo kwenda namanga, ila wanamwaga mafuta na unawakabidhi documents zote muhimu za pikipiki kwa ajili ya njiani kukitokea tatizo.

Nadhani jamaa aliyenisafilishia bado yupo pale ubungo.
Garama ilifika elfu50.
 
Ukipakia kwenye gari za mizgo itafka karutu si chini ya wiki hiyo...labda ubahatike upate gari linalotoka siku hiyohiyo hata hivyo utapokea baada ya siku 2 kupita
 
Tafuta demu mkali akae nyuma ya bodaboda endesha chombo siku ya pili jioni unaingia Karatu na bodaboda yako huku umebeba kipozeo,safari hutachoka maana ni safari na muziki.
 
Tafuta demu mkali akae nyuma ya bodaboda endesha chombo siku ya pili jioni unaingia Karatu na bodaboda yako huku umebeba kipozeo,safari hutachoka maana ni safari na muziki.
Tembeza chombo mpk karatu
Mkuu nipe niiendeshe Hadi karatu kwa gharama ya Elfu 60 ila mafuta utaweka wewe full tenki
Weka kwenye road machine hiyo inafika bila shida
Korona imeathiri akili za watu.
 
unatembea tu..
jana nmefka mbeya nikitokea kyaka-kagera via dom iringa zaid ya km 1700.
cha msingi tafuta koti zako kama 3 nzuri,vaa gloves,tafuta helmet ya kioo..
tembea na constant speed utakayochagua wewe.
tembea muda ambao unakuwa umeyaacha au upo nyuma ya mabasi ya dar.Madereva wa mabasi baadhi wana fujo. Malori usiyaogope madereva wako poa.
uwe na maji ya kunywa plus energy drink.ukijihisi uchov cmamisha chombo nyoosha miguu.
utafika tu usiogope wala wasikuogopesha.
hakikisha chombo umeifanyia service nzur
 
Back
Top Bottom